Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ulikuwa wananchi wa Kata za Goweko, Kigwa, Nsololo na Igalula kupata maji Desemba, 2021 lakini majibu ya Serikali yamekwenda tena Juni, 2022. Lakini utekelezaji wake mpaka sasa hivi umefikia asilimia 10.

Je, Serikali haioni kuusogeza karibu mradi huu uweze kutekelezeka kwa kasi ili wananchi wa kata hizo waweze kupata maji? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Jimbo la Igalula lina changamoto sana ya upatikanaji wa maji, ndiyo maana tunaelekeza Serikali iwekeze katika uchimbaji wa mabwawa. Niiombe Serikali haioni haja ya uharakishaji wa haraka wa usanifu wa uchimbaji wa mabwawa hasa hili Bwawa la Kizengi? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Igalula kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya. Ni Mbunge mfuatiliaji, mpambanaji hususan katika suala zima la wananchi wake waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha. Nitoe shukrani kwa Bunge lako tukufu kwa kutuidhinishia fedha zaidi ya bilioni 680 lakini Mheshimiwa Rais naye ametupatia fedha ya nyongeza zaidi ya bilioni 207. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge maeneo ambayo tutayapa kipaumbele na kuyapa fedha za kutosha ili kukamilisha mradi ule ni eneo la mradi huu wa Igalula kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na wananchi wake wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Wizara yetu ya maji tumeboresha Kitengo chetu cha Uchimbaji wa Mabwawa. Tunaona kabisa yapo maeneo ambayo hayana fursa ya uchimbaji wa visima. Tunataka maji ya mvua isiwe laana, tunataka tuyavune kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa ili Watanzania waweze kunufaika na uvunaji wa maji ya mvua waweze kupata huduma ya maji.

Kwa hiyo, mkakati uliokuwepo tunakwenda kununua seti ya ujenzi wa mabwawa kwa maana ya vitendea kazi ili kazi hii ianze na Watanzania waweze kunufaika na ujenzi wa mabwawa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona nami kuuliza swali la nyongeza.

Kwanza nishukuru Serikali kwa kuanzisha RUWASA, lakini pamoja na hayo RUWASA inakabiliwa sana na tatizo la upungufu wa wataalam pamoja na vitendea kazi.

Je, Serikali ina mkakati gani katika kutatua tatizo hilo ili kuleta ufanisi wa utendaji kazi? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kutambua umuhimu wa uanzishwaji wa Wakala wa Maji Vijijini - RUWASA; hili nipendekezo lenu Waheshimiwa Wabunge. Kwa hiyo, kikubwa ambacho tulianzisha RUWASA kwa minajimu ya kwenda kutatua tatizo la maji vijijini. Ipo changamoto hususan ya watumishi. Tumeomba kibali kupitia Ofisi ya Rais - Utumishi kuhakikisha kwamba tunapata watumishi wa kutosha. Lakini katika kipindi hiki maelekezo ambayo tumeyatoa Wizara ya Maji kuhakikisha kwamba tuna Mamlaka za Maji kule mikoani waungane kwa pamoja ili katika kuhakikisha kwamba wana team up ili kuhakikisha kwamba miradi inakwenda na Watanzania wanapata huduma ya maji safi na salama.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa maji katika Kata ya Mnazi, Tarafa ya Umba ni takribani miezi miwili sasa RUWASA wamepeleka saruji na mipira ile midogo, lakini mpaka sasa tunasubiri mabomba. Ni lini mabomba haya yatapelekwa ili maji katika Mji wa Mnazi na viunga vyake yaweze kupatikana kwa urahisi? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Shangazi, kaka yangu ambaye anafanya kazi kubwa sana katika Jimbo lile la Mlalo.

Mheshimiwa NaibU Spika, nataka nimhakikishie maji hayana mbadala na sisi kama Wizara ya Maji umuhimu wetu na jukumu letu ni kuhakikisha tunalinda uhai wa wana Mlalo na wana Mnazi. Natoa maelekezo kwa Mhandisi wa Maji wa pale Lushoto kuhakikisha mpaka Jumatatu mabomba yamefika na kazi ianze mara moja. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu SPika, maji ni uhai kwa viumbe vyote, maji ni muhimu kwa ustawi.

Naomba kuuliza swali langu, Jimbo langu la Mchinga halina maji safi na salama. Sasa ningeomba jimbo hili lifikiriwe kwa umakini mkubwa kupata maji safi na salama kutoka chanzo kikubwa cha Ng’apa.

