Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Sehemu kubwa ya Mji wa Lindi imezungukwa na bahari, ambapo wananchi wa Kijiji cha Kitunda wanajishughulisha na shughuli za kilimo na kuishi huko kutumia usafiri ambao sio salama wa mitumbwi midogo midogo kutoka kijijini hapo kwenda Lindi Mjini kwa ajili ya mahitaji muhimu ya kibinadamu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka kivuko kwa ajili ya kuvusha wananchi hao ambao maisha yao yapo hatarini kwa kutumia mitumbwi midogo midogo kutoka Lindi Mjini kwenda Kata ya Kitumbikwela?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru kwa dhati kabisa Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu wakati wa kampeni zake ilikuwa ni ahadi yake ya kujenga kivuko cha kutoka Lindi kwenda Kitunda na alisema baada ya wiki moja Mkurugenzi wa vivuko atakuja Lindi na kweli alikuja, akaja kuangalia eneo. Sasa baada ya kumaliza katika shughuli hiyo ya kwanza tulikuwa hatufahamu kinachoendelea ni kipi, lakini namshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri yenye matumaini.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Rais alituahidi kwamba, katika maeneo yote kuanzia Tanga, Dar es Salaam kuja Lindi mpaka Mtwara kutakuwa na uwezekano wa kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kwa sababu wananchi hawa ni wavuvi wa samaki, kujenga kiwanda cha samaki ili kuongeza ajira kwa wananchi wa maeneo haya.
Je, Serikali imejipangaje katika kuhakikisha maeneo haya yanakuwa na kiwanda cha samaki?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, napokea shukurani kutoka kwa Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum. Namshukuru sana na kwa kweli nafurahia sana Wabunge wengi wanatambua juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza ahadi, ana dhamira ya dhati na kila alipoahidi anajitahidi kutafuta fedha ili kuweza kuteleza ile ahadi yake. Sisi kwa kweli tulioko katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano tunajivunia kwa kupewa dhamana hii ya kuwajengea Watanzania miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu sehemu ya viwanda; maadam alitoa ahadi, nimhakikishie ahadi hiyo itatimia. Kama ambavyo amemsikia Mheshimiwa Mwijage, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji wakati akihitimisha hotuba yake ya bajeti, aliongelea kwa mapana kwamba, karibu kila mahali kuna aina ya viwanda ambavyo anavikusudia kuviboresha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa vyovyote vile, katika maeneo ya Pwani, wavuvi nao watafikiriwa katika kuhakikisha kwamba, tunapata viwanda na viwanda hivyo vinahamasishwa kutoka sekta binafsi waweze kuwekeza na sisi tutawawekea mazingira mazuri ili hatimaye watujengee viwanda na kuchangia katika kuibadilisha nchi hii kuwa nchi ya viwanda itakapofika mwaka 2025.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Sehemu kubwa ya Mji wa Lindi imezungukwa na bahari, ambapo wananchi wa Kijiji cha Kitunda wanajishughulisha na shughuli za kilimo na kuishi huko kutumia usafiri ambao sio salama wa mitumbwi midogo midogo kutoka kijijini hapo kwenda Lindi Mjini kwa ajili ya mahitaji muhimu ya kibinadamu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka kivuko kwa ajili ya kuvusha wananchi hao ambao maisha yao yapo hatarini kwa kutumia mitumbwi midogo midogo kutoka Lindi Mjini kwenda Kata ya Kitumbikwela?

