Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aeshi Khalfan Hilaly

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumbawanga Mjini

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y. MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:- Shamba la Garagua linalomilikiwa na KNCU lililopo katika Wilaya ya Siha, liliamuliwa liuzwe mwaka 2015 ili kulipa mkopo wa shilingi bilioni nne uliochukuliwa na KNCU na baadaye kushindwa kufanya marejesho ya mkopo huo kwa wakati:- (a) Je, ni kwa nini Serikali isiwawajibishe viongozi wa KNCU waliousababishia ushirika hasara kwa kuchukua mkopo ambao wameshindwa kuulipa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuyarudisha mashamba ya ushirika yanayotumika kwa maslahi ya wachache au ambayo ushirika umeshindwa kuyaendeleza katika umiliki wa Halmashauri za Wilaya husika?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza; je, Serikali iko tayari kukisaidia Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Pwani (CORECU) ili kiweze kujijenga na kuwasaidia wakulima wa Mkoa wa Pwani hasa wakulima wa korosho wa Wilaya ya Mkuranga waweze kuuza korosho zao kwa bei nzuri lakini pia kupata pembejeo ya sulphur kwa kuwasaidia Chama Kikuu cha Ushirika (CORECU) kulipa deni wanalodaiwa na Benki ya CRDB?
La pili, kuwasaidia Chama Kikuu cha Ushirika (CORECU) kuweza kuyatwaa tena maghala yake yaliyomilikiwa na watu binafsi yaliyopo kule Ukonga, Dar es Salaam?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inasaidia na imekuwa ikikaa mara kwa mara na CORECU ili kukabiliana na changamoto mbalimbali katika kusaidia wakulima wa korosho katika Mkoa wa Pwani, ikiwa ni pamoja na wanaotoka katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge. Tayari Wizara imeisaidia CORECU kuweza kulipa sehemu kubwa ya deni ambalo wanadaiwa na CRDB. CRDB walikuwa wanadai CORECU shilingi bilioni 3.5, lakini Serikali ikawasiliana na BOT ili kuweza kulipa asilimia 75 ya principal sum ya deni ambalo walikuwa wanadaiwa kwa sababu BOT alikuwa ni guaranter katika mkataba wa deni lile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tayari imeshalipwa bilioni 1.2 na sasa hivi tunavyoongea bado CORECU wanadaiwa bilioni 2.4, lakini bado tunaendelea kuongea na CRDB ili waweze kuangalia namna ya ku-restructure lile deni ili Chama cha Ushirika cha CORECU waweze kulipa kwa muda mrefu zaidi wasije wakauziwa mali zao. Vilevile, Wizara kwa kushirikiana na Bodi ya Korosho imejiandaa kuhakikisha kwamba pembejeo zinapatikana kwa wakulima wote wa korosho hususan pembejeo ya sulphur kwa ajili ya mikorosho.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, linahusu maghala ambayo yanamilikiwa. Nimechukua ombi la Mheshimiwa Mbunge na tayari alishafika ofisini kufuatilia hili, nimweleze tu kwamba majadiliano yanaendelea ndani ya Wizara kuangalia ni namna gani bora ya kuweza kurudisha yale maghala kwa wenyewe halali ambao ni Chama cha Ushirika cha CORECU. Ahsante.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y. MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:- Shamba la Garagua linalomilikiwa na KNCU lililopo katika Wilaya ya Siha, liliamuliwa liuzwe mwaka 2015 ili kulipa mkopo wa shilingi bilioni nne uliochukuliwa na KNCU na baadaye kushindwa kufanya marejesho ya mkopo huo kwa wakati:- (a) Je, ni kwa nini Serikali isiwawajibishe viongozi wa KNCU waliousababishia ushirika hasara kwa kuchukua mkopo ambao wameshindwa kuulipa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuyarudisha mashamba ya ushirika yanayotumika kwa maslahi ya wachache au ambayo ushirika umeshindwa kuyaendeleza katika umiliki wa Halmashauri za Wilaya husika?

