Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali italeta Mradi wa Kuhifadhi Mazingira Mufindi katika chanzo cha maji cha Mto Ruaha na shamba la miti la Sao Hill?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini kwa kuwa Serikali inatambua jambo hili ambalo nimesema nataka kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, ni lini Serikali itamaliza kero ya maji katika ukanda huu wa baridi ambapo kuna vyanzo hivyo na hivyo kufanya tatizo la maji kuwa historia katika maeneo ya Kata za Migohole, Kasanga, Mninga, Mtwango, Idete pamoja na maeneo mengine ya Makungu, Kiyowela na Mtambula?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la nyongeza, kwa kuwa suala la maji ni mtambuka na ni muhimu sana, katika eneo hilo la Mufindi Kusini kulikuwa na mradi ulikuwa unaitwa Imani, ni lini Serikali itakwenda kuufufua kwa kuboresha miundombinu ili wananchi waliokuwa wananufaika waweze kunufaika especially kwenye Kata za Ihoanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Nyololo, Maduma na Itandula?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba majibu.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda sana kumpongeza Mheshimiwa Mbunge David Kihenzile kwa namna ambavyo amekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa matatizo ya maji katika Jimbo lake. Hii ni kawaida yake kwa sababu pia amekuwa akitoa ushirikiano mkubwa kwangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ameuliza tatizo la maji litakoma lini, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama Ilani ya CCM inavyotutaka Serikali kuhakikisha kufika mwaka 2025 tuweze kukamilisha maji vijijini kwa 95%, kwa maeneo ya Mufindi tutahakikisha mwaka ujao wa fedha tunakuja kuweka nguvu ya kutosha ili libaki kuwa historia.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile suala la kufufua miundombinu, katika maeneo mbalimbali suala hili linaendelea kutekelezwa. Katika eneo la Mufindi, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kabla ya mwaka huu wa fedha haujaisha tutakuwa tumeshafanya kwa sehemu kubwa kuona miundombinu chakavu tunaitoa na tunaweka miundombinu ambayo inaendana na matumizi ya sasa.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali italeta Mradi wa Kuhifadhi Mazingira Mufindi katika chanzo cha maji cha Mto Ruaha na shamba la miti la Sao Hill?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Liwale unakua kwa haraka sana na mahitaji ya maji yamekuwa ni makubwa na uhaba wa maji ni mkubwa sana. Bajeti iliyopita tuliletewa fedha shilingi milioni 100 kwa ajili ya kutafuta chanzo cha pili cha maji cha Mji wa Liwale lakini mpaka leo tunaambiwa DDCA hawana nafasi ya kuja Liwale. Ni lini Serikali watakuja sasa kutafuta chanzo cha pili cha maji kwa ajili ya Mji wa Liwale?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Liwale. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo anafuatilia na amekiri tumewapatia shilingi milioni 100. Nachoweza kumwambia hawa DDCA nitawasimamia na nitahakikisha ndani ya mwezi huu Aprili watakuja ili waweze kuona kwamba shughuli ambayo ilipaswa kufanyika basi sasa inaenda kutekelezwa.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali italeta Mradi wa Kuhifadhi Mazingira Mufindi katika chanzo cha maji cha Mto Ruaha na shamba la miti la Sao Hill?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Kilolo inafanana kabisa na Wilaya ya Mufindi; na kwa kuwa vyanzo vya mito kama Mto Mtitu na Mto Lukosi vinachangia kwa kiwango kikubwa kwenye vyanzo vikubwa vya mabwawa na pia ni vyanzo ambavyo vinasaidia katika nchi yetu. Je, ni lini Wizara itajibu kiu ya wananchi kwa kutatua tatizo la maji kwa kutoa fedha kwenye Mradi wa Mto Mtitu ambapo tayari RUWASA walishatoa na maji hayo yatafika hadi Iringa Mjini lakini pia yatahudumia kata zaidi ya 15 za Wilaya ya Kilolo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge alivyokiri kwamba tayari shughuli zinaendelea pale kupitia Wakala wetu wa Maji Vijijini (RUWASA). Kadiri tunavyopata fedha tunahakikisha tunagawa katika maeneo yote ambayo miradi ipo kwenye utekelezaji.

Kwa hiyo, pamoja na mradi huu ambao upo katika Jimbo lake na ni Jimbo ambalo tumelitendea haki kwa sehemu kubwa sana, tutaendelea kupeleka fedha kadiri tunavyopata ili kuhakikisha mito yote ambayo mmebarikiwa watu wa Kilolo na maeneo mengine yote tunashughulikia kwa wakati. Lengo la Wizara ni kuhakikisha wananchi wanapata maji bombani na si vinginevyo.