Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni akiwa Mkoani Mwanza aliahidi kuifanya Mwanza kuwa Geneva; lakini Mwanza Mjini kuna barabara zenye urefu wa kilometa 546.1 ambapo kilometa 43.67 zina lami na kilometa 3.556 zimejengwa na mawe:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza barabara zenye kiwango cha lami? (b) Je, Serikali itashirikiana vipi na Halmashauri za Ilemela na Nyamagana ili kuboresha barabara zilizopo chini ya halmashauri hizo kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya Nyakato – Buswelu - Mhonze ina urefu wa kilometa 25 ambapo kilometa 6 ni urefu wa barabara kutokea Nyakato National kuelekea Buswelu Wilayani. Serikali pamoja na kutoa kilometa 2.4 ambapo katika hizo kilometa 1 ilitengwa shilingi milioni 500 na sasa wametenga shilingi bilioni 1.16. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza kilometa 4 ili kuweza kuifanya barabara hiyo kufika Wilayani?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Rais aliyepita wa Awamu ya Nne aliahidi kuijenga barabara ya Kamanga – Sengerema kwa kiwango cha lami na barabara hiyo inawasaidia wanawake wa Vijiji vya Katungulu, Kasomeko pamoja na Nyamililo kufanya kazi zao za kiuchumi. Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kiteto Zawadi Koshuma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, umuhimu wa kuongeza fedha ili kuhakikisha ile barabara inafika Makao Makuu ya Wilaya, Wizara inautambua na ndiyo maana hata katika mwaka wa 2016/2017 tumeongeza kiwango cha fedha tulichotenga. Nimhakikishie Mheshimiwa Kiteto Zawadi Koshuma kwamba juhudi zake hizo zitazaa matunda kwa kadri fedha zitakapokuwa zinapatikana mwaka hadi mwaka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili kwa barabara ya Kamanga – Sengerema, naomba tu nimjulishe kwamba yale ambayo tuliyaeleza katika swali kama hilo hilo hapo nyuma tulidhamiria. Tuna dhamira ya kujenga hiyo barabara na tutaendelea kwa hatua zile ambazo tulizieleza. Tutaanza na masuala ya feasibility study pamoja na detail design kama ambavyo Wizara imepanga.

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni akiwa Mkoani Mwanza aliahidi kuifanya Mwanza kuwa Geneva; lakini Mwanza Mjini kuna barabara zenye urefu wa kilometa 546.1 ambapo kilometa 43.67 zina lami na kilometa 3.556 zimejengwa na mawe:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza barabara zenye kiwango cha lami? (b) Je, Serikali itashirikiana vipi na Halmashauri za Ilemela na Nyamagana ili kuboresha barabara zilizopo chini ya halmashauri hizo kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wakandarasi hawa wakati wanaendelea kujenga barabara hizi katika maeneo yetu mbalimbali wamekuwa wakitumia bidhaa mbalimbali ikiwemo mawe, mchanga, maji, vibarua na vifusi; na kwa kuwa Serikali katika mikataba yao inakuwa kwenye BOQ imeweka bei maalum ambayo inawalipa wakandarasi hawa lakini wengi wakandarasi hawa wamekuwa wakichukua bidhaa hizo katika vijiji vyetu bure au kwa bei ndogo sana na hivyo kuwakosesha wananchi wa maeneo hayo kunufaika na bidhaa hizo. Je, ni lini Serikali sasa itatoa angalau bei elekezi kwa wakandarasi wote wanaofanya kazi za kujenga barabara waweze kununua mawe na bidhaa nyingine ili wananchi nao wafaidike kama watu wa madini na maeneo mengine?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Omary, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumkumbusha Mheshimiwa Mbunge kwamba wanaojenga hizo barabara ni sisi wenyewe, ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kodi zetu. Kwa kweli masuala haya lazima tukubaliane tunaya-balance vipi kati ya upatikanaji wa material ya kujengea barabara pamoja na upatikanaji wa fedha za kujenga barabara yenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Omary kwamba Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambayo ndiyo yenye dhamana ya kutoa bei ya fidia kwa maeneo ambayo yanatwaliwa na Serikali italifanyia kazi suala hili lakini siyo rahisi kutoa bei elekezi kwa sababu nchi ni kubwa na kila mahali pana thamani yake tofauti sana. Vinginevyo itakuwa ni kitabu kikubwa sana ambacho kitaorodhesha kila mahali na thamani ilivyo kwa nchi nzima, itakuwa ni ngumu. Nadhani njia inayotumika ambayo kwa kawaida ni mazungumzo kati ya halmashauri na wale ambao wanahusika na eneo linalotwaliwa pamoja na mkandarasi ni nzuri zaidi kufikia muafaka wa bei ya kutumika katika kununua eneo linalotumika kwa ajili ya upatikanaji wa hayo material ya kujengea barabara.
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini naomba niongezee kwamba Serikali haiwezi ikaanza kununua udongo ama changarawe kwa sababu miradi hii tutashindwa kuijenga. Sasa hivi Serikali inatumia kila kilometa 1 kujenga barabara kwa takribani shilingi bilioni 1. Sasa kama tutaanza kununua udongo, changarawe tutashindwa kuwajengea wananchi wetu hawa barabara hizi. Serikali inalofanya tu ni kulipa fidia hasa kwenye structure kwa mfano majengo na maeneo mengine lakini hatuwezi kuanza kununua udongo, changarawe na vitu vingine tutatishindwa kujenga miundombinu kwa ajili ya Watanzania.

