Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Katika Bunge la Kumi aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii aliunda Kamati Ndogo ya kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara:- (a) Je, ni nini matokeo ya Kamati Ndogo iliyoundwa? (b) Je, ni lini wananchi watapewa taarifa ya Kamati Ndogo iliyokuwa inashughulikia mgogoro huo?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mgogoro uliopo kati ya Wananchi wa Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara ni sawasawa na mgogoro uliopo kati ya Hifadhi ya Mkungunero na wananchi wa vijiji 11 vya Wilaya ya Kondoa. Katika mgogoro huo wananchi wameuawa, Askari wa Hifadhi ya Mkungunero wamekufa na mgogoro huu ni wa muda mrefu na tumeiomba Serikali washughulikie mgogoro huo na wananchi wanaomba kilometa 50 tu ili mgogoro umalizike.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mawaziri waliopita wametembelea na wamefanya mikutano na wananchi wa vijiji 11 wa Wilaya ya Kondoa pamoja na Chemba. Je, Mheshimiwa Waziri ni lini mgogoro wa wananchi wa Wilaya ya Kondoa, vijiji 11 utaisha kati ya Hifadhi ya Mkungunero na wananchi hao?

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kujibu swali la nyongeza kuhusu Mbuga ya Mkungunero. Wizara yangu pamoja na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, imeandaa mpango wa kupima maeneo yote ambayo yana mgogoro kati ya wananchi na Hifadhi za Taifa ili kufanya juhudi za kutatua matatizo haya moja kwa moja.
Mh

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Katika Bunge la Kumi aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii aliunda Kamati Ndogo ya kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara:- (a) Je, ni nini matokeo ya Kamati Ndogo iliyoundwa? (b) Je, ni lini wananchi watapewa taarifa ya Kamati Ndogo iliyokuwa inashughulikia mgogoro huo?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Mgogoro huu kati ya wananchi na Hifadhi ya Ziwa Manyara umedumu kwa muda mrefu na chanzo cha mgogoro ni ardhi ya wananchi kuchukuliwa na Hifadhi bila ridhaa yao.
Huko nyuma waliwaruhusu waweze kutumia angalau umbali wa mita 100 kwa ajili ya kuchungia mifugo yao na baadaye hifadhi ikanyang‟anya tena.
Je, Serikali haioni suluhisho la kuondoa mgogoro huu ni kuwaachia hizo mita 100 tu ili mgogoro uishe kabisa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Waziri alipokuja alitoa ahadi kwa wananchi kwamba, kuna fedha shilingi milioni 160 zitapelekwa; shilingi milioni 100 kwa ajili ya madarasa na shilingi milioni 60 kwa ajili ya soko la akinamama, lakini mpaka leo fedha hizo hazijatolewa! Ni lini fedha hizi zitatolewa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu kuwaachia wananchi eneo linalozungumziwa. Swali la msingi lilikuwa ni nini matokeo ya Kamati. Sehemu yake ya pili, ni lini wananchi watapewa Taarifa ya Kamati hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya kikamilifu ya swali hili yamo katika Taarifa tunayoizungumzia. Kwa hiyo, kwa kuwa, Taarifa tayari ipo na tumemwambia Mheshimiwa Mbunge kwamba Taarifa hiyo itakuwa tayari kuwasilishwa mbele ya wananchi ndani ya muda wa miezi mitatu. Nikisema ndani ya muda wa miezi mitatu, inaweza kuwa wiki moja, itakuwa ni vema tukasubiri wakati utakapofika tujue wale waliofanya utafiti wa kitaalam na wakaandaa taarifa wamesema nini, kuliko jibu ambalo linaweza kuwa la haraka haraka tu hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi ya fedha halikadhalika kwa sababu waliofanya utafiti wameangalia mgogoro kwa ujumla wake na upana wake na muundo wa Kamati yenyewe iliyofanya uchunguzi ulijumuisha wananchi pia, nina hakika kama hili ni mojawapo ya mambo yaliyozungumziwa, litakuwemo ndani ya ripoti hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo naomba Mheshimiwa Mbunge, akubaliane na mimi tu kwamba kwa kuwa, nimesema ndani ya miezi mitatu na nimesema ndani ya miezi mitatu inaweza kuwa wiki moja, akavumilia tu Wizara itakapokuja kuwasilisha taarifa hii mbele ya wananchi na mambo yote yatakayojitokeza yatakuwa yameamuliwa wakati huo.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Katika Bunge la Kumi aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii aliunda Kamati Ndogo ya kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara:- (a) Je, ni nini matokeo ya Kamati Ndogo iliyoundwa? (b) Je, ni lini wananchi watapewa taarifa ya Kamati Ndogo iliyokuwa inashughulikia mgogoro huo?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Migogoro ya ardhi kati ya hifadhi zetu na wananchi wanaozunguka hifadhi imekuwa ni migogoro ya muda mrefu na imeenea katika nchi nzima. Katika Jimbo langu la Liwale sisi ni miongoni mwa tuliozungukwa na Hifadhi ya Selous.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunao mgogoro mkubwa sana kati ya hifadhi ya Selous pamoja na Kijiji cha Kikulyungu wakigombea bwawa la Kihurumila. Mgogoro huu umeshapoteza maisha ya watu kwa muda mrefu na hata Mbunge aliyepita wa Jimbo la Liwale mgogoro huu umemfanya asirudi tena Bungeni pale alipotamka Bungeni kwamba anasikia watu wamefariki katika bwawa hilo, badala ya yeye kwenda kujiridhisha na kuangalia hali halisi ya mgogoro huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini basi Mheshimiwa Waziri atashiriki katika kutatua mgogoro huu ili maisha ya watu wa Liwale yasiendelee kupotea wakigombea bwawa la Kihurumila? Naomba majibu.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo amemaliza kuuliza Mheshimiwa Mbunge hivi punde. Waheshimiwa Wabunge karibu wote wanaopakana na hifadhi wakisimama hapa watazungumza matatizo yanayofanana kuhusiana na suala la mipaka baina ya hifadhi na wananchi wanaoishi jirani nazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niseme tu kwa jibu la ujumla ili kila mmoja ajiandae kupokea matokeo katika hili. Ni kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ambayo inatekeleza Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2015 - 2020, imejipanga vizuri kwa kuweka suala hili baada ya kuliona kuwa ni tatizo kubwa sana; imejipanga vizuri kwa kuliweka waziwazi kwenye Ilani yake na imesema hivi:
“Katika kutatua migogoro hii, Chama kitaendelea kusimamia Serikali yake kuhakikisha kwamba, kinaendelea kujenga mahusiano mema baina ya Hifadhi za Taifa na wananchi wanaoishi karibu na hifadhi hizo kwa namna ambayo wananchi hao watanufaika na uwepo wa hifadhi hizo.”
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia, Ilani hiyo hiyo ukurasa wa 23 mpaka 25 inasema:
“Tutasimamia zaidi katika kutatua migogoro ya mipaka kati ya wananchi na maeneo ya jirani na hifadhi kwa kushirikisha wadau katika kuhakiki mipaka ya maeneo ya hifadhi kwa kuweka alama za kudumu, kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi na kuzingatia utawala wa sheria katika kusimamia rasilimali za maliasili.”
Sasa hata wale wanaoingilia katikati ninavyozungumza, pengine wanataka kusema kwamba, hilo ndilo lililoandikwa, lakini wanasubiri utekelezaji. Sasa nataka niseme kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga sasa kutekeleza kwa vitendo haya ambayo nimeyasema, kama ambavyo yamekuwa yakisemwa siku zote, lakini sasa hivi tumejipanga vizuri zaidi katika utekelezaji.

