Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Mji wa Mpwapwa wenye wakazi zaidi ya 41,000 unakabiliwa na tatizo kubwa sana la maji, ambapo wananchi wanapata shida kubwa sana kutembea mwendo mrefu zaidi ya kilometa tano kufuata huduma ya maji; na kuna baadhi ya mitambo imeharibika na Mamlaka ya Maji Safi na Salama hawana fedha za kukarabati mitambo hiyo. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja kubwa ya kusaidia ukarabati wa mitambo hiyo ili wananchi wa Mji wa Mpwapwa na vitongoji vyake waweze kupata huduma ya maji karibu na makazi yao?

Supplementary Question 1

Kwanza ninamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ni kweli mitambo imekarabatiwa, lakini bado huduma ya maji haiwafikii wananchi wa vijiji vya Ving‟awe namba 30, Mbuyuni, Ving‟awe Juu, Ilolo, Kwa Mshangu, Mahang‟u na Ising‟u; kwa hiyo nilikuwa nakupa taarifa tu kwamba maji hayafiki kule.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kwamba kuna vijiji ambavyo hakuna uwezekano mwingine wa kupata chanzo cha maji ni kuchimba visima. Sasa naiomba Serikali, kwa vijiji nitakavyovitaja iwachimbie visima ili waweze kupata huduma ya maji. Kwanza Ngalamilo, Mgoma, Mzogole, Kisisi, Godegode, Mkanana, Chamanda, Lupeta, Makutupa, Nana, Simai, Isalaza, Nzonvu pamoja na Iwondo. Naomba sana wananchi hawa wana shida kubwa sana ya maji Serikali iwasaidie. Je, Waziri unasemaje kuhusu hilo.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Lubeleje babu yangu gereda la zamani huyu, lakini makali ni yale yale, anafanya kazi nzuri sana kwa wananchi wa Jimbo la Mpwapwa.
Mheshimiwa Naibu Spika nikupe taarifa tu kwamba, wiki mbili zilizopita Mheshimiwa Lubeleje, aliondoka na Waziri wangu kwenda Mpwapwa kwenda kuangalia ukarabati wa hizo starter na sasa hivi kwa kweli Mpwapwa maji yanapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vijiji bado havifikiwi na hayo maji, katika jibu langu la msingi nimesema kwamba Serikali itaendelea kufanya matengenezo na nimuahidi kwenye awamu ya pili ya program ya maendeleo ya maji, tutahakikisha kwamba Mpwapwa tunahakikisha vijiji vyote vinafikiwa na maji. Swali hapa muhimu ilikuwa ni kuna vijiji kwa sababu Mpwapwa ni kubwa, kuna vijiji ambavyo bado havijapata huduma ya maji yenye mfumo na ameomba kwamba tuchimbe visima.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu yangu na Babu yangu Mheshimiwa Lubeleje katika Bajeti ya mwaka huu, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa tumetenga zaidi ya shilingi bilioni 1.58 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kipaumbele. Kwa hiyo, nikuombe ushirikiane na Halmashauri yako kuhakikisha hivi vijiji, basi mnafanya study na mnachimba visima ili mwaka wa fedha utakaofuata, tuendelee kutoa hela kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata huduma ya maji, kwa maana ya kuchimba visima; lakini ikiwa ni pamoja na kujenga mabwawa ili tuwe na uhakika wa maji katika maeneo ya Mpwapwa.