Supplementary Question 2

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Kwa kuwa tatizo la kivuko cha Kitunda, Lindi linafanana sana na tatizo la kivuko baina ya Kilindoni na Nyamisati katika Wilaya ya Rufiji; na kwa kuwa, wananchi wa Mafia kupitia Mbunge wao, tuliiomba Wizara itupatie iliokuwa MV Dar es Salaam, ambayo kwa sasa imepaki pale Navy, Dar es Salaam ili ije itusaidie Mafia kuunganisha baina ya Kilindoni na Nyamisati. Je, ni lini Wizara itaridhia ombi hilo?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza niendelee kumhakikishia Mheshimiwa Dau kwamba, dhamira yetu ya kuhakikisha kivuko kinakuwepo kati ya Kilindoni na Nyamisati ni ya dhati na tutahakikisha inatekelezwa. Kikubwa nimwahidi kwamba hii meli anayoingolea MV Dar es Salaam, tumeshaeleza katika Bunge hili kwamba, meli hii bado hatujaipokea kutoka kwa supplier kutokana na hitilafu chache zilizokuwa zimeonekana na tumemtaka supplier arekebishe hizo hitilafu kabla haijatumika ilivyokusudiwa kutoka Dar es Salaam kwenda Bagamoyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Dau kwamba, kama wahusika wataona kwamba ni busara kwa sababu aina hii ya kivuko siyo ya kuipeleka mwendo mrefu sana. Kila kivuko kina design yake na kina capacity yake ya distance ya kutembea. Wataalam watakapotushauri kwamba, hili eneo nalo linaweza likatumika kwa MV Dar es Salaam, nimhakikishie hatutakuwa na sababu ya kusita kuhakikisha MV Dar es Salaam inahudumia kutoka Dar es Salaam hadi Bagamoyo na Dar es Salaam hadi Mafia.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Sehemu kubwa ya Mji wa Lindi imezungukwa na bahari, ambapo wananchi wa Kijiji cha Kitunda wanajishughulisha na shughuli za kilimo na kuishi huko kutumia usafiri ambao sio salama wa mitumbwi midogo midogo kutoka kijijini hapo kwenda Lindi Mjini kwa ajili ya mahitaji muhimu ya kibinadamu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka kivuko kwa ajili ya kuvusha wananchi hao ambao maisha yao yapo hatarini kwa kutumia mitumbwi midogo midogo kutoka Lindi Mjini kwenda Kata ya Kitumbikwela?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na matatizo yaliyozungumzwa ya watu wa Kijiji cha Kitunda ambayo kwa karibu sana yanafanana na watu wa Jimbo la Busega, ambako kule Busega tuna Ziwa Victoria, hawa wana Bahari. Sasa hivi usafiri wa majini ni tatizo na Waziri mwenye dhamana wakati ule alitembelea Kijiji cha Nyamikoma katika Wilaya ya Busega na akaahidi ujenzi wa gati, lakini mpaka sasa hivi sijajua Serikali inamefikia wapi? Je, Mheshimiwa Waziri anaweza akawahakikishia wananchi wa Busega kwamba, lile gati la Nyamikoma litajengwa ili kusaidia usafiri kwa wananchi wa Jimbo la Busega na Majimbo mengine jirani kama Mwibara, Bunda na Ukerewe?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tuna maeneo mengi ambayo yameainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni anafahamu kwamba, katika aliyoyaeleza yamo. Nimhakikishie kile kilichoko katika Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi, ni wajibu wetu na ni lazima tukitekeleze katika kipindi hiki cha miaka mitano ambacho tumeahidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni tulitafakari kwa undani kuchunguza katika kila kituo ambacho amekiorodhesha tuone. Hatimaye tumpe majibu kipi tunaanza lini na kipi kitafuata lini na hatimaye apate ratiba kamili ya utekelezaji wa ahadi hiyo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa kweli nimsifu sana kwa kazi kubwa anayofanya ya kufuatilia maslahi ya watu wako wa Jimbo la Busega. Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Sehemu kubwa ya Mji wa Lindi imezungukwa na bahari, ambapo wananchi wa Kijiji cha Kitunda wanajishughulisha na shughuli za kilimo na kuishi huko kutumia usafiri ambao sio salama wa mitumbwi midogo midogo kutoka kijijini hapo kwenda Lindi Mjini kwa ajili ya mahitaji muhimu ya kibinadamu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka kivuko kwa ajili ya kuvusha wananchi hao ambao maisha yao yapo hatarini kwa kutumia mitumbwi midogo midogo kutoka Lindi Mjini kwenda Kata ya Kitumbikwela?

Supplementary Question 4

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Wilaya ya Pangani imepakana na Mji wa Zanzibar na wakazi wa Pangani wamekuwa wakijishugulisha na Mji wa Zanzibar kutokana shuguli za kijamii na kiuchumi. Je, ni lini Serikali itatupatia usafiri wa uhakika ili wakazi wa Pangani na wananchi wa jirani Muheza na maeneo ya Kilimanjaro na Arusha ili waweze kunufaika na usafirishaji huu kwa unafuu ili kuweza kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumewahi kutamka ndani ya Bunge lako Tukufu kwamba, iliyokuwa TACOSHIL tuliipaki kwa sababu tulikuwa tunatarajia sekta binasi ndiyo ijihusishe zaidi katika kutoa huduma za usafiri wa majini katika Bahari ya Hindi.
Mheshimiwa Naibu Spika, inaonekana bado kuna kilio cha wengi na vile vile, hata jana nilikuwa na wateja wengine Dar es Salaam nao wanasisitiza kwamba, pengine tuangalie upya suala la TACOSHIL au tuseme huduma za meli kwenye upende wa Bahari kwamba na Serikali nayo ijihusishe kwa sababu kuna baadhi ya maeneo hayawezi kuendeshwa na sekta binafsi kwa faida.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaliangalia ndani ya Serikali, tuangalie kama kuna umuhimu wa kubadilisha sera hiyo na kama tutaona kwamba, hakuna umuhimu badala yake tuendelee kuhamasisha wawekezaji binafsi tutafanya hivyo. Kama tutaona kuna umuhimu tutaleta hapa tufanye maamuzi kwamba, labda turudishe ule uamuzi au yale masuala ambayo tulikuwa tunayafanya miaka ya nyuma chini ya TACOSHIL.