Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA K.n.y. MHE. ENG.STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bonde la Mto Ruhuhu lililopo Kata ya Lituhi linawanufaisha wananchi kwa kuweka miundombinu ya Kilimo na umwagiliaji?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile Mkoa wa Ruvuma umejaaliwa kuwa na mito mingi mikubwa, mito hiyo ipo pia katika eneo la Jimbo la Madaba moja katika mito mikubwa ni mto huo Ruhuhu, lakini kuna Mto Hanga.

Nini sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha maeneo hayo yote yanayofaa kwa umwagiliaji tunakuwa na miundombinu mikubwa na rafiki itakayoboresha kilimo cha mpunga na kilimo cha umwagiliaji katika ujumla wake maeneo ya Mkoa wetu wa Ruvuma?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mhagama kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali sasa hivi tunachokifanya ni kufanya review ya master plan yote ya umwagiliaji na kubadili mfumo wa Tume yetu ya Umwagiliaji ili kuweza kupata tija katika miradi yetu ya umwagiliaji na kuwa na gharama ambazo ni affordable na kuna value for money, hili ni jambo la kwanza.

La pili tunachokifanya sasa hivi tutatambua maeneo ya kimkakati ambayo Serikali itaenda kuwekeza yenyewe 100% na maeneo mengine ya umwagiliaji tuta-encourage sekta binafsi kuweza kufanya hayo maeneo na kuwekeza sekta binafsi kwa makubaliano ya long term ili kupunguza mzigo. Kwasababu siyo lazima kila sehemu ndiyo Serikali iweze kujenga yenyewe. Kwa hiyo, tunafanya jitihada za namna hiyo kuweza kuzi-cruster hii miradi ya umwagiliaji katika maeneo ambayo itawekeza sekta binafsi na maeneo ambayo Serikali itakwenda kuwekeza kwenye miradi mikubwa ambayo sekta binafsi haiwezi kuwekeza.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA K.n.y. MHE. ENG.STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bonde la Mto Ruhuhu lililopo Kata ya Lituhi linawanufaisha wananchi kwa kuweka miundombinu ya Kilimo na umwagiliaji?

Supplementary Question 2

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Serikali imeanza kuwekeza fedha za awali katika scheme za umwagiliaji kama scheme ya Ilemba, Ng’ongo, Sakalilo, Mititi na Bonde la Ilembo; ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia hizi scheme ambazo tayari imeanza na ipo katika mipango yake?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza priority namba moja katika bajeti ya mwaka huu tunayoanza nayo ni kukamilisha scheme ambazo tulishapeleka fedha na ambazo hazijakamilika. Kwa hiyo, scheme zote zipo karibu 1000 na kidogo ambazo zimepelekewa fedha nusu/nusu hazijakamilika. Kwa hiyo, hii ni priority ya kwanza.

Kwa hiyo, nimuhakikikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine kote ambako tulishapeleka fedha na kuanza kuzifanyia kazi, tunafanya tathmini ya mapungufu yaliyopo na ukamilishaji, kwa sababu zipo scheme ambazo tulienda kujenga mifereji wakati hatujatengeneza bwawa la kuweza kuhifadhi maji, kwa hiyo, ni wastage of resources. Kwa hiyo, tunafanya hiyo tathmini na kuitambua na tuta-communicate officially kwa Wabunge kila mmoja kuweza kufahamu scheme zake zilizoko kwenye eneo lake ni lini zitaanza kufanyiwa kazi na zipo kwa sababu tuna-resource ndogo, tutapeleka scale of preference na kuchagua zipi tunaanza nazo kuweza kuzifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, priority ya pili ya bajeti yetu ya mwaka huu kwenye fedha tulizotenga ni kuwekeza fedha kwenye mashamba 13 ya kuzalisha mbegu ili tuondokane na tatizo la mbegu katika nchi kwa sababu tuna mashamba ya kuzalisha mbegu, lakini hatujawekea miundombinu. Serikali inakwenda shambani kuandaa mbegu wakati ambapo mkulima naye yupo shambani. Kwa hiyo, ni jambo la aibu, tumeamua kwamba resource tunaweka namba moja kwenye mbegu; namba mbili kukamilisha scheme ambazo tulipelekeka fedha kidogo kidogo. (Makofi)