Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KACHAUKA K.n.y. MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, Serikali iko tayari kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Makata - Liwale ambao wameanzisha ujenzi wa Chuo cha VETA na madarasa mawili yamekamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante pamoja na majibu haya ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale. Swali la kwanza, je, Serikali inatuahidi nini katika bajeti ijayo?

Lakini swali la pili; je, Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri atakuwa tayari kwenda kuona juhudi za wananchi Liwale lakini wakati wa kwenda au wa kurudi apitie Kilwa Masoko kwa ajili ya kuona changamoto zilizopo katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kassinge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ijayo kwasababu tuna ujenzi wa vyuo hivi 29 katika Wilaya 29 nchini. Katika bajeti ijayo tumepanga kununua vifaa ambavyo vitakavyowezesha sasa vyuo hivi ifikapo Januari, 2022 viweze kuanza kutoa huduma kwa maana kwamba vianze kutoa huduma ya kufundisha wanafunzi katika maeneo hayo. Hilo ndio lengo letu katika bajeti ijayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hili suala la pili la kuweza kwenda kuona maeneo haya nipo tayari, baada ya Bunge hili la Bajeti tutapanga ziara na hata jana tulikuwa na uwekeaji wa jiwe la msingi katika chuo chetu cha VETA pale katika Wilaya ya Ruangwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo pamoja na maeneo mengine na dhamira ya dhati kabisa kuhakikisha kwamba nafika Liwale, lakini nitafika Ruangwa, lakini vilevile nitafika kwa ndugu yangu Kassinge pale Kilwa Kusini kuweza kuona changamoto zilizopo na kwa namna gani ya kuweza kuzitatua. Ahsante. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KACHAUKA K.n.y. MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza:- Je, Serikali iko tayari kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Makata - Liwale ambao wameanzisha ujenzi wa Chuo cha VETA na madarasa mawili yamekamilika?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Swali langu lilikuwa, kwanza niwapongeze Makete tumepata Chuo cha VETA ambacho kwa Mkoa mzima wa Njombe kipo Makete tu. Lakini tuna changamoto ya kozi ambazo mnazitoa pale nyingi hazipo kwenye soko kwa mfano; hatuna kozi ya ufundi magari, hatuna kozi ya ufundi umeme majumbani, hatuna kozi ya ambayo inashughulikia masuala ya mabomba kwa maana ya ufundi mabomba.

Je, ni lini Serikali italeta hizo kozi ambazo kwa sasa ziko kwenye soko Tanzania kutokana na hizi ambazo tunatekeleza kwenye Ilani hasa hasa suala la umeme vijijini ambapo wana Makete wengi wangependa wafanye kazi kwenye mazingira hayo lakini kozi hizo hazipo? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba nijibu swali la Mheshimiwa Sanga, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna kozi ambazo ziko standard karibu kwenye maeneo mengi sana na kwa sasa hivi kunaonekana kama kuna uhitaji mkubwa sana kwenye baadhi ya maeneo kwamba tubadilishe kozi kuendana na maeneo yale yalivyo. Mfano, nilikuwa kule Mwanza katika Visiwa vile vya Ukerewe hakuna kozi zinazohusiana na masuala ya uvuvi. Lakini wakasema sasa ni muhimu sana tuweze kuianzisha kozi ile. Nimtoe wasi wasi Mheshimiwa Sanga kwamba jambo hili tunakwenda kulifanyia kazi, tutakwenda kukaa na uongozi wa Mkoa na kuhakikisha kwamba kozi hizi ambazo ni muhimu, lakini vilevile zenye soko kwenye maeneo hayo zinaenda kuanzishwa mara moja. Ahsante.