Je, ni lini maji safi na salama ya bomba yatapelekwa katika Jimbo langu la Mchinga kwa ajili ya wananchi wa jimbo hilo? Ahsante. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, dhati ya moyo kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Mama yangu Salma Kikwete, kiukweli ni Mbunge ambaye kwanza anajua changamoto za watu wake na anaelala na mgonjwa ndiye anayejua mihemo ya mgonjwa. Kwa hiyo, naomba nimpe upendeleo maalum kabisa moja kufika kwanza katika jimbo lake la Mchinga, lakini la pili tunatambua kweli tuna chanzo toshelevu pale Ng’apa ambapo tumejenga mradi ule wa Lindi. Tunataka tuyatoe maji ya pale Ng’apa ili kuhakikisha kwamba yanafika katika Jimbo la Mchinga ili wananchi wa Mchinga waweze kuondokana na tatizo hilo la maji. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Supplementary Question 5

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bwawa la Ichemba lililopo katika Kata ya Ichemba lilikuwa kwenye mpango wa upembuzi yakinifu tangu mwaka 2015 lakini mpaka dakika hii halijawekwa kwenye huo mpango na baada ya kuingia RUWASA hilo bwawa limesahaulika kabisa. Tunajua bwawa hilo likikamilika linakwenda kutatua kero katika kata tisa za Jimbo la Ulyankulu.

Je, ni lini bwawa hili sasa litawekwa katika mpango wa upembuzi yakinifu na kukamilika kwa ujenzi? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge na nimpongeze sana; katika kipindi ambacho tunaenda kuandika historia katika Wizara yetu ya Maji ni kipindi hiki kwa sababu Mheshimiwa Rais amedhamiria kwa dhati kabisa. Wanasema, yafaa nini imani bila matendo? Mheshimiwa Rais ametuongezea fedha zaidi ya shilingi bilioni 207 kwa ajili ya kwenda kutatua matatizo ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, maeneo ambayo tutawapa kipaumbele ni maeneo yale yenye changamoto na ninatambua Ulyanhulu ni maeneo ambayo yana changamoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, tutaunga mkono na tutatoa fedha kuhakikisha ile kazi inaanza na wananchi wako waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Supplementary Question 6

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa tatizo la maji katika Jiji la Dar es Salaam kwenye Jimbo langu la Kawe hasa Kata ya Wazo kwenye eneo la Madale, Kisanga, Mbezi Juu hakuna maji kabisa. Waziri anasemaje kwa habari ya kuwapa maji watu wa Kawe, ni lini hasa Mheshimiwa Waziri? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, brother wangu Gwajima kwa kazi kubwa ya muda mfupi ambayo anaifanya katika Jimbo lile la Kawe. Tarehe 5 Julai nitakuwepo Jijini Dar es Salaam nina mazungumzo na watu wa DAWASA.

Mheshimiwa Mbunge nikuombe uwepo katika kikao kile na moja ya maelekezo ya haraka tutakayoyafanya ni kuhakikisha wananchi wa Wazo wanaenda kupata maji kwa haraka. Ahsante sana.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: - (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha mradi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Kata za Kigwa, Goweko, Igalula na Nsololo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa uchimbaji wa mabwawa katika Kata za Mmale, Miswaki, Lutende na Kizengi ili kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo hayo?

Supplementary Question 7

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu za Serikali zinaonesha kwamba maji vijijini yanapatikana asilimia 74 na mijini ni asilimia 85 kwenda 90; lakini uhalisia unaonesha kwamba mnasema watu wamepata maji kutokana na kuweka miundombinu na sio nyumba kwa nyumba.

Kwa kuwa sasa hivi tunaenda kwenye sensa ya Taifa ambapo watu wataenda kufanyiwa hesabu nyumba kwa nyumba. Kwa nini msitumie utaratibu huu wa sensa ili kuweza kupata takwimu halisi ya kila nyumba ambayo inapata maji nchi hii? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze na nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge dada yangu Halima, sisi Wizara yetu ya Maji inafanya mageuzi makubwa sana na moja ya eneo ambalo eneo unalizungumzia sisi tumeshalifanyia kazi. Tumekutana na watu wetu wa takwimu ili kuhakikisha kwamba tunakwenda kwenye hilo hilo. Lakini tunataka tujiongeze mbali zaidi. Badala ya kusema tu asilimia ngapi watu wanapata maji, tunataka twende mbali zaidi, tunataka tujue Tanzania kuna vijiji vingapi, vingapi vimepata maji, vipi havijapata maji ili tuhakikishe tunaviongezea nguvu maeneo ambayo hayana maji ili waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana. (Makofi)