Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Capt. Abbas Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Fuoni

Primary Question

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI Aliuliza:- (a) Je, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ina Taasisi ngapi na zipi zina uwezo wa kujiendesha zenyewe? (b) Je, ni zipi kati ya Taasisi hizo zinapeleka gawio Serikalini? (c) Je, gawio ni takwa la kisheria?

Supplementary Question 1

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa zipo baadhi ya Taasisi za Serikali ambazo zinakidhi vigezo vya mkopo kutoka katika mabenki ya kibiashara. Je, taasisi ya aina hizo ni ruksa kukopa kwa lengo na madhumini ya kugharamia miradi yao bila kuingiliwa na Serikali?

Swali la pili, zile taasisi kama alivyojibu Mheshimiwa Naibu Waziri, hazipeleki chochote na ni mzigo kwa vile ni tegemezi katika suala zima la ruzuku. Je, ni busara kuendelea na aina hiyo ya taasisi? Ahsante sana.(Makofi)

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa alivyojibu swali la msingi, lakini pili, napenda kujibu swali la Captain Abbas Ali Mwinyi, Mbunge wa Fuoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba zipo taasisi ambazo zinakidhi vigezo vya kukopa Serikalini, lakini taasisi hizi zina mwenyewe ambaye ni Msajili wa Hazina. Kwa hiyo, japokuwa kazi hizi zinakidhi vigezo vya kukopa bado zinahitaji ruhusa ya Serikali kupitia kwa Msajili wa Hazina kabla ya kuweza kupata mikopo ili kuweza kuteleleza miradi yake ambayo nayo inabidi ipitiwe na kupitishwa na Wizara na kuingizwa kwenye bajeti kama ambavyo tumepanga hapa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ni kuhusu taasisi tegemezi, taasisi tegemezi tulizonazo ni zile ambazo zinatoa huduma ambazo zinategemea ruzuku ya Serikali. Kwa hiyo, ni muhimu ziendelee kuwepo kama Taasisi za Bodi za Usajili ambazo hazizalishi mapato bali zinatoa huduma kwa ajili ya udhibiti. Ahsante.

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI Aliuliza:- (a) Je, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ina Taasisi ngapi na zipi zina uwezo wa kujiendesha zenyewe? (b) Je, ni zipi kati ya Taasisi hizo zinapeleka gawio Serikalini? (c) Je, gawio ni takwa la kisheria?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ya swali la nyongeza na nitauliza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Shirika la Huduma za Mawasiliano Nchini, yaani TTCL inadai Taasisi za Serikali zaidi ya bilioni 82 za Kitanzania na Shirika la Posta linadai zaidi ya bilioni 1.5 kwa Taasisi za Serikali nchini.

Je, nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wadaiwa wote sugu wanalipa madeni yao haraka ili mashirika haya yaweze kujiendesha kiushindani? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kushukuru sana kwa kunipa fursa hii nikiunganisha na kadondoo ulikokasema nakushukuru sana kwa mwongozo huo, na ni washukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa jinsi ambavyo wamesimama na Serikali pamoja na Wizara ya Fedha katika kutoa elimu ya sheria tulizozipitisha na tumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuzisaini.

Mheshimiwa Spika, nikirejea kwenye jambo alilokuwa ameliuliza Mheshimiwa Mbunge ni kweli tumeshapokea deni la TTCL na tuna hata baadhi ya wengine wanaoidai na wenyewe TTCL wamelazimika kufika hata Wizarani kwetu kusema tunaidai TTCL, lakini TTCL wanasema na wenyewe wanazidai Taasisi za Serikali, mnatusaidiaje.

Mheshimiwa Spika, nikiri mbele ya Bunge lako Tukufu kwamba jambo hili tumelipokea na jambo ambalo ameleta Mheshimiwa Mbunge tumelipokea tunaendelea kufanyia kazi na uchambuzi na namna ya kushughulika na madeni haya madogo pamoja na haya makubwa na tutaziangalia hizi taasisi ambazo tutaongea ndani ya Serikali kuziangalia hizi taasisi za Serikali kwa sababu Serikali ni moja tuweze kuona ni namna gani tunalisaidia shirika letu hili ili na lenyewe liweze kufanya hizo commitment ambazo zimefanya katika hizo taasisi zingine.