Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR) aliuliza:- Suala la Madaktari feki limezoeleka nchini Tanzania na linazidi kuendelea siku hadi siku katika hospitali zetu:- (a) Je, Serikali haioni kuwa suala hili ni kuhatarisha maisha ya Watanzania kutokana na uzembe na usimamizi mbovu wa hospitali zetu? (b) Je, Serikali imechukua hatua gani kuondoa kadhia/ kero hii isiendelee?

Supplementary Question 1

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya ngongeza. Kwa kuwa mbali na matatizo ya Madaktari hatari feki ambao wameenea katika baadhi ya hospitali zetu, lakini pia kuna tatizo sugu la dawa feki ambazo zinateketeza ama zinaleta athari kwa watumiaji wa dawa hizo. Je, Serikali inalishughulikiaje tatizo hilo la dawa feki? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Waganga wa Tiba Asilia wameenea katika maeneo mengi ya nchi yetu ya Tanzania na kwa kuwa baadhi yao hutumia dawa feki ambazo hazijathibitishwa.
Je, kwa nini Serikali inawaruhusu Waganga hao wa Tiba za Asili kufanya kazi zao na baadhi yao kutoa dawa feki kwa watumiaji? Ahsante.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu dawa feki, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Faida Mohamed Bakar, Waheshimiwa Wabunge wote na wananchi kwa ujumla kwamba uwezekano wa kuwa na dawa feki kwenye vituo vya kutolea tiba hapa nchini ni mdogo sana, almost hakuna kwa sababu tuna utaratibu mzuri wa kuhakiki viwango vya ubora wa dawa ambazo zinatolewa kwa ajili ya matumizi ya binadamu na hata zile za mifugo hapa nchini kwetu, utaratibu huu ni mgumu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kusajili dawa ambayo itaingia kwenye soko inachukua muda mrefu, inachukua Mamlaka mbalimbali za uchunguzi kuichunguza dawa hiyo na hatimaye kuiruhusu iweze kutumika katika vituo vyetu. Kama ikijitokeza kukawa kuna walau fununu tu za uwepo wa dawa feki basi, Serikali kutumia mamlaka zake za uchunguzi hutuma kikosi cha ukaguzi kwenye eneo hilo ili kuweza kuthibitisha kama kweli maneno hayo yanayosemwa kuhusu uwepo wa dawa feki ni ya kweli ama laa. Mara nyingi hatua kali huchukuliwa dhidi ya mtu yoyote yule ambaye atakutwa na dawa feki.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu waganga wa tiba asili, waganga wa tiba asili wapo kisheria, wanatambuliwa kwa mujibu wa sheria na wanasajiliwa kwa mujibu wa sheria ya waganga wa tiba asili na tiba mbadala ya mwaka 2002.
Mheshimiwa Naibu Spika, hawa ni kweli baadhi yao wanatoa dawa ambazo ni feki na siku zote tumekuwa tukiwabaini na tukichukua hatua za kuwadhibiti. Napenda kutumia Bunge lako Tukufu kuwaeleza waganga wote feki ambao hawajasajiliwa kuchukua hatua za kufika kwenye Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala mara moja, kwa ajili ya kusajiliwa pia kutumia utaratibu mpya ambao tumeuanzisha baada ya lile tukio la Dkt. Mwaka nilipoamua kumtembelea kwa ghafla. Tumeanzisha utaratibu mpya sasa wa kusajili dawa zote ambazo zinatolewa na waganga wa tiba asili na tiba mbadala hususani zile ambazo zinafanyiwa packaging kisasa. Utaratibu huo na wenyewe utakuwa mgumu kama ulivyo huu wa dawa hizi za tiba ya kisasa ili kuweza kudhibiti uwezekano wa uwepo wa waganga wa tiba asili ambao wanaweza wakawa wanatoa dawa ambazo zina sumu ndani yake.

Name

Hafidh Ali Tahir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR) aliuliza:- Suala la Madaktari feki limezoeleka nchini Tanzania na linazidi kuendelea siku hadi siku katika hospitali zetu:- (a) Je, Serikali haioni kuwa suala hili ni kuhatarisha maisha ya Watanzania kutokana na uzembe na usimamizi mbovu wa hospitali zetu? (b) Je, Serikali imechukua hatua gani kuondoa kadhia/ kero hii isiendelee?

Supplementary Question 2

MHE. HAFIDH ALI TAHIR: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza, kwa sababu Watanzania huwa wanasafiri kati ya Bara na Zanzibar kwa ajili ya kutafuta matibabu, na kwa sababu Wizara hizi mbili siyo za Muungano. Mheshimiwa Waziri unaweza kutuambia nini kuhusu ushirikiano wa pamoja kati ya Bara na Zanzibar kuhakikisha waganga hao feki wanapigwa vita ili wananchi waende vizuri.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yetu ya Afya inafanya kazi kwa karibu sana na Wizara ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwenye mambo yote yanayohusu afya, ikiwemo tiba asili na tiba mbadala. Hivyo kama kuna tatizo hilo kule Zanzibar kuna fursa ya wataalamu kushirikiana, kuna fursa ya viongozi wa hizi Wizara mbili kushirikiana na utamaduni huo umekuwepo toka hata sisi hatujaingia humu kwenye Serikali. Kwa hiyo, asiwe na shaka kama kuna tatizo huwa tunawasiliana na tunashirikiana kwa ukaribu.

