Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Pamoja na juhudi kubwa ya Serikali ya Awamu ya Nne katika kutekeleza ahadi ya miradi katika Ilani ya Uchaguzi bado haikuweza kukamilisha ahadi zote ilizotoa:- Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mpango gani wa kukamilisha ahadi za miradi iliyoachwa na Serikali ya Awamu ya Nne bila kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Ni kweli kama alivyosema Naibu Waziri kwamba Serikali itaendelea kutekeleza ahadi za Serikali ya Awamu ya Tano. Naomba nimuulize kama anafahamu pia kwamba kuna mradi wa barabara kutoka Singida – Irongero – Mtinko - Meria mpaka inaungana na Mkoa wa Manyara ambayo pia ilikuwa ni ahadi ya Rais aliyemaliza muda wake. Je, yuko tayari pia kuiingiza barabara hii katika mchakato wa kuikamilisha mapema ili wananchi wale wasiendelee kusubiri kwa muda mrefu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Mlata kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, anachosema Mheshimiwa Mlata ni kweli na juzi nilikuwa katika Mkoa wa Singida na hiyo barabara ni miongoni mwa barabara ambazo nimeziona. Jambo la kufurahisha zaidi katika barabara hiyo, Waziri mweye dhamana ya Miundombinu alipita na kuna daraja la Sibiti ambapo amesema katika bajeti ya mwaka huu mchakato wa lile daraja tayari umeshatengewa fedha kuona ni jinsi gani litaweza kujengwa. Kwa hiyo, commitment ya Serikali ni kuhakikisha kwamba barabara ile inajengwa na tukijua wazi kwamba kwa watu wanaoenda kwa mfano katika Mkoa wa Simiyu, kitendo cha kupita Nzega ni changamoto kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mlata kwamba jambo hili liko katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi. Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali kuangalia katika miaka mitano tutafanya vipi ili mradi wananchi waweze kupata fursa za maendeleo.

