Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA Aliuliza:- Je, ni lini uzalishaji wa madini ya niobium utaanza katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Nashukuru vile vile kwa majibu ya Serikali ambayo yanaleta matumaini sasa kwa matumizi ya chuma na matumizi ya niobium na kuwepo kwa kiwanda cha FerroNiobium hapa hapa kwetu nchini. Swali la kwanza, je, sasa kwa vile haya madini inaonesha kuwa ni madini ya viwandani ambayo yatachanganywa pamoja na chuma na ikiwezekena pamoja na aluminium, ni lini sasa Serikali itahakikisha kuwa uzalishaji wa chuma ikiwemo machimbo ya Liganga na Mchuchuma yataanza mara moja ili yaweze kutengenezwa FerroNiobium hapa hapa nchini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa sababu haya madini yanatengeneza FerroNiobium, je, viwanda vya FerroNiobium vinaangukia kwenye Sheria za Uwekezaji za EPZ? Nashukuru.

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, nipende kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba madini ya Niobium yatachanganywa pamoja na madini ya chuma ili kutengeneza muunganiko huu wa FerroNiobium na ni kweli kwamba Serikali kwa sasa iko katika mazungumzo rasmi na mwekezaji anayewekeza katika Mradi wa Liganga ili hatimaye tuweze kuanza mradi huo kwa sababu umechelewa sana. Kwa hiyo napenda kuamini kwamba maongezi haya yatakapokuwa yamekamilika baina ya mwekezaji wa Liganga na suala likiwa hasa katika mikataba, basi mtanzuko huo utakapokuwa umeondoka tunapenda kuamini kwamba itakuwa ni fursa ya kuendeleza mradi wa Niobium ambayo itachanganywa na chuma chetu cha Liganga.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la Mheshimiwa Mbunge, ni kweli kwamba madini mengine yana matumizi katika viwanda na pia ndiyo iliyokuwa ni sticking point katika mazungumzo yetu na mwekezaji. Sasa ukiangalia madini ya Niobium katika periodic table ni transition metals, kwa hiyo tunapaswa tuyatambue kwamba ni madini ya metali na ukiyabadilisha yakaonekana kwamba kwa vile yana matumizi katika viwanda tozo inayotozwa ya royalty madini ya viwanda ni asilimia tatu, madini ya metali ni asilimia sita.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hapa napo tulikuwa na mkinzano na mwekezaji kwamba matumizi ya baadaye yasitusababishe tukaanza kuonesha kwamba hayako katika group la metali, kwa sababu hata dhahabu nayo pamoja na kwamba ni metali inaweza ikapata matumizi katika viwanda. Kwa hiyo tukaona kwamba hebu tuendelee kuuangalia upande wa kwamba madini ya niobium ni madini ya metali, royalty yake ibakie kuwa asilimia sita hata kama baada ya hapo itakuja kuchanganywa na kuwa FerroNiobium. Kwa hiyo hayo ni maongezi ambayo tumeongea na mwekezaji na tunaamini kwamba tutafikia muafaka. Ahsante. (Makofi)