Supplementary Question 2

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa matatizo haya ya KNCU yanafanana na matatizo yaliyopo katika Chama Kikuu cha Ushirika cha MAMCU cha Mkoa wa Mtwara na Vyama vyake vya Msingi, nataka niulize swali; kwa kuwa wakulima wa korosho wa Wilaya ya Masasi wanadai bilioni nne ambazo ni malipo ya tatu ya malipo ya korosho na hadi sasa kumekuwa na ubabaishaji mkubwa juu ya kupatikana kwa malipo hayo. Je, Mheshimiwa Waziri atatoa maelekezo gani kwa Mrajis wa Vyama kuhakikisha kwamba anafanya uchunguzi wa haraka ili wananchi wale waweze kulipwa malipo yao?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama alivyosema kwamba changamoto ya CORECU ni changamoto ambayo ipo katika Vyama vya Ushirika vingi, vingi vina madeni. Namwomba sana Mheshimiwa Mbunge, tukitoka hapa leo tukutane ofisini kwangu niweze kupata hili analosema kwa mapana na marefu ili tuanze kufanyia kazi mara moja na nimfahamishe tu kwamba, tayari kuna kikao kinaendelea huku cha Vyama Vikuu vya Ushirika na itakuwa ni fursa vilevile ya kulizungumzia katika wakati huu. Kwa hiyo nimwahidi tu kwamba, tutalifanyia kazi.

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y. MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:- Shamba la Garagua linalomilikiwa na KNCU lililopo katika Wilaya ya Siha, liliamuliwa liuzwe mwaka 2015 ili kulipa mkopo wa shilingi bilioni nne uliochukuliwa na KNCU na baadaye kushindwa kufanya marejesho ya mkopo huo kwa wakati:- (a) Je, ni kwa nini Serikali isiwawajibishe viongozi wa KNCU waliousababishia ushirika hasara kwa kuchukua mkopo ambao wameshindwa kuulipa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuyarudisha mashamba ya ushirika yanayotumika kwa maslahi ya wachache au ambayo ushirika umeshindwa kuyaendeleza katika umiliki wa Halmashauri za Wilaya husika?

Supplementary Question 3

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa yapo mashamba ambayo yamebinafsishwa na hayajaendelezwa; je, Serikali ina mpango gani wa kuyarudisha mashamba hayo kwa wananchi ili vijana wa Taifa hili waweze kupata fursa ya kuyatumia mashamba hayo kwa shughuli ya kiuchumi?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, tunavyozungumza hivi kuna kikao kinaendelea Ukumbi wa Hazina hapa Dodoma kuzungumzia kuhusu mashamba haya ya Vyama vya Ushirika ambayo hayaendelezwi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi tunajaribu kutengeneza mkakati ambao haya mashamba yanaweza yakatumika katika maana nzuri zaidi ikiwa ni pamoja na kupeleka na kurudisha kwa wananchi kama tunaona kwamba hakuna utaratibu mwingine wa Vyama vya Ushirika kuyatumia. Kwa hiyo, nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo analosema litafanyiwa kazi.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y. MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL) aliuliza:- Shamba la Garagua linalomilikiwa na KNCU lililopo katika Wilaya ya Siha, liliamuliwa liuzwe mwaka 2015 ili kulipa mkopo wa shilingi bilioni nne uliochukuliwa na KNCU na baadaye kushindwa kufanya marejesho ya mkopo huo kwa wakati:- (a) Je, ni kwa nini Serikali isiwawajibishe viongozi wa KNCU waliousababishia ushirika hasara kwa kuchukua mkopo ambao wameshindwa kuulipa? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuyarudisha mashamba ya ushirika yanayotumika kwa maslahi ya wachache au ambayo ushirika umeshindwa kuyaendeleza katika umiliki wa Halmashauri za Wilaya husika?

Supplementary Question 4

MHE. MPAKATE D. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa matatizo ya ushirika yameenea katika maeneo yote ya nchi yetu ya Tanzania, na kwa kuwa Sheria Na. 6 ya Mwaka 2013 ilianzisha rasmi Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania. Je, ni lini Serikali itaifanya Tume hii iwe na uongozi wa kudumu kwa kuteua Mwenyekiti wa Tume pamoja na Makamishna wa Tume ili ushirika usimamiwe vizuri?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa anavyosema kwamba Tume ya Ushirika bado inakabiliwa na changamoto ya uongozi, nimhakikishie tu kwamba mapendekezo kuhusu uongozi tayari yapo mezani kwa Waziri, kwa hiyo muda mfupi tutasikia kukamilika kwa uteuzi wa viongozi wote wa Tume ya Ushirika.