Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:- Kumekuwa na utaratibu mbovu na Mawaziri wa Elimu kuingilia shughuli za mitaala kwa kubadilisha mitaala, mfumo wa madaraja na hata aina ya mitihani hasa kuweka maswali ya kuchagua katika somo la hisabati:- Je, ni lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya NECTA ili Bunge libadili Sheria ya Baraza kifungu cha 30 ili kuondoa nguvu ya Waziri ya kutoa maelezo bila kuhoji na hata bila kushirikisha wataalam wa elimu?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nadhani kuna shida ya mawasiliano, wakati nilipoletewa nifanye marekebisho niliandika ni kifungu namba 20 na nikazungushia na sheria ninayo.
Mheshimiwa Spika, jambo la pili, naomba niseme tu kwamba nasikitika sana kwa majibu niliyopewa. Haya majibu, nimeuliza kuhusiana na mitaala utamsikiliza katika majibu Mheshimiwa Naibu Waziri hakugusa kabisa mitaala. Nimeuliza juu ya maswali ya kuchagua ya masomo ya hesabu, hakugusia. Nimeuliza kipengele cha tatu cha Waziri kutoa maelekezo, Sheria inasema The Minister may give the Council directions of a general or specific character and the Council shall give effect to every such direction, hakuna kushauriana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nitaomba niulize maswali mawili ya nyongeza wakati anajiandaa kunipa majibu sahihi kwenye swali hili.
Swali la kwanza, kwa nini Waziri wanang‟ang‟ania na kipengele cha kutunga mambo yao wao yaani kusema leo watu watumie GPA au watumie division, yaani leo waseme tufanye sayansi, hesabu na physics pamoja, biology na kemia. Haya wanakubali yawepo lakini hii ya ushauri na wataalam hawataki kwa nini naomba tujibu?
Mheshimiwa Spika, jambo la pili, kwa nini Wizara hii inakataa kushirikisha Wataalam katika maamuzi ya kupima wanafunzi wetu, atueleza hapa wale watoto ambao walipimwa kwa kiwango cha kutumia GPA na wakapewa vyeti, sasa hivi Waziri ametoa tamko lake hapa anasema sasa ni division, hivi vyeti anavi-compromise namna gani katika elimu? Naomba atusaidie mambo hayo.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa amelalamika kwamba hatujazungumzia masuala ya kuchagua majibu ya hesabu na mambo mengine. Kimsingi najibu kadri ya swali lilivyowekwa, kule uliweka utangulizi lakini swali lako ulisema kwa nini kifungu hiki kisiondolewe na ndicho nilichokujibu.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo kimsingi lazima ieleweke Mheshimiwa Waziri hafanyi maamuzi kwa kukurupuka bila kupata taarifa mbalimbali zinazomwezesha kufanya maamuzi hayo. Hata hivyo si kwamba kila jambo linalofanyika kwenye Wizara linakuwa limetangazwa, lakini hatua mbalimbali zinakuwa zimechukuliwa, ikizingatiwa kwamba Wizara hii inazingatia sana masuala ya kitaalam.
Mheshimiwa Spika, katika maswali ya kuchagua majibu ya hesabu, siku za nyuma wanafunzi walikuwa hivyo hivyo wanachagua, lakini walikuwa na sehemu ya kufanyia kazi halafu wanachagua. Hata sasa hivi wanapewa karatasi wanazofanyia kazi, lakini wanachagua kwa ku-shade kwa misingi kwamba kwa siku za nyuma kwa sababu walikuwa wanasahihisha karatasi kwa mikono, sasa hivi inasahihisha mashine, ndiyo maana baada ya kuchagua lile jibu lake sahihi anakwenda ku-shade na kuweka ili mashine iweze kusahihisha.
Hiyo imepunguza kazi iliyokuwa inatakiwa kufanyika na watu 3000, sasa inafanyika na watu 300. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali lingine Mheshimiwa amezungumzia kwamba kwa nini tumeking‟ang‟ania hicho kifungu. Siyo suala la kuking‟ang‟ania, kifungu hiki kikitumika vibaya ndipo kina kasoro, lakini kama kinatumika vizuri kinaharakisha utendaji na maamuzi ya Wizara.
