Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE Aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha dhana ya elimu bure kwa kutoa elimu bure kuanzia Shule ya Msingi hadi Kidato cha Tano na cha Sita?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika swali langu la msingi nimesema kwa kuwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi imefanya kazi nzuri ya kutoa elimu bure katika shule za msingi mpaka sekondari; na kwa kuwa Waraka wa Serikali Namba 5 wa 2015 unasema, elimu bure ni kutoka shule ya msingi mpaka sekondari; na kwa kuwa kidato cha tano na kidato cha sita ni sekondari, ni kitu gani kinazuia Serikali kutoa elimu bure kwa kidato cha tano na cha sita kwa sababu ni sekondari hiyohiyo ambayo inazungumzwa?

Mheshimiwa Spika, umesikia Wabunge wengi wanasema hapa, Mheshimiwa Oliver, Mheshimiwa Sanga na wengine kwamba imetajwa katika Waraka kwamba elimu bure ni shule ya msingi mpaka sekondari, kidato cha tano na cha sita ni sekondari. Sasa ni lini Serikali itatoa elimu bure kwa kidato cha tano na cha sita?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, tumezungumza humu mara nyingi sana na hili swali naliuliza kama mara ya tano sasa, Shule ya Sekondari za Unyali, Mkomalilo, Mihingo, Esparanto, Makongoro, Wamamta, Salama, hazina walimu wa sayansi. Watu wanachanga, tumejenga majengo mazuri watoto wanasoma lakini hawana walimu. Lini Serikali itapeleka walimu kwenye shule hizi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Getere, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Waraka Namba 5 wa mwaka 2015 wa Elimu Msingi, unaelekeza kwamba itakuwa elimu bure kuanzia elimu ya awali mpaka kidato cha nne. Mheshimiwa Mbunge anauliza kwa nini kidato cha tano na cha sita hakipo katika mpango huo. Ni kweli, kidato cha tano na cha sita hakipo kwenye mpango huu lakini naomba nilieleze Bunge lako tukufu kuwa tunaendelea kuboresha bajeti yetu ya Serikali, mpango huu unaweza kufikiwa iwapo tu bajeti ya Serikali itakuwa imekaa sawasawa.

Mheshimiwa Spika, kama mnavyofahamu, baada ya kupata fursa hii ya kutoa elimu bure usajili wetu wa wanafunzi, tuchukulie mfano wa darasa la kwanza, umeweza kuongezeka kutoka wanafunzi 1,300,000 mwaka 2014 mpaka wanafunzi 2,070,000 mwaka 2016/2017. Utaona kuna ongezeko hilo kubwa kutokana na Sera hii ya Elimu Bure. Kwa hiyo, upatikanaji wa fedha utatupeleka kuhakikisha kwamba kidato cha tano na cha sita tunawaingiza katika mpango huu.

Mheshimiwa Spika, halikadhalika napenda kueleza kwa zile kaya ambazo ni maskini tuna mpango wetu wa TASAF ambapo kwa mwanafunzi wa shule ya msingi anapata shilingi 12,000/= kwa mwezi na wale wa sekondari wanapata shilingi 16,000/= kwa mwezi. Hawa wanaweza wakasaidiwa katika mpango huu ili kuhakikisha kwamba tunaweza kufikia yale malengo ya kulipi hiyo ada ndogo ambayo inalipwa katika kidato cha tano na cha sita.

Mheshimiwa Spika, katika swali la pili, shule alizozitaja na hasa kuhusu wale walimu wa sayansi, Mheshimiwa Waziri Mkuu hapa ametoka kujibu swali kama hilo katika kipindi kifupi kilichopita, Serikali tayari imeshaanza mpango wa kuajiri walimu. Katika mwaka 2020 tumeajiri zaidi ya walimu 8,000 wameshapelekwa shuleni. Sasa hivi Serikali iko kwenye mchakato wa kuajiri tena walimu 5,000 ambao katika kipindi kifupi kijacho tunaamini shule hizi alizozitaja zinaweza zikapata hao walimu wa sayansi.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE Aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha dhana ya elimu bure kwa kutoa elimu bure kuanzia Shule ya Msingi hadi Kidato cha Tano na cha Sita?