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Katika Bunge la Kumi aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii aliunda Kamati Ndogo ya kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara:- (a) Je, ni nini matokeo ya Kamati Ndogo iliyoundwa? (b) Je, ni lini wananchi watapewa taarifa ya Kamati Ndogo iliyokuwa inashughulikia mgogoro huo?

Supplementary Question 4

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa migogoro iliyozungumzwa katika hifadhi haitofautiani na malalamiko ya muda mrefu yanayotolewa na Jumuiya za Wapagazi, Waongoza Watalii na Wapishi katika Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro na hifadhi nyingine za Taifa, wakigombana au wakilalamikia Tours Operators wao.
Je, Serikali kwa sababu, inalifahamu hili, ni lini itatatua migogoro hii ili maslahi na mazingira ya kikazi ya Jumuiya hizo za Wapagazi, Waongoza Watalii na Wapishi yaweze kuboreshwa, kama mabalozi wema wa kustawisha utalii katika nchi yetu?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri lenye mwelekeo wa kuboresha zaidi huduma kwenye sekta ya utalii huku tukitambua wote kwamba, utalii unaongoza katika kuliingizia Taifa hili fedha za kigeni. Si zaidi ya wiki mbili nilikuwa KINAPA pale Kilimanjaro National Park, lakini baada ya pale niliungana na Mheshimiwa Waziri, Arusha Mjini ambako tulikutana na Vyama vya Watoa Huduma wote kwenye Sekta ya Utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, zilijitokeza changamoto nyingi, mojawapo ilikuwa ni hiyo na kwamba, sasa Serikali tayari imeshaweka jedwali la changamoto zote hizo ambazo zimezungumziwa na sasa tumejipanga kuhesabu moja baada ya nyingine ili kuweza kupata majawabu na kuweza kutatua migogoro hiyo na matatizo hayo ili tuweze kuboresha Sekta ya Utalii.