Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu ilijengwa na mradi wa GGM kusaidia kundi kubwa la wasichana wasome Wilayani Geita, shule hii ina hosteli za kutosha na nyumba za walimu. Je, ni kwa nini shule hiyo imebaki kuwa shule ya kutwa wakati mazingira yake yanafaa kuwa sekondari ya bweni?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimwia Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa amejibu kwamba ni jukumu la Mkurugenzi kuandika na kuomba shule hii iwe ya bweni; ni lini sasa ofisi yake itamuagiza Mkurugenzi huyo ambaye anaonekana hafahamu kama yeye ndiyo anawajibika ili aweze kuandika barua na kuomba? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa mwezi huu au mwisho wa mwezi ujao, Serikali itaajiri walimu wapya na uchunguzi wangu shule nyingi za Jimbo la Geita za Vijijini hazina walimu; ni maagizo gani Serikali itatoa kwa walimu wapya ili waelekezwe zaidi Vijijini badala ya Mjini? Nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini nitamwagiza Mkurugenzi, nadhani huu mchakato unaanza kwenu ninyi katika Baraza la Halmashauri, kwa sababau hii ni need ambayo ninyi mnahitaji. Kama Baraza la Madiwani mtaona kwamba ninyi mnahitaji hilo, baadaye Mkurugenzi ataandika barua, akishaandika barua maana yake ikifika katika Wizara ya Elimu, Wizara ya Elimu inatuma wataalamu chini ya Kamishna wake, wataenda kufanya uhakiki, baadaye vigezo vikishapita ndiyo shule hiyo itasajiliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niliache suala hili katika Baraza lenu la Madiwani, maana inawezekana Mkurugenzi akaandika halafu Madiwani wakamgeukia kwa nini umegeuza shule hii kwa mahitaji yako bila kutaka maelekezo kutoka katika Baraza la Madiwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba niache jambo hili katika mchakato wa Baraza la Madiwani litaamua kumwelekeza Mkurugenzi aweze kufanya haraka kupeleka Wizara ya Elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo kuhusu suala la upelekaji wa walimu. Ni kweli hivi sasa tupo katika mchakato siyo muda mrefu sana tutaajiri walimu wapya. Katika kuajiri, kuna Mikoa ambayo inabidi ipewe kipaumbele, tuna Mikoa takribani sita ambayo ina changamoto kubwa sana ya walimu ikiwepo ni pamoja na Mkoa wa Kigoma, Rukwa, Katavi na Geita. Kwa hiyo, katika maeneo hayo yote tutaangalia walimu watakaopatikana basi tutawapa maelekezo maalum. Wakifika pale lazima waende maeneo ambayo wananchi wanataka huduma, bahati mbaya wakati mwingine inajitokeza walimu tukiwaajiri, tukiwapeleka kule inawezekena wengine sisi Waheshimiwa tunapeleka vi-memo ili yule mwalimu arudi mjini, tunasababisha maeneo ya vijijini yanakosa walimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Ofisi ya Rais TAMISEMI tunaelekeza walimu watakaopangwa lazima waende kufanya kazi katika maeneo husika.

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu ilijengwa na mradi wa GGM kusaidia kundi kubwa la wasichana wasome Wilayani Geita, shule hii ina hosteli za kutosha na nyumba za walimu. Je, ni kwa nini shule hiyo imebaki kuwa shule ya kutwa wakati mazingira yake yanafaa kuwa sekondari ya bweni?

Supplementary Question 2

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii.
Kwa kuwa, hili suala la Geita linafanana sana na tatizo lililoko Wilaya ya Kakonko, Jimbo la Buyungu kutokuwa na sekondari kabisa ya A-level na tunayo shule moja ya sekondari Kakonko ambayo ikiwekewa miundombinu mizuri yafaa kuwa na A-level.
Je, Waziri yuko tayari kuweka kipaumbele katika shule ya sekondari Kakonko ili ipewe hadhi ya kuwa na A-level itakayokuwa ya kwanza katika Wilaya ya Kakonko?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba Serikali kutoa kipaumbele, nadhani hili tumetoa maagizo katika maeneo mbalimbali, kwa sababu tuna shule nyingi sana za kata. Shule hizi za kata watoto wakifaulu lazima waende Advance Level. Tunapokuwa na shule za kata wanafunzi wanishia form four maana yake wakikosa nafasi za kwenda advance, shule zikiwa chache vijana inawezekana wakafaulu lakini wakakosa nafasi.
Kwa hiyo, haya ni maelelekezo ya maeneo yote, ndiyo maana mwaka huu hata ukiangalia bajeti yetu tumezungumza, tunakarabati zile shule kongwe, hali kadhalika kuhamasisha maeneo mbalimbali kujenga shule. Kwa sababu tunajua eneo lile jiografia yake ni ngumu tutaangalia jinsi gani ya kufanya maeneo ambayo hayana shule za Kata tuyape msukumo shule za advance level ili kwamba watoto wakifaulu katika shule a O level waende advance level katika maeneo husika.