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Pamoja na juhudi kubwa ya Serikali ya Awamu ya Nne katika kutekeleza ahadi ya miradi katika Ilani ya Uchaguzi bado haikuweza kukamilisha ahadi zote ilizotoa:- Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mpango gani wa kukamilisha ahadi za miradi iliyoachwa na Serikali ya Awamu ya Nne bila kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo hayajaweza kutia matumaini makubwa, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilitenga fedha kwa bajeti ya 2015/2016 kwa ajili ya miradi ya kipaumbele na ya kilio cha muda mrefu cha wananchi hususani mradi wa maji katika Hospitali yetu ya Rufaa ya Haydom ambayo inatumikia mikoa zaidi ya minne ikiwepo Manyara, Singida, Simiyu na kwingineko na ambayo hadi leo haijakamilika kutokana na kukosa fedha lakini pia ikiwepo na bwawa la maji la Dongobeshi ambacho ni kilio cha muda mrefu. Hata Mheshimiwa Rais alipopita wakati wa kampeni walimpa mabango na ni kilio cha muda mrefu kweli kweli na sasa mkandarasi ameacha hiyo kazi kwa sababu pia hajalipwa fedha zake. Je, nini kauli ya Serikali kuhusu miradi hii ya kipaumbele cha wananchi na kilio cha muda mrefu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, miradi ya maendeleo ambayo inatengewa fedha kwa kipindi kilichopita huwa zile fedha zinakwenda kwenye dharura nyingine ambazo zinapangwa na Serikali kuliko fedha kwenda kwenye miradi iliyokusudiwa kama ilivyoidhinishwa na Bunge. Je, Serikali ina mikakati gani sasa kwa bajeti ya 2016/2017 kuhakikisha kwamba fedha zote zinakwenda kwenye miradi yenye kilio cha muda mrefu cha wananchi kuliko kwenda kwenye miradi ya dharura kama ambavyo ilikwenda kwenye miradi ya maabara kipindi kilichopita?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martha kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya maji ya Dongobeshi pamoja na bwawa la Dongobeshi, ni kweli kwamba miradi hii ilitambuliwa katika programu ya kwanza ya maendeleo ya sekta ya maji ambayo ilianza mwaka 2006/2007 na imekamilika mwaka 2015. Ilianza kutekelezwa na iko katika hatua mbalimbali lakini kutokana na matatizo kidogo ya fedha basi miradi hiyo haikukamilika kwa wakati. Tayari tumeshaanza kupeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo ya Dongobeshi na katika bajeti ya mwaka huu tumetenga fedha na tumeelekeza kwamba kwanza lazima tukamilishe miradi ambayo ilikuwa inaendelea ndiyo tuanze miradi mingine mipya. Kwa hiyo, tutahakikisha tunashirikiana na Mheshimiwa Mbunge kuhakikisha kwamba tunakamilisha miradi hii na hasa ule ambao utakuwa unapeleka maji kwenye Hospitali Teule ya Dongobeshi.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kweli kabisa kuna miradi mingi ya kipaumbele ambayo ilishindwa kupelekewa fedha katika awamu iliyopita lakini Mheshimiwa Mbunge wewe mwenyewe ni shahidi kwamba mwaka 2015 Serikali ilikuwa na majukumu mengi sana na yalikuwa ni majukumu yale ya muhimu kama vile suala la uchaguzi, kulikuwa na suala la kutengeneza Katiba, hivi vitu ni vya muhimu, ndiyo uhai wa nchi kwa hiyo fedha ilipelekwa kwenye maeneo haya. Nikuhakikishie kwamba kwa sasa majukumu hayo yameshakamilika na tayari tumeongeza ukusanyaji wa fedha. Kwa hiyo, miradi yote ambayo ilikuwa imeainishwa na kupewa kipaumbele tutahakikisha kwamba inakamilishwa.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Pamoja na juhudi kubwa ya Serikali ya Awamu ya Nne katika kutekeleza ahadi ya miradi katika Ilani ya Uchaguzi bado haikuweza kukamilisha ahadi zote ilizotoa:- Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mpango gani wa kukamilisha ahadi za miradi iliyoachwa na Serikali ya Awamu ya Nne bila kukamilika?

Supplementary Question 3

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, zipo ahadi nyingi zilizotolewa na viongozi kuanzia Awamu ya Tatu, Awamu ya Nne na sasa Awamu ya Tano. Je, kwa nini Serikali isiweke utaratibu wa kuandaa ahadi hizo kwa kutengeneza kitabu cha mpango wa utekelezaji na sisi Wabunge tukagawiwa?

Name

Dr. Abdallah Saleh Possi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Malocha kwa kifupi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni ushauri mzuri na Serikali tunaupokea.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:- Pamoja na juhudi kubwa ya Serikali ya Awamu ya Nne katika kutekeleza ahadi ya miradi katika Ilani ya Uchaguzi bado haikuweza kukamilisha ahadi zote ilizotoa:- Je, Serikali ya Awamu ya Tano ina mpango gani wa kukamilisha ahadi za miradi iliyoachwa na Serikali ya Awamu ya Nne bila kukamilika?

Supplementary Question 4

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mji wa Korogwe unapitiwa na Mto Pangani katikati ya mji, je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kwa kuutumia mto ule kuwapatia watu wananchi wa Mji wa Korogwe maji hasa ikizingatiwa kwamba wana shida ya maji, wanaangalia mto lakini maji hawayapati?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji na Umwagiliaji inatekeleza mradi wa HTM na tayari tumeshaahidiwa fedha kwa wafadhili na usanifu wa mradi huo umekamilika. Bahati nzuri ni kwamba usanifu huo utachukua maji kutoka Mto pangani tena karibu kabisa na eneo la Korogwe.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nakuahidi kwamba wakati tunachukua maji kutoka katika Mto wa Pangani hatuwezi kuacha kupeleka maji sehemu yenye chanzo. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba eneo la Korogwe pia litapatiwa maji kutokana na huo mradi wa HTM.