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR) aliuliza:- Suala la Madaktari feki limezoeleka nchini Tanzania na linazidi kuendelea siku hadi siku katika hospitali zetu:- (a) Je, Serikali haioni kuwa suala hili ni kuhatarisha maisha ya Watanzania kutokana na uzembe na usimamizi mbovu wa hospitali zetu? (b) Je, Serikali imechukua hatua gani kuondoa kadhia/ kero hii isiendelee?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA A.BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya madhara ya Madaktari feki wamekuwa wakisababishia wagonjwa hawa vilema vya maisha au kupoteza maisha kwa ujumla.
Je, kuna utaratibu wowote wa fidia kuwafidia watu hawa?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, japo kuwa Mheshimiwa Halima Bulembo ni jirani yangu ungenitonya kwamba utaniuliza swali. Kwanza hakuna tukio lolote lile ambalo limewahi kuripotiwa ambapo Daktari feki amesababisha madhara kwa mgonjwa. Madaktari feki hawa mara nyingi kwa matukio ambayo tunayafahamu wamekuwa wakitoa huduma kisanii tu kwa malengo ya kutaka kukusanya pesa hususani zile wa rushwa kutoka kwa wateja. Lakini haijatokea wakafanya haswa kitendo cha kwenda kutoa tiba kwa mgonjwa, hususani labda kufanya operesheni ama kufanya procedure. Kama ingewahi kutokea hivyo pengine labda kungekuwa kuna sheria ambayo ingekuwa inatuongoza kwamba nini kiwe fidia kwa mteja yoyote yule ambaye atakuwa amesababishiwa madhara kutokana na Madaktari feki.

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR) aliuliza:- Suala la Madaktari feki limezoeleka nchini Tanzania na linazidi kuendelea siku hadi siku katika hospitali zetu:- (a) Je, Serikali haioni kuwa suala hili ni kuhatarisha maisha ya Watanzania kutokana na uzembe na usimamizi mbovu wa hospitali zetu? (b) Je, Serikali imechukua hatua gani kuondoa kadhia/ kero hii isiendelee?

Supplementary Question 4

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa uchumi wa nchi yetu umekuwa ukiimarika na mikakati ambayo imeendelea ambayo imekuwa ikifanywa hivi sasa inaonyesha kwamba nchi yetu itakuwa ni Taifa bora. Lakini vilevile kwa kuwa idadi ya watu inazidi kuongezeka na kwa miaka mingi ya nyuma Serikali yetu imekuwa ikisomesha Watanzania wengi katika nchi mbalimbali lakini baadhi ya Watanzania ambao ni Madaktari waliamua kuondoka hapa Tanzania na kwenda nje kwa ajili ya sababu kuwa zikiwa ni maslahi.
Je, Serikali ina mkakati gani maalum wa kuweza kuwarejesha Madaktari hawa ambao sasa wamepata uzoefu mkubwa.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli kwamba Serikali yetu imekuwa ikiongeza udahili kwa ajili ya kufundisha Watanzania wenzetu kwenye fani za tiba kwa kiasi kikubwa sana katika miaka ya hivi karibuni. Hivi tunavyozungumza hapa kwa mwaka mmoja tuna uwezo sasa hivi wa kuzalisha takribani Madaktari wa tiba 1,000. Hiki ni kiasi kikubwa sana na ni uwekezaji mkubwa sana ambao umefanywa na Serikali yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kutambua uwekezaji huu mkubwa uliofanyika ni kweli nakiri kwamba tumekuwa na uwezo mdogo wa kuwa- absorb kwenye system wale wote wanaohitimu kwenye fani za tiba na utabibu kwa ujumla wake. Serikali ya Awamu ya Tano tayari ina mkakati mahsusi wa kuhakikisha tunaongeza kiasi cha Madaktari ambao wanakuwa absorb kwenye system ya kutolea huduma za afya ili tuwe na Madaktari wengi zaidi ambao wanafanya kazi kwenye Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu maslahi mpaka hivi ninavyoongea hapa Madaktari ni mojawapo ya fani za kitaalamu hapa nchini ambao wanalipwa vizuri sana kuliko wengine. Hivi ninavyoongea Daktari anayemaliza masomo yake ya Degree analipwa vizuri sana kuliko ukilinganisha na fani zote zile kwenye Serikali na tunavyoongea kwenye sekta binafsi sasa wanaanza kupata shida kuajiri Madaktari ambao wamehitimu kwa kuwa ndani ya Serikali maslahi ni mazuri zaidi kuliko hata yale ya kwenye sekta binafsi na ni jambo la kujivunia. Kwenda nje pia siyo jambo la kusema ni baya, kwa sababu wa navyoenda wengi wao wanakaa miaka mitatu, miaka sita wanarudi nchini kuja kutoa tiba hapa na tayari wanakuwa wameshapata uzoefu wa kufanya kazi nje ya nchi. Kwa hivyo, ni fursa na hatuwezi kuwabana kwa njia nyingine yoyote ile zaidi ya kusema tuboreshe maslahi ndani ya Serikali ili Madaktari waweze kutoa huduma kwa Watanzania wengi hapa nchini.