Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.DKT. PINDI H. CHANA Aliuliza:- Serikali imekuwa ikisaidia sana vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu nchini kupitia Halmashauri za Wilaya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Mifuko hiyo ili kutoa viwango vikubwa zaidi vya mikopo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, kaka yangu Dkt. Dugange kutoka Wanging’ombe, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika jibu la msingi tumesema kwamba inatokana na mapato ya kipindi husika asilimia 10, napigia mstari neno kipindi husika. Naomba kupendekeza maboresho kwamba halmashauri zinapokusanya pesa, let say, ya 2020; baada ya yale marejesho, inapokwenda 2021, ichukuliwe ile ya 2020 ichanganywe na 2021, ule Mfuko uwe Cumulative Revolving Fund na fedha ziwe nyingi. Halafu tunapokwenda 2022 tunachanganya ile miaka miwili, yaani Mfuko unakuwa mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, hatuoni sasa wakati umefika wa kukusanya ule Mfuko wa kukopesha ukawa ni Revolving Fund?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, hatuoni kama wakati umefika, maafisa wanaosimamia mikopo hii wakapata elimu kama Maafisa Mikopo katika benki zetu ambao mara nyingi ni Maafisa Maendeleo ya Jamii kama Loan Officer?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na mikopo ya asilimia 10 kutolewa kwa kipindi husika, kama ambavyo jibu la msingi limesema, ni kweli kipindi husika cha makusanyo ndicho ambacho tumesisitiza kama Serikali kuhakikisha halmashauri zinatenga asilimia 10 kwa ajili ya mikopo kwa makundi hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mikopo hiyo ni ile ambayo inahusisha wajasiriamali ambao fedha zile ambazo zinakopeshwa zinatakiwa kurejeshwa ili kutoa fursa kwa vikundi vingine kuweza kukopa fedha hizo. Kwa hiyo, napokea ushauri mzuri wa Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana kwamba tutaendelea kusimamia, kuhakikisha kwamba mapato yanayokusanywa kwa kipindi husika, asilimia 10 inatengwa na kupelekwa kwenye vikundi hivyo ili kuwawezesha kuendesha shughuli zao za ujasiriamali kwa ufanisi mkubwa zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana naMfuko huu kuwa Revolving Fund, kimsingi Mfuko huu ni Revolving Fund mpaka sasa, kwa sababu baada ya kukopeshwa, vikundi vinarejesha kiasi cha fedha kilichokopwa bila riba kwa ajili ya kuwawezesha wakopaji wengine waweze kunufaika na mfuko huo. Kwa hiyo, tutaendelea kuelimisha jamii yetu na vikundi vya wajasiriamali kuweza kurejesha mikopo hiyo ili na wengine wapate fursa hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na mchango na ushauri wa kuwa na maofisa ambao wanapata mafunzo mbalimbali ya mifumo hii katika benki na maeneo mengine, tunauchukua ushauri huo.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.DKT. PINDI H. CHANA Aliuliza:- Serikali imekuwa ikisaidia sana vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu nchini kupitia Halmashauri za Wilaya:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Mifuko hiyo ili kutoa viwango vikubwa zaidi vya mikopo?

Supplementary Question 2

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mikopo hii inahusu watu wenye ulemavu; na swali langu ni kwamba, inapotokea mtu mwenye ulemavu ambaye hawezi kufanya shughuli yoyote, lakini ana mlezi ambaye anamlea. Je, Serikali sasa haioni kuna sababu ya kumkopesha yule mtu ambaye anamlea mtu mwenye ulemavu ili aweze kufanya shughuli itakayomwezesha yule mtu kuweza kumlea vizuri yule mtu mwenye ulemavu? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa michango yao mikubwa mpaka tulipofikia hapa. Tukumbuke kihistoria kwamba Mfuko huu ulikuwa haufanyi vizuri, lakini kwa taarifa tuliyoitoa mwaka 2020, zaidi ya shilingi bilioni 124 ziliweza kuelekezwa katika makundi haya. Mpaka leo taarifa yetu ya miezi sita mpaka mwezi Desemba, zaidi ya shilingi bilioni 22.45 zimeelekezwa katika makundi hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, nazishukuru Kamati za Bunge hasa Kamati ya TAMISEMIna Kamati ya LAAC katika kutoa ushauri wa uboreshaji wa Kanuni na hasa makundi ya watu wenye ulemavu. Hivi sasa tume-review kanuni zetu za kuhakikisha, hata kama mlemavu ni mmoja, aweze kupata mkopo ambapo hayo