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Mji wa Mpwapwa wenye wakazi zaidi ya 41,000 unakabiliwa na tatizo kubwa sana la maji, ambapo wananchi wanapata shida kubwa sana kutembea mwendo mrefu zaidi ya kilometa tano kufuata huduma ya maji; na kuna baadhi ya mitambo imeharibika na Mamlaka ya Maji Safi na Salama hawana fedha za kukarabati mitambo hiyo. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja kubwa ya kusaidia ukarabati wa mitambo hiyo ili wananchi wa Mji wa Mpwapwa na vitongoji vyake waweze kupata huduma ya maji karibu na makazi yao?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona, naomba na mimi niulize swali dogo la nyongeza;
Kwa kuwa, Mji wa Manyoni ni mkongwe ni sawa na ule wa Mpwapwa na matatizo ni makubwa, mitambo ya maji iliyopo sasa hivi imezeeka sana. Sasa hivi inakisiwa kwamba asilimia 35 tu ya wananchi wa Manyoni ndiyo wanapata maji na asilimia 65 hawapati maji;
Je, Serikali inatoa kauli gani ya matumaini kwa wananchi wa ule Mji wa Manyoni Mjini, kwa sababu shida ya maji ni kubwa. Maeneo ya Sayuni, Mwanzi, Kipondoda, Mgulang‟ombe, Mwembeni, Manyoni Mjini, Majengo hali ni mbaya akina mama wanapata shida sana, Serikali ina kauli gani kuhusu shida hii ya maji katika Mji wa Manyoni. Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIJAI: Mheshimiwa Naibu Spika, tumeishaelekeza kwamba sasa hivi katika awamu ya pili ya program ya maendeleo ya maji, tutahakikisha kwamba miundombinu ya zamani inafanyiwa utafiti, tunatoa fedha na tunakarabati ili mfumo wa maji ule uweze kuendelea. Pamoja na kukarabati tutapanua kwa sababu katika hayo maeneo kwa mfano, kama mtambo ulijengwa muda mrefu miaka ya 1960 au 1970 wakati ule wananchi walikuwa ni wachache, sasa hivi wananchi wameongezeka, huduma za binadamu vilevile zimeongezeka kwa hiyo mahitaji ya maji yameongezeka. Hivyo, pamoja na kukarabati hiyo mifumo tutahakikisha tunaipanua ili kuhakikisha kwamba huduma ya maji inakuwa ya kutosheleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba Mheshimiwa Mbunge tushirikiane pamoja na Halmashauri yako, ikiwa ni pamoja na kufanya utafiti wa kuchimba mabwawa. Kama vile Itigi Serikali imekamilisha bwawa na ninayo taarifa bwawa hilo linavuja na nimeishaelekeza kwamba wataalam waende kuhakikisha wanaziba ili tuwe na maji ya kutosha.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Mji wa Mpwapwa wenye wakazi zaidi ya 41,000 unakabiliwa na tatizo kubwa sana la maji, ambapo wananchi wanapata shida kubwa sana kutembea mwendo mrefu zaidi ya kilometa tano kufuata huduma ya maji; na kuna baadhi ya mitambo imeharibika na Mamlaka ya Maji Safi na Salama hawana fedha za kukarabati mitambo hiyo. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja kubwa ya kusaidia ukarabati wa mitambo hiyo ili wananchi wa Mji wa Mpwapwa na vitongoji vyake waweze kupata huduma ya maji karibu na makazi yao?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Kwa kuwa, matatizo yaliyoko Mpwapwa yanafanana sana na matatizo yaliyopo katika Jimbo langu la Itigi. Watu wanaenda kilometa nyingi sana kufuata maji hasa katika vijiji vya Rungwa, Kintanula, Kalangali, Mitundu, Chabutwa na Mabondeni;
Je, Serikali itasaidiaje kutatua tatizo hili katika Jimbo la Manyoni Magharibi;

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekamilisha program ya utekelezaji wa maendeleo ya maji, iliyodumu kuanzia mwaka 2006/2007 mpaka 2015. Sasa hivi tumeingia katika program ya pili. Huu ni mwendelezo wa kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wanapata huduma ya maji iliyo safi na bora, na kusogeza huduma ya maji iwe karibu ili akina mama wasitumie muda mrefu kupata maji.
Mheshimiwa Yahaya Masare nikuhakikishie kwamba tunaendelea na kama ambavyo umeona katika Bajeti ya mwaka huu tumehakikisha kwamba kila Halmashauri imetengewa fedha, tutaendelea kupeleka wataalam na tutasimamia tuhakikishe kwamba fedha hii inatumika. Sheria ndogo ndogo imepitishwa tumeweka value for money, tuhakikishe kwamba hela iliyopelekwa inafanya kazi nzuri na kuhakikisha wananchi wanapata maji.
Hivyo, nikuhakikishie kwamba tutatenga fedha kila mwaka, kuhakikisha kwamba wananchi wako wa maeneo hayo mpaka ya Rungwa wanapata maji.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Mji wa Mpwapwa wenye wakazi zaidi ya 41,000 unakabiliwa na tatizo kubwa sana la maji, ambapo wananchi wanapata shida kubwa sana kutembea mwendo mrefu zaidi ya kilometa tano kufuata huduma ya maji; na kuna baadhi ya mitambo imeharibika na Mamlaka ya Maji Safi na Salama hawana fedha za kukarabati mitambo hiyo. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja kubwa ya kusaidia ukarabati wa mitambo hiyo ili wananchi wa Mji wa Mpwapwa na vitongoji vyake waweze kupata huduma ya maji karibu na makazi yao?

Supplementary Question 4

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii.
Matatizo ya Mamlaka ya Maji ya Mji wa Mpwapwa yanafanana na matatizo ya Mamlaka ya maji ya Mji wa Mwanuhuzi. Mradi wa Mamlaka ya Maji ya Mji wa Mwanuhuzi ulikamilishwa mwaka 2009 na ukakabidhiwa katika Mamlaka ya Maji Mwanuhuzi. Mradi huu ulilenga kusambaza maji katika vijiji Nane lakini ni vijiji Vitatu tu vilisambaziwa maji; na kusababisha qubic mita za ujazo wa maji, ambayo yanatumika ni moja ya tatu tu, na hivyo gharama ya uendeshaji katika Mamlaka ya maji kuwa juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilishiriki katika Bajeti ya mwaka huu...
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa, naomba uulize swali tafadhali.
MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri haikuwa na fedha kwa ajili ya upanuzi wa mradi huu, kwa sababu fedha iliyokuwepo ilikuwa ni kwa ajili ya Mkandarasi mshauri wa vijiji 10;
Je, Serikali ina utaratibu gani wa kusambaza maji katika vijiji vilivyobaki vya Bulyanaga, Mwambegwa, Mwagwila, na Mwambiti ili wananchi waweze kunufaika na mradi huu.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze yeye ni Mama anajua matatizo ya maji, kwa hiyo ufuatiliaji wake ni kwamba unamgusa moja kwa moja. Ametoa taarifa kwamba kuna mradi ulikamilika lakini umehudumia vijiji vichache. Mheshimiwa Leah Komanya, naomba sana ushirikiane na Halmashauri; kwa sababu mwaka huu tumetenga fedha kwa kila Halmashauri, kuhakikisha kwamba hayo maeneo ya vijiji yaliyokuwa yamekosa kupata maji basi muhakikishe kwamba nayo yanapata maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, na kama kuna tatizo la utaalam, Mheshimiwa Komanya, naomba utakapokuwa umefika kule na mmepata shida ya wataalam basi tuwasiliane ili tuweze kushirikiana kuleta wataalam atuweze kufikisha huduma hiyo hapo. Suala la nyongeza ni kwamba hii Mwanuhuzi iko Mkowa wa Simiyu, na Mkoa wa Simiyu tuna mradi mkubwa ambao utachukua maji kutoka ziwa Victoria, usanifu sasa umekamilika; na wakati wowote tutakamilisha taratibu ili kuhakikisha kwamba Mkoa wote wa Simiyu sasa tatizo la maji tunaliondoa.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Mji wa Mpwapwa wenye wakazi zaidi ya 41,000 unakabiliwa na tatizo kubwa sana la maji, ambapo wananchi wanapata shida kubwa sana kutembea mwendo mrefu zaidi ya kilometa tano kufuata huduma ya maji; na kuna baadhi ya mitambo imeharibika na Mamlaka ya Maji Safi na Salama hawana fedha za kukarabati mitambo hiyo. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja kubwa ya kusaidia ukarabati wa mitambo hiyo ili wananchi wa Mji wa Mpwapwa na vitongoji vyake waweze kupata huduma ya maji karibu na makazi yao?

Supplementary Question 5

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa sababu tatizo la Mpwapwa linalingana kabisa na tatizo kubwa la Makambako. Mji wa Makambako una wakazi wengi zaidi ya laki moja, na tatizo la maji ni kubwa sana. Wananchi wa Mji wa Makambako alipopita Mheshimiwa Dkt. Magufuli kipenzi chao na kipenzi cha watanzania, walimueleza tatizo la maji katika Mji wa Makambako, kuna mradi ambao ulishasanifiwa wenye gharama ya zaidi ya bilioni 57, na Waziri wa Maji ambaye yupo sasa alikuwepo siku hiyo wakati anaahidi.
Je, sasa tatizo hili la mradi mkubwa wa bilioni 57 litatatuliwa lini ili wananchi wa Makambako waendelee kupata maji.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Sanga kwa ufuatiliaji wake. Maana yake pamoja na kufuatilia miradi midogo midogo ya Halmashauri ya Makambako, lakini bado kumbe amesoma na nyaraka za mradi mkubwa unaolenga kutoa maji Mto Tagamenda, kuhakikisha kwamba maji yanapatikana katika Mji wa Makambako. Lakini nikufanyie marekebisho kidogo kwamba, mradi huo unatarajia kugharimu dola milioni 32.9 na Serikali yako Serikali ya Chama cha Mapinduzi ambayo mwenyewe uliwashawishi wananchi wako wameichagua, ilipeleka andiko Serikali ya India, na nisema tu kwamba Mheshimiwa Sanga unawaisha shughuli, tunatarajia ifikapo tarehe 15 mwezi Julai, mwezi tunaouanza kesho kutwa mambo yanaweza yakaiva kutoka Serikali ya India na tayari tukaanza na taratibu ya kutekeleza huo mradi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, nikuhakikishie pamoja wananchi wa Mji wa Makambako, na hasa kwa kuzingatia kwamba ndugu yangu Sanga wewe ni shemeji yangu, kwa hiyo maji utapata.