Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Majengo mengi katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara yamechakaa; je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina swali la nyongeza.

Kwa kuwa hospitali ile ni kongwe na mpaka sasa hivi kwenye Hospitali ya Ligula Mtwara haina x-ray machine, lakini katika suala hilo la kutokuwa na x-ray machine huduma za theatre kwa ujumla wake hazipo.

Je, ni lini Serikali sasa itaamua kututengenezea masuala mazima ambayo yanahusu package hiyo ya x-ray machine pamoja na jengo la theatre? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili, je, ni lini Serikali itaratibu suala zima la kutuletea Madaktari Bingwa ambapo tunashida ya Madaktari Bingwa wa Watoto, Madaktari Bingwa wa Koo ambao vifo vinasababisha kuwa vikubwa sana kwenye hospitali yetu? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, kaka yangu Hassan Tenga kwa ufuatiliaji wake wa kina sana kwa suala zima la Hospitali ya Mkoa, lakini sio tu Hospitali ya Mkoa, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya kwenye Wilaya yake.

Swali lake la kwanza ni lini hospitali hiyo itapata x-ray, lakini pamoja na vifaa vya theatre. Kama ambavyo nimekuwa nikisema hapa Rais wetu miezi michache iliyopita alitoa shilingi bilioni 123 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa na hospitali yake hiyo ipo kwenye bajeti kwa ajili ya vifaa husika ambavyo ameulizia.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili analoulizia ni suala ambalo mimi na yeye kama ambavyo nimemuomba la madaktari kupelekwa kwenye hospitali yake; na ni ukweli kwamba kuna tatizo la madaktari kwenye maeneo mengi tu sio eneo la kwake na kuna makakati huo sasa wa ajira mpya ambazo zinakuja tunamfikiria lakini mimi na yeye kama tulivyopanga tutakwenda kwenye hospitali yake kufuatilia Hospitali ya Mkoa tutakwenda pamoja tutaona tatizo ni kubwa kiasi gani tuone tunafanya nini kuhamisha sehemu nyingine ili madaktari waweze kusaidia eneo hilo.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Majengo mengi katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara yamechakaa; je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize Hospitali ya Wilaya ya Hai imekuwa na changamoto kubwa sana ya majengo mpaka ninivyozungumza hatuna jengo la mama na mtoto, hatuna jengo la pharmacy, hatuja jengo la maabara kakini pia work way za kuwasiliana kwenye majengo haya hatuna.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutujengea majengo haya? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze kaka yangu Saashisha Mafuwe kwa kazi kubwa ambayo anaifanya kwenye Wilaya ya Hai hasa kwenye kufuatilia miundombinu tu sio tu ya Hospitali ya Wilaya, lakini zahanati zake lakini vituo vya afya na Hospitali ya Machame ambayo ni DDH, ni ya kanisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja kuna kazi kubwa sana inafanywa na Waziri wa Afya Mheshimiwa Dorothy Gwajima pamoja na Waziri wa TAMISEMI dada yetu Ummy Mwalimu ya kuhakikisha tunapata resources kupita sources zingine ili tuweze kukamilisha miradi kama hiyo ambayo anaisema ambayo inawezekana haijaingia kwenye bajeti kubwa ambayo sasa tumeipitisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Saashisha tukitoka hapa twende pamoja, tuangalie mkakati huo wa Mawaziri wetu wawili tuone ni namna gani inaweza kufanyika kupitia Global Fund, ahsante sana. (Makofi)

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Majengo mengi katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara yamechakaa; je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana; kwa kuwa Serikali imeendelea na ukarabati wa Hospitali ya Rufaa ya Mandewa, nataka kujua tu ni nili itakamilisha ukarabati huo ili kuondoa adha inayojitokeza katika suala la kupata huduma ya afya katika Mkoa wa Singida? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tulishakwisha kusema hapa kwa bajeti ya mwaka 2021/2022 zimetengwa zaidi ya shilingi bilioni 57 kwa ajili ya kufanya ukarabati na ujenzi katika hospitali mbalimbali za rufaa hapa nchini hospitali aliyoitaja Mheshimiwa hapa ni mojawapo ya hospitali ambayo ipo kwenye mpango huo.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Majengo mengi katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara yamechakaa; je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu Hospitali ya Rufaa ya Ligula tuna ujenzi wa Hospitali ya Kanda ya Kusini Mtwara ambao naishukuru Serikali imekamilisha kwa awamu ya kwanza; je, Serikali imejipangaje kuanza ujenzi awamu ya pili ya hospitali hiyo?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo amekuwa karibu sana kufuatilia ujenzi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Kanda nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwenye bajeti ya mwaka huu ni moja wapo ya hospitali ambazo zimetengewa fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi na kumalizia baadhi ya unit ambazo ilikuwa hazijamaliziwa, ni hospitali aliyoitaja.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Majengo mengi katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara yamechakaa; je, ni lini Serikali itaanza ukarabati wa Hospitali ya Mkoa wa Mtwara?

Supplementary Question 5

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la x-ray katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Ligula mimi niliuliza hilo swali Bunge lililopita Naibu Waziri wakati ule Mheshimiwa Ndugulile aliniambie x-ray machine ya Mkoa wa Mtwara ipo bandarini, leo majibu ya Naibu Waziri anaongea as if hakuja kitu kabisa. Mimi nataka tu kujua ile x-ray yetu ambayo tuliambiwa ipo bandarini ime-evaporate au vipi? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze dada yangu mpambanaji kwa swali lake zuri ambalo linahusu wananchi; moja ni kwamba anasema kwamba x-ray hiyo ilikuwa ipo bandarini na mpaka sasa haijafika kwenye eneo husika. Nikuombe dada yangu tukimaliza maswali hapa twende mimi na wewe tukakae pale tufuatilie hiyo x-ray na tuweke utaratibu iweze kufika mapema inapotakiwa, ahsante sana.