Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. KHATIB SAID HAJI) aliuliza:- Kumekuwa na mfululizo wa migomo, misuguano na migongano ya mara kwa mara kwa wafanyakazi wa viwandani na Kampuni binafsi zinazotokana na malalamiko ya mishahara na maslahi ya wafanyakazi:- Je, ni mfumo upi na viwango gani vilivyowekwa kisheria wanavyotakiwa kulipwa wafanyakazi wa viwanda na Kampuni binafsi?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, kwa kuwa kiwango hicho ni kidogo ambacho kinapelekea hata nauli; kwa mfano, hata katika mabasi ya mwendo kasi ukipiga hesabu hayamtoshelezi huyu mfanyakazi; hawaoni sasa wafanyakazi hawatafanya kazi kwa moyo na tija kwa sababu ya mshahara mdogo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kuna wenzetu wawekeza wa nje hasa Wachina wameingia, wanafanya kazi ambazo Watanzania wanazifanya, tena kwa bei nafuu; sasa Serikali haioni ni wakati wa kuwabana kuhakikisha kwamba zile shughuli zinazoweza kufanywa na Watanzania zifanywe na Watanzania badala ya wawekezaji wanaouza mpaka vocha ambao wameshaingia nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA, NA WENYE ULEMAVU – MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza Mheshimiwa Mbunge amehoji juu ya viwango hivyo kwamba ni vidogo na katika jibu langu la msingi nimeeleza vyema ya kwamba, Serikali kila baada ya miaka mitatu kupitia Waziri mwenye dhamana, amekuwa akitoa kitu kinaitwa wage order. Wage order ndiyo mshahara wa kima cha chini kwa sekta binafsi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge wage order ya mwaka wa mwisho ilikuwa ni ya mwaka 2013.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sasa hivi tayari Mheshimiwa Waziri ameshaunda Bodi ya watu 17 ambao wanaanza kushughulikia suala hilo la mshahara wa kima cha chini. Bodi hii itafanya uchunguzi kutoka na sekta husika na wataangalia maisha ya leo jinsi yalivyo na gharama zilivyo na baadaye sasa watapendekeza kwa Mheshimiwa Waziri kima kingine cha chini cha mshahara kutokana na sekta.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, napenda kumwambia Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu zoezi hili ndio linaendelea sasa na Mheshimiwa Waziri ameshakamilisha kazi yake, tunasubiri mapendekezo kutoka kwenye Vyama vya Wafanyakazi, Vyama vya Waajiri pamoja na Serikali ili baadaye Mheshimiwa Waziri aweze kutoa amri kwa maana ya order.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nichukuwe fursa hii kuwasisitiza wenzetu wa Vyama vya Wafanyakazi kuhakikisha kwamba wanasimamia majukumu yao ipasavyo ili waendelee kufanya vikao na waajiri ili katika yale ambayo bado wanaweza wakazungumza na waajiri katika kuboresha maslahi ya wafanyakazi, basi wafanye hivyo kwa niaba ya wafanyakazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Mbunge aliuliza kwamba wako wafanyakazi wengi sana wa kigeni ambao wanaendelea kufanya kazi ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2015 Bunge hili lilipitisha Sheria ya Kuratibu Ajira kwa Wageni na ninyi wenyewe ni mashahidi, Serikali kupitia Wizara ya Kazi, tumekuwa tukisimamia sana sheria hii kuhakikisha kwamba zile kazi zote ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania na ambazo zina ujuzi ndani ya nchi hii ziweze kufanywa na Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sisi kama Wizara, tutaendelea kuimarisha kaguzi mbalimbali ili kuwabaini watu wote ambao wanafanya kazi ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania ambapo kwa namna moja ama nyingine kumekuwa kuna tatizo kubwa sana la udanganyifu kwa maana ya kwamba, watu wakiomba vibali wanadanganya nafasi anayokuwa, lakini baadaye unakuta amechukua nafasi ambazo zinaweza zikafanywa na Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sisi kama Serikali tutahakikisha kwamba tunaimarisha ukaguzi ili jambo hili lisiendelee kuwepo na tumekuwa tukichukuwa hatua stahiki pale inapobainika.

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. KHATIB SAID HAJI) aliuliza:- Kumekuwa na mfululizo wa migomo, misuguano na migongano ya mara kwa mara kwa wafanyakazi wa viwandani na Kampuni binafsi zinazotokana na malalamiko ya mishahara na maslahi ya wafanyakazi:- Je, ni mfumo upi na viwango gani vilivyowekwa kisheria wanavyotakiwa kulipwa wafanyakazi wa viwanda na Kampuni binafsi?

Supplementary Question 2

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mbali na matatizo ya mishahara kwa wafanyakazi wengi wa viwandani, lakini pia kuna tatizo moja sugu la ukatiwaji wa bima, yaani wafanyakati wa viwandani kupatiwa bima. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuvilazimisha viwanda viwakatie bima za maisha wafanyakazi wao?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA, NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa Serikali imegundua kwamba yapo matatizo ya namna mbalimbali ambayo wafanyakazi wanatakiwa wahifadhiwe kwa kufuata mifumo inayotakiwa katika nchi yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua tatizo hilo, Serikali imeanzisha ule Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi na baada ya kuanzisha mfuko huo na kuwalazimisha waajiri watii takwa la kisheria la luchangia mfuko huo, sasa tunauhakika na ninaomba niwahakikishie wafanyakazi watulie kwa sababu sasa Serikali itakuwa ikiwafidia kupitia kwenye mfuko huo ambao umeanzishwa na Serikali na sisi tutaendelea kuusimamia kuhakikisha wafanyakazi wanafidiwa katika viwango vinavyostahiki kulingana na sheria ilivyo na namna mbalimbali ambazo zitakuwa zimetokea katika sekta zao za kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Serikali imelisimamia hilo na tutaendelea kulifanyia kazi vizuri.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. KHATIB SAID HAJI) aliuliza:- Kumekuwa na mfululizo wa migomo, misuguano na migongano ya mara kwa mara kwa wafanyakazi wa viwandani na Kampuni binafsi zinazotokana na malalamiko ya mishahara na maslahi ya wafanyakazi:- Je, ni mfumo upi na viwango gani vilivyowekwa kisheria wanavyotakiwa kulipwa wafanyakazi wa viwanda na Kampuni binafsi?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika Jimbo langu la Mkuranga liko tatizo la wafanyakazi wanaofanya kazi katika viwanda hivyo vya Wachina, kulipwa malipo madogo kwa muda mrefu wa kazi. (Makofi)
Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kuja Mkuranga kuonana na vijana wale wanaofanya kazi katika viwanda vile na kuzungumza nao na hatimaye kuweza kuwapa matokeo ya kuweza kuwasaidia kama Serikali?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA, NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ulega (Baba Tulia) kama ifuatavyo:- (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Ulega, ni kweli amewaleta hao wafanyakazi mpaka ofisini kwangu na anafuatalia sana suala hilo. Nami kama Waziri, naomba nimhakikishie kwamba tutampa ushirikiano. Tutaangalia Sheria inataka nini na hao wawekezaji ni kwa kiasi gani wanavunja sheria ambazo ziko katika nchi yetu, basi ninathubutu kusema kwamba nitaongozana na Mheshimiwa Ulega (Baba Tulia) kwenda katika maeneo hayo anayoyasema na tutapanga utaratibu. Ila tu tutamwomba mtoto Tulia asiingilie utaratibu wa ziara yangu na Mheshimiwa Ulega kwenda kuangalia matatizo hayo.