Supplementary Question 2

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, Mkoani Arusha kuna shule ya St. Jude, ni shule ambayo inasomesha watoto wenye mazingira magumu na kwa kupitia misaada ya watu mbalimbali huko duniani. Siku za karibuni TRA imeenda kwenye account ya shule hiyo imechukua fedha na kusababisha shule hiyo kupata misukosuko na kufungwa kiasi ambacho watoto wenye mazingira magumu wamekosa nafasi ya kwenda kusoma pamoja. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa ahueni kwa shule hii ili suala la elimu ambayo ni kipaumbele chetu liweze kupewa mstari wa mbele?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama alivyobainisha uwepo wa shule hiyo na changamoto zilizotokea kuhusiana na wenzetu wa TRA, suala hili naomba tulichukue twende tukalifanyie kazi na badaye tutaweza kutoa majibu muafaka kwa Mheshimiwa Mbunge na Mkoa wa Arusha kwa ujumla. Ahsante.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE Aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha dhana ya elimu bure kwa kutoa elimu bure kuanzia Shule ya Msingi hadi Kidato cha Tano na cha Sita?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, wakati Mheshimiwa Naibu Waziri anajibu maswali amezungumzia neno elimu bure, lakini najua anajua tofauti kati ya elimu bure na elimu bila kulipa ada. Nazungumza hivi kwa sababu kinachofanyika mashuleni huko wanafunzi na wazazi wanatozwa fedha ama za kulipa mlinzi ama za kulipa maji ama za kulipa walimu wa sayansi ambao wanawatafuta wa ziada ama masomo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nataka Serikali iweke hoja wazi kabisa hapa mezani, kinachofanyika ni elimu bila kulipa ile ada ya Sh.20,000 na Sh.70,000 na siyo elimu bure, ili wazazi wanapochangia huko wajue kwamba wao kwenye mchakato wa elimu ya Tanzania wana-stake yao ya kuchangia na Serikali ina stake yake ya kuchangia. Kwa hiyo, aweke wazi hapa ni elimu bila ada na sio elimu bure. Sasa kwa tafsiri ya kamusi bure ina maana yake na ada ina maana yake. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya msingi, Waraka Namba 5 wa mwaka 2015 ulikuwa unaeleza kwamba elimu bila malipo kwa elimu ya awali mpaka kidato cha nne.

Mheshimiwa Spika, lakini kuna michango ambayo huenda ikawa inatokea huko ambayo ni michango ya hiariā€¦

SPIKA: Ngoja Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa hiyo, ni elimu bila malipo siyo elimu bure.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, elimu bila malipo. (Makofi)

SPIKA: Nisikuwekee maneno mdomoni Mheshimiwa Naibu Waziri, nilitaka tu uweke vizuri, hebu rudia wewe mwenyewe.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, nilikuwa nazungumzia Waraka Namba 5 wa mwaka 2015 unaeleza kwamba elimu ya awali mpaka elimu ya kidato cha nne itakuwa ni elimu bila malipo, tafsiri yake ni elimu bure. Kwa hiyo, waraka huo unaeleza hivyo.

Mheshimiwa Spika, katika muktadha huo, amezungumzia kwamba kuna michango wazazi wanachangishwa ya walinzi, usafi au ya vitu vingine, naomba nilieleze Bunge lako Tukufu kuwa Serikali katika Waraka ule imebainisha wazi kwamba michango ile yote ambayo mzazi alikuwa anachangia katika kipindi cha nyuma katika maeneo haya ya elimu ya awali kwa hivi sasa haipo na gharama hizo zinakwenda Serikalini.

Sambamba na hilo, nadhani keshawahi kusikika Mheshimiwa Waziri wa Elimu lakini Mheshimiwa Rais ameshawahi kuzungumza mara nyingi sana, kama mzazi au mlezi ana mchango wa aina yoyote ambao anaona bora au inafaa mchango huo autoe ni vema aufikishe au auwasilishe kwa Mkurugenzi ambapo yeye atapanga kitu gani cha kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.