Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Miaka kadhaa iliyopita Serikali iliahidi kuwa itajenga barabara ya kutoka Kitai Wilayani Mbinga hadi Lituhi Wilayani Nyasa kwa kiwango cha lami, lakini hadi sasa wananchi hawaelewi kinachoendelea juu ya ujenzi huo:- Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Mbinga na Nyasa juu ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na pia nashukuru kwa pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, ni lini sasa hii kazi ya upembuzi yakinifu itakamilika ili ujenzi uanze?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, wananchi wa Mbinga pamoja na Nyasa wanafurahi na wanaishukuru Serikali kwa kupata mradi wa ujenzi wa barabara wa Mbinga – Mbamba Bay chini ya mradi wa Mtwara Corridor. Je, Serikali haioni haja sasa kwa kutumia fursa hii kuunganisha kipande cha barabara inayotoka Unyoni mpaka Kijiji cha Mango Wilayani Nyasa kupitia Mapera, Maguu na Kipapa? Ahsante

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martin Mtonda Msuha, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Martin Mtondo Msuha pamoja na Mheshimiwa Stella Manyanya kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha Wilaya yao ya Mbinga inakuwa na miundombinu ya uhakika ili mazao wanayoyalima hasa kahawa inalifikia soko kwa urahisi na kwa bei nafuu. Mimi niwapongeze sana na nawahakikishieni kwamba nikiwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Mheshimiwa Waziri wangu tutahakikisha dhamira yenu inakamilika katika kipindi hiki cha miaka mitano kwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, kwanza naomba tuikamilishe na suala la tunaikamilisha lini kwa maana ya kutoa tarehe sio rahisi sana kwa sababu kwa sasa tupo katika hatua ya kumpata huyo mkandarasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mtuamini kwamba tuna nia ya dhati, kazi hiyo tutaifanya na tutaisimamia na itakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili, naomba niwajulishe Waheshimiwa Wabunge wote wa Wilaya ya Mbinga kuanzia Mheshimiwa Mtondo Msuha, Mheshimiwa Stella Manyanya na Mheshimiwa Sixtus Mapunda kwamba mwaka huu tunaanza kuijenga ile barabara ya kutoka Mbinga - Mbamba Bay.
Naomba mtupe fursa tuikamilishe barabara hii. Mtakumbuka ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kutembea kwa taxi kutoka Mtwara hadi Mbamba Bay na kutoka Bukoba hadi Mtwara itakuwa imekamilika kikamilifu kabisa. Baada ya hapo, nawahakikishia nguvu zetu zote tutakuwa tunaelekeza katika barabara hizo zingine ikiwa ni pamoja na hii barabara ya kutoka Unyoni hadi Mango kupitia vijiji ambavyo Mheshimiwa Mtondo Msuha amevitaja.

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Miaka kadhaa iliyopita Serikali iliahidi kuwa itajenga barabara ya kutoka Kitai Wilayani Mbinga hadi Lituhi Wilayani Nyasa kwa kiwango cha lami, lakini hadi sasa wananchi hawaelewi kinachoendelea juu ya ujenzi huo:- Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Mbinga na Nyasa juu ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali nayo pia imeahidi ujenzi wa barabara ya Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo - Lumecha - Namtumbo Songea katika kiwango cha lami. Sasa ni muda barabara hiyo bado haijaanza kujengwa.
Swali langu, ni lini sasa hii kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itakamilika na barabara hii kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dokta Hadji Mponda, Mbunge wa Malinyi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie Wabunge wote wanaohusika na barabara hii ya kutoka Ifakara - Malinyi - Namtumbo - Songea kwamba Serikali ina nia ya dhati ya kuanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Labda nimhakikishie tu kwamba kazi iliyofanyika hadi sasa ni kubwa. Unafahamu kwamba kipande kile cha kutoka Lumecha - Londo kimeshakamilika kwa maana kufunguliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile tumebakabiza kilometa 4 tu kukamilisha kuifungua hii barabara, wakati kazi ya feasibility study na detail design ikiendelea kufanyika. Nikuhakikishie kazi hii ya feasibility study na detail design pamoja na kipande hiki cha kilometa 4 kilichobaki cha kufunguliwa barabara hii itakamilika katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 unaoanza Ijumaa.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Miaka kadhaa iliyopita Serikali iliahidi kuwa itajenga barabara ya kutoka Kitai Wilayani Mbinga hadi Lituhi Wilayani Nyasa kwa kiwango cha lami, lakini hadi sasa wananchi hawaelewi kinachoendelea juu ya ujenzi huo:- Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Mbinga na Nyasa juu ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujua tu ahadi ya ujenzi wa barabara ya kutoka Nyamwiswa – Bunda kwa kiwango cha lami ni ya muda mrefu toka mwaka 2000. Sasa napenda kujua ni lini Mkandarasi wa kujenga barabara hiyo ataanza kazi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumbukumbu yangu, hii barabara imeshaanza kujengwa. Tatizo kiwango tunachokijenga ni kidogo, labda ndiyo anachokilalamikia Mheshimiwa Mbunge. Nimhakikishie kama kumbukumbu zangu zitakosea atanisamehe, lakini kuanza tumeshaanza. Namwahidi tu kwamba, tutaongeza kasi ili hatimaye barabara hii ikamilike kujengwa katika muda mfupi.