Kwa hiyo, nasimamia katika sura hiyo kusema kwamba, Waziri aliyeaminiwa na Serikali kutekeleza majukumu yake ipasavyo, naamini atakitumia kifungu hiki inavyostahili. Hata hivyo, baada ya kubadilisha GPA kuweka katika division, kimsingi hakuna athari zilizopatikana kwa sababu bado kuna uwiano katika hizo alama na wanafunzi hawa bado wanaendelea kupata haki zao kama kawaida.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:- Kumekuwa na utaratibu mbovu na Mawaziri wa Elimu kuingilia shughuli za mitaala kwa kubadilisha mitaala, mfumo wa madaraja na hata aina ya mitihani hasa kuweka maswali ya kuchagua katika somo la hisabati:- Je, ni lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya NECTA ili Bunge libadili Sheria ya Baraza kifungu cha 30 ili kuondoa nguvu ya Waziri ya kutoa maelezo bila kuhoji na hata bila kushirikisha wataalam wa elimu?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi ili niulize swali moja dogo la nyongeza. Ukiangalia katika majibu amesema kwamba, mabadiliko haya yanafanywa baada ya utafiti, baada ya wataalam kuleta taarifa mbalimbali. Naomba kujua GPA imetumika kuanzia mwaka 2013 na sasa 2015 tayari imebadilika imekuwa madaraja, yaani ilikuwa madaraja ikaja GPA within a year, sasa naomba kujua huo utafiti ulifanywa lini hasa ikizingatiwa wataalam walioko Baraza la Mitihani ni wale wale kuanzia Mtendaji Mkuu? Kwa hiyo, naomba kujua huo utafiti umefanywa wapi na mazingira ya jamii ni watu gani walitaka hasa wabadilishwe kutoka madaraja kwenda GPA na kurudi tena kwenye madaraja?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, kimsingi wakati huu mfumo wa GPA unaanza kutumika ulikuwa pia uanze katika misingi ya majaribio. Lengo lilikuwa ni kufanya kwamba, toka mwanafunzi anapokuwa katika hatua za awali yaani katika sekondari na kuendelea aweze kuwa na mfumo mmoja unaokwenda mpaka vyuo vikuu. Kwa sababu unakuta vyuo vikuu tunatumia GPA, lakini huku chini tulikuwa tunatumia division na kwa kweli lilikuwa ni jambo jema tu, lakini kukawa na maneno tena ya malalamiko mbalimbali kupitia vyombo, kama jana ulivyoona Mheshimiwa Susan Lyimo ulisema kwamba hata magazeti na yenyewe pia ni nyaraka sahihi kutumika katika Bunge letu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, maneno haya yamekuwa yakitoka katika pressure mbalimbali na hata hivyo baada ya kupitisha huu mfumo wa division hii juzi, nafahamu kuna magazeti mengi hata Waheshimiwa Wabunge walipongeza. Sasa mjue tu kwamba ni hayo mawazo yetu tunayoyatoa na Serikali ni wajibu wake kufanyia kazi. Ahsante sana.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri ametoa ufafanuzi mzuri, ningependa tu kuongezea pale alipojibu Mheshimiwa Naibu Waziri, kwamba kama alivyoeleza Mheshimiwa Naibu Waziri hata huu mfumo wa GPA ulitokana na maoni ya wadau. Hata hivyo, baada ya Serikali kutekeleza, wadau tena wakawa wameleta malalamiko, kwa hiyo, lazima Serikali tuweze kuyafanyia kazi kadri mahitaji yanavyojitokeza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kuwasihi Watanzania tunapopewa nafasi ya kutoa maoni, tuitumie nafasi hiyo kutoa maoni ya dhati kabisa. Kwa sababu tunatoa maoni, Serikali inapotekeleza halafu tena kuna kuwa na malalamiko kama ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri amesema. Vilevile ningependa pia kuchukua nafasi hii kumwambia Mheshimiwa Ndugu yangu Mwita Waitara kwamba hii Sheria ya Baraza la Mitihani akisoma kifungu cha nne, kinatoa fursa kwa wananchi kutoa maoni kwa Baraza la Mitihani kuhusiana na masuala ya uendeshaji mitihani na maoni yao yanazingatiwa. (Makofi)
Kwa hiyo, siyo kwamba tu imempa mamlaka Waziri wa Elimu, lakini vilevile imetoa fursa kwa maoni kutolewa na naomba kama kuna maoni yoyote ambayo yana tija, basi wahakikishe na yatafanyiwa kazi.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:- Kumekuwa na utaratibu mbovu na Mawaziri wa Elimu kuingilia shughuli za mitaala kwa kubadilisha mitaala, mfumo wa madaraja na hata aina ya mitihani hasa kuweka maswali ya kuchagua katika somo la hisabati:- Je, ni lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya NECTA ili Bunge libadili Sheria ya Baraza kifungu cha 30 ili kuondoa nguvu ya Waziri ya kutoa maelezo bila kuhoji na hata bila kushirikisha wataalam wa elimu?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Chama cha Mapinduzi kwenye Ilani yake kimesema kwamba shule ni bure kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha nne. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuyaachia matokeo ya wanafunzi ambao wanadaiwa na NECTA kwa sasa?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa hoja yake, niseme kwamba hilo suala tumelipokea, tutalifanyia kazi, halafu tutakuja kutoa majibu