Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka injini mpya ya Kivuko cha MV Kitunda - Lindi Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimshukuru Waziri kwa majibu ya Serikali ambayo ameyatoa, lakini naiomba Serikali kwamba MV Kitunda ni kivuko ambacho kinawasaidia sana wananchi wa Lindi kuvusha magari na bidhaa mbalimbali na shughuli za kiuchumi zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa ninavyoongea kivuko kimesimama kwa muda wa wiki moja changamoto iliyopo injini Na.2 kwenye selecta valve kuna shida. Naiomba Serikali kusaidia kwa haraka kupatikana kwa valve hii ili kivuko kiendelee kufanya kazi na wananchi waendelee kutumia kivuko hicho.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatambua umuhimu wa kivuko hiki cha MV Kitunda na kutokana na umuhimu wake tayari Wizara kupitia TEMESA imeshapeleka boti na hata hivi kutokana kwa kweli na ufuatiliaji wa karibu sana wa Mheshimiwa Hamida, Mbunge wa Lindi Mjini, tumepeleka boti kwa ajili ya kusaidia changamoto ambazo zinajitokeza.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mbunge kwamba, kama tulivyoahidi kivuko hiki kitatengenezwa, lakini wakati kiko matengenezo boti hilo litaendelea kubaki hapo kwa ajili ya kusaidiana na boti la Halmashauri ya Lindi ili kuhakikisha kwamba eneo hilo halisimami kufanya kazi kati ya Lindi na Kitunda. Ahsante.