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni akiwa Mkoani Mwanza aliahidi kuifanya Mwanza kuwa Geneva; lakini Mwanza Mjini kuna barabara zenye urefu wa kilometa 546.1 ambapo kilometa 43.67 zina lami na kilometa 3.556 zimejengwa na mawe:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza barabara zenye kiwango cha lami? (b) Je, Serikali itashirikiana vipi na Halmashauri za Ilemela na Nyamagana ili kuboresha barabara zilizopo chini ya halmashauri hizo kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ipo ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati akiomba kura kwa wananchi wa Biharamuro ya kujenga barabara kilometa 4 - 5 kwa kiwango cha lami kwenye Mji wa Biharamuro. Naomba kufahamu kutoka Serikalini kwamba utekelezaji wa ahadi hiyo umefikia wapi? Ahsante

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Biharamuro, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi anayoongelea ni kweli ilitolewa na Mheshimiwa Rais na kwa kweli ahadi hiyo ilianzia kutoka Serikali ya Awamu ya Nne na ni kwa ajili ya eneo hilo lakini vilevile eneo jirani ambalo Mheshimiwa Dkt. Kalemani anatoka, ahadi hizo zote tutazitekeleza. Lini, itategemea na upatikanaji wa fedha kwa sababu utekelezaji wa ahadi hizo unahitaji rasilimali fedha. Kwa hiyo, naomba nikuahidi ahadi hizo tutazitekeleza na nikuahidi miaka mitano hii ambayo ndiyo tumepewa hii dhamana ya kuwajengea Watanzania miundombinu na kutekeleza ahadi zote ambazo viongozi wetu walizitoa nikuhahikikishie tutazitekeleza.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni akiwa Mkoani Mwanza aliahidi kuifanya Mwanza kuwa Geneva; lakini Mwanza Mjini kuna barabara zenye urefu wa kilometa 546.1 ambapo kilometa 43.67 zina lami na kilometa 3.556 zimejengwa na mawe:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza barabara zenye kiwango cha lami? (b) Je, Serikali itashirikiana vipi na Halmashauri za Ilemela na Nyamagana ili kuboresha barabara zilizopo chini ya halmashauri hizo kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Sera ya Serikali ni kuunganisha barabara za mikoa na za wilaya kwa lami lakini katika Mkoa wetu wa Iringa, Wilaya ya Kilolo ni wilaya ambayo toka mwaka 2002 imepata hadhi ya kuwa wilaya mpaka leo hii haijaweza kuunganishwa kwa lami kutoka yalipo makao makuu. Ni lini sasa Serikali itaunganisha wilaya hii na makao makuu kwa lami ili hii sera iweze kutimia?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Wilaya ya Kilolo haijaunganishwa na barabara ya lami kama ambavyo Mbunge wa Kilolo na Mbunge wa Viti Maalum Mheshimiwa Ritta Kabati wamekuwa wakifuatilia suala hili ofisini kwetu na nyakati zote tumekuwa tukiwaahidi kwamba tutafuatilia. Kwanza Mheshimiwa Rais alipopita lile eneo hiyo pia ilikuwa ni sehemu ya ahadi yake licha ya kwamba hii ni ahadi ya kiujumla kwa wilaya zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie maadam dhamira yetu ni kuhakikisha miundombinu inajengwa na ahadi zote za viongozi wetu tunazitekeleza atupe muda ili tutakapopata ratiba kamili ya suala hili tutatekeleza. Mnafahamu tumeanza kwa kiwango fulani, ni kiwango ambacho hakitoshelezi nakubali kama ambavyo Mheshimiwa Mwamoto amekuwa akinisukuma kila wakati kuhusu hilo suala. Niwahakikishie wote Mheshimiwa Mwamoto na Mheshimiwa Ritta Kabati kwamba ahadi hiyo tutaitekeleza kama ambavyo tumeongea nao tukiwa maofisini.