Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. SILLO D. BARAN Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza migogoro ya mipaka kati ya Hifadhi ya Tarangire na Vijiji vya Gijedabung, Ayamango, Gedamar na Mwada katika Jimbo la Babati Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. SILLO D. BARAN: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa bado mgogoro huu unafurukuta katika vijiji nilivyovitaja, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufanya ziara ili wananchi wapate kutatua migogoro hii?

Mheshimiwa Spika, swali la piliā€¦

SPIKA: Kwa nini Waheshimiwa mnamgombea Mheshimiwa Waziri kama mpira wa kona aje majimboni kwenu?

Endelea Mheshimiwa swali la pili.

MHE. SILLO D. BARAN: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mwaka 2019 ulitokea uharibifu wa mazao ya wananchi katika vijiji nilivyovitaja ambao ulisababishwa na wanyama hasa tembo, je, ni lini Serikali itawalipa kifuta jasho wananchi hawa ambao mashamba yao yameathirika?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sillo Daniel Baran, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Sillo juu ya kuongozana na mimi maana ni majukumu yangu ya kazi, hivyo hilo niko tayari baada ya Bunge lako hili Tukufu tutaenda naye. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili la nyongeza ambalo ameuliza juu ya uharibifu wa wanyama wakali; Serikali inawajali sana wananchi wake na inatambua kwamba kuna uharibifu wa wanyama wakali ambao wamekuwa wakiwasumbua wananchi hasa wale ambao wanakuwa wamepanda mazao yao na wanyama wakali hususan tembo huenda katika maeneo hayo na kuharibu.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kutambua hilo ilianzisha Mfuko ambao huwa tunalipa kifuta jasho au kifuta machozi. Kifuta machozi au kifuta jasho ni kwa ajili ya kuwapoza wale ambao wanakuwa wameathirika na changamoto hii ya wanyama wakali. Hivyo, hadi Machi, 2020, Serikali ilikuwa imeshalipa jumla ya shilingi bilioni 5.9 kwa ajili ya kifuta machozi au kifuta jasho kwa wananchi hawa ambao wamekuwa wakiathirika na changamoto ya wanyama wakali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kuhakiki madai yote ambayo wananchi wameathirika na changamoto hii ya wanyama wakali na itaendelea kulipa kadri inavyopata taarifa.