Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI (K. n. y. MHE. LEAH J. KOMANYA) aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Chuo cha Ufundi (VETA) na kuwa vijana wengi waliohitimu elimu ya msingi na sekondari:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga chuo cha ufundi ili vijana hao waweze kupata elimu ya ufundi na kuweza kujiajiri?

Supplementary Question 1

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naitwa Mashimba Mashauri Ndaki hivyo ukisema Mashauri Ndaki bado ni sawa. Niulize swali moja la nyongeza, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri.
Kwa kuwa, tuna chuo kizuri cha VETA pale Maswa Mjini na kwa kuwa pia, tuna Chuo cha Maendeleo ya Jamii Malampaka, wakati huu ambapo matayarisho ya kujenga Chuo cha VETA cha Mkoa yanaendelea, Je, Serikali ina mpango gani wa kuviboresha vyuo hivi viwili ili viweze kuanza kuchukua vijana wakati tunaendelea na mpango wa kujenga Chuo cha VETA mkoani?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwamba Serikali ina mpango gani wa kuviboresha vyuo vya ufundi vya Malampaka na Chuo cha Ufundi cha VETA niseme tu kwamba, Serikali itafanya mapitio ya uendeshaji wa mafunzo ya ufundi stadi nchini. Nimekuwa nikisikiliza michango ya Waheshimiwa Wabunge na maswali ambayo wamekuwa wakiuliza kuhusiana na suala la mafunzo ya ufundi stadi VETA ni kwamba, Wizara ya Elimu inaona kuna umuhimu wa kufanya tathmini ya mafunzo ya ufundi stadi yanatolewa katika vyuo vyote nchini kwa lengo la kuangalia upya aina ya mafunzo yanayotolewa, kuangalia teknolojia inayotumika, na niseme tu kwamba hili ni zoezi ambalo baada tu ya kufunga Bunge lako hiyo ndiyo kazi agenda namba moja ambayo tutafanya tathmini kwa nchi nzima. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa nikiwasikiliza sana Waheshimiwa Wabunge michango yao mizuri na maswali yao kuhusiana na VETA wamekuwa pia wanahoji kuhusiana na teknolojia, kwa mfano baadhi ya vyuo vya ufundi vinaendelea kutumia labda cherehani za miguu, wakati zimepitwa na wakati kwa hiyo hiyo ni tathmini ya ujumla ambayo itahusisha nchi nzima ikiwa nii pamoja na maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyauliza. Baada ya hapo hatua mahsusi zitachukuliwa katika kuhakikisha kwamba VETA zinatoa mafunzo ya kisasa, mafunzo ambayo yanaendana na mahitaji ya sasa hivi ya viwanda tunavyotarajia kuvianzisha.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI (K. n. y. MHE. LEAH J. KOMANYA) aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Chuo cha Ufundi (VETA) na kuwa vijana wengi waliohitimu elimu ya msingi na sekondari:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga chuo cha ufundi ili vijana hao waweze kupata elimu ya ufundi na kuweza kujiajiri?

Supplementary Question 2

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Sera ya Serikali ni kuwa na chuo cha ufundi VETA kila Wilaya lakini hadi sasa ipo baadhi ya Mikoa haina hata chuo kimoja cha ufundi VETA kwa mfano Mkoa wa Rukwa.
Je, Serikali ina mpango gani, wa kiuwiano wa kuhakikisha Mikoa yote ambayo haina vyuo vya ufundi VETA inapewa kipaumbele kwanza?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba mpango wa Serikali wa kuhakikisha kwamba kila Wilaya inakuwa na VETA na kila Mkoa inakuwa na VETA bado uko palepale. Niseme tu kwamba kwa mfano Mkoa wa Rukwa aliyosema changamoto iko ndani ya Mkoa katika kutoa kiwanja, kwa hiyo tungeomba kwamba zile changamoto ambazo zinajitokeza za upatikanaji wa eneo Mkoa wakamilishe ili ahadi ya Serikali iendelee kutekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kwa sababu Mheshimiwa Rais ameipatia Wizara yangu, vyuo vya Folk Development College‟s Wizara kama nilivyosema kwenye majibu ya awali itafanya tathmini ya VETA, itafanya tathmini ya hizo Folk Development College‟s ambazo ni 53 tumekabidhiwa kwa lengo la kuhakikisha kwamba tutatoa kipaumbele kwenye yale maeneo ambayo yalikuwa hayana vyuo vya ufundi ili kuhakikisha kwamba hii ahadi ya Serikali inatekelezwa kwa vitendo.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI (K. n. y. MHE. LEAH J. KOMANYA) aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Chuo cha Ufundi (VETA) na kuwa vijana wengi waliohitimu elimu ya msingi na sekondari:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga chuo cha ufundi ili vijana hao waweze kupata elimu ya ufundi na kuweza kujiajiri?

Supplementary Question 3

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.
Kwa kuwa, katika Wilaya ya Mkalama wako wafadhili wa Marekani wanaitwa Family Community Connection wana pesa takribani zinazozidi shilingi bilioni moja, wamejitokeza kujenga kituo cha VETA Nkungi kwa masharti kwamba Halmashauri ipeleke maji na umeme, na Halmashauri haina pesa. Je, Wizara inasema nini, katika mazingira kama hayo na pesa ziko mkononi?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ningemwomba kama fedha ziko mkononi anikabidhi basi niwe nazo mfukoni, zisiishie kuwa mkononi ziingie mfukoni kwangu. Lakini ningependa tu kusema kwamba kama suala ni upatikanaji wa maji na miundombinu, nadhani hayo ni mambo ambayo yanazungumzika na Wizara yangu haikuwa na taarifa na hili jambo basi atuletee tu rasmi tutalifanyia kazi, lakini naomba hiyo hela ije iingine mfukoni kwa Waziri wa Elimu ili tuweze kufanyia kazi.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI (K. n. y. MHE. LEAH J. KOMANYA) aliuliza:- Mkoa wa Simiyu hauna Chuo cha Ufundi (VETA) na kuwa vijana wengi waliohitimu elimu ya msingi na sekondari:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga chuo cha ufundi ili vijana hao waweze kupata elimu ya ufundi na kuweza kujiajiri?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Karagwe tuna kituo cha ufundi stadi cha KVTC Kayanga. Serikali iliandaa mchoro wa kupanua hiki chuo kwa muda mrefu sasa miaka mingi. Ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni lini Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya kupanua hiki chuo cha KVTC Kayanga.

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba bajeti ya mwaka 2016/2017 Serikali imetenga fedha za kufanya ukarabati wa vyuo viwili. Chuo cha Ufundi Stadi cha Korogwe pamoja na Karagwe kwa hiyo fedha zimetengwa katika bajeti ya mwaka huu.