Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Ifakara – Mahenge utaanza kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara hii swali lilkuwa ni lini ujenzi utaanza. Lakini barabara hii haina tofauti na barabara nyingine ya kutoka Kilosa kuja Mikumi ambayo ipo kwenye Ilani ya mwaka 2015/2020, 2020/2025 na ipo kwenye bajeti hii ya mwaka huu na bado tunaambiwa kwama ipo kwenye maandalizi. Sasa Je, ni lini ujenzi wa barabara hii unaenda kuanza? Nashukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nniaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Londo, Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti ni kweli barabara ile aliyotaja ya Kilosa Mikumi ipo kwenye Ilani na imetengewa fedha kwa bajeti inayokuja. Kwa hiyo, tunaamini kwamba tutakapoanza utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2021/2022 basi hii barabara itakuwa moja ya barabara ambazo zitaendelea kujengwa kwani tayari barabara hii upande inapoanzia eneo la hapa njia panda barabara ya Morogoro – Dodoma; tayari imeshajengwa mpaka Kilosa na tunaendelea na ujenzi. Kwa hiyo kipande kilichobaki cha Kilosa kwenda Mikumi barabara hii naamini nayo itaanza kujengwa katika bajeti tunayoanza kuitekeleza. Ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Ifakara – Mahenge utaanza kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu wa barabara hii inayotajwa pia upo kwenye kufungua Mkoa wa Lindi na kwa ajili ya uchumi wa Kusini. Lakini Serikali mara nyingi imekuwa ikiongea tu kuhusu eneo hili la kusahau junction inayoanzia maeneo ya Mbingu kule Ifakara inapita Liwale inakwenda kutokea Nachingwea mpaka Masasi na yenyewe ni muhimu kama ilivyo hivyo.

Sasa Serikali itueleza hapa kwa sababu tulikuwa tukiongea kuhusu barabara hii mara nyingi kwamba ni lini sasa pamoja na nia njema ya kutaka kutengeneza hii barabara inayokwenda Ruvuma mtamalizia na ile junction inayokuja kutokea Liwale kuja Nachingwea mpaka Lindi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwambe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja kuanzia Mbingu, Liwale hadi Nachingwea ni barabara ambayo kweli ipo imeahidiwa lakini ujenzi wa barabara hii utategemea na upatikanaji wa fedha. Kwa hiyo, kwanza itatakiwa ifanyiwe upembuzi na baadaye usanifu wa kina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tumepitisha bajeti, kwa hiyo, itategemea na upatikanaji wa fedha ambayo kama itapatikana fedha basi miradi hii itaanza kutekelezwa sawasawa na miradi mingine. Lakini kikubwa ni ufinyu wa bajeti ambao unafanya barabara hizi zote haziwezi kutekelezwa kwa wakati mmoja. Lakini ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii inajengwa ili kuweza kufungua maeneo haya na pia kupunguza umbali ambao wananchi wanasafiri kuzungukia barabara ambazo ni ndefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.