Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapima maeneo yote ya umma ikiwemo Shule, Vituo vya Afya na Zahanati kwa kutumia Sheria Na. 4 na Na. 5 ili kuondokana na matatizo ya migogoro ya mipaka kwa Wananchi, lakini pia kuondokana na hoja za ukaguzi ambazo zaidi ya asilimia 90 ya Halmashauri wanazipata?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nilikuwa naomba Serikali itoe kauli, hasa kwa kutumia Sheria Na. 5 ambako halmashauri nyingi zipo huko kupima ardhi kwa kutumia hati za kimila; kwa sababu ukiangalia kwenye statement nyingi za halmashauri zetu inaonekana hoja kubwa ya migogoro ni kutokuwa na hati za kumiliki ardhi.

Je, Serikali ina mpango gani kwa kutumia hati miliki za kimila kuhakikisha maeneo yote ya umma, shule na vituo vya afya yanapimwa kama inavyotakiwa?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa; ya kwamba hoja yake ni ya msingi na ni nzuri, lakini, shule ambazo zinamilikiwa na halmashauri haziwezi kupimwa kwa hati ya kimila, zile zinapimwa chini ya Sheria Na. 4; kwa maana ya kwenda kwenye general land. Kwa hiyo kama hitaji hilo lipo ni kwamba ni halmashauri pia, tuone namna ya kuhakikisha, na Wizara ilishaelekeza, kwamba taasisi zote za umma zipimwe. Huwezi kuipima kwa kutumia Sheria Na. 4.

Mheshimiwa Spika, niombe tu kwamba halmashauri zijipange katika kutumia Sheria Na. 5 kwasababu ile imeshaingia kwenye general land na haiwezekani tena kukaribisha kwenye umiliki wa kijiji. (Makofi)

SPIKA: Kwa hiyo Mheshimiwa Naibu Waziri zikishapimwa zitapewa hati each na hati ile inalipiwa kodi ya ardhi, au inakuwaje?

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, watapewa, na kodi inayolipwa sasa hivi; tulibadilisha sheria hapa mwaka 2019, wanalipa token tu, shilingi 5,000 kwa mwaka badala ya kutumia ukubwa wa eneo. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapima maeneo yote ya umma ikiwemo Shule, Vituo vya Afya na Zahanati kwa kutumia Sheria Na. 4 na Na. 5 ili kuondokana na matatizo ya migogoro ya mipaka kwa Wananchi, lakini pia kuondokana na hoja za ukaguzi ambazo zaidi ya asilimia 90 ya Halmashauri wanazipata?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na maeneo ya umma kama ambavyo Serikali imeelekeza na kuzielekeza halmashauri kupima lakini migogoro mingine mingi tunapata sana kwenye taasisi kama Majeshi na Magereza. Kwa mfano, Iringa pale Kata ya Isakalilo ina mgogoro mkubwa wa ardhi wa mipaka pamoja na wananchi na Jeshi la Magereza.

Je, Serikali inahusiana vipi na Wizara nyingine kuhakikisha pia inatatua hilo?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pia nimshukuru na muuliza swali.

Mheshimiwa Spika, Wizara katika zoezi zima la utatuzi wa migogoro kila tunapokwenda kwenye zoezi la migogoro utatuzi wake tunashirikisha halmashauri husika na tunashirikisha pande zote mbili. Na unapotaka kutatua mgogoro lazima uwe na lile Gazeti la Serikali linalotangaza mipaka ya eneo husika; na hauwezi kuutatua mgogoro ule unless mmekwenda kwenye site na kuweza kutafsiri. Kwa hiyo kazi kama Wizara tunayoifanya katika migogoro hiyo ya taasisi na wananchi tunaendelea kuitatua kwa kuzingatia sheria zinasema nini na mara nyingi tunapokwenda, Halmashauri husika inahusishwa na pande mbili zinazogombana zinahusika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama Kata ya Isakalilo na Magereza bado kuna mgogoro naelekeza wapimaji wa Mkoa wa Iringa wafike kule site ili waone namna ya kutafsiri mpaka ili kuondoa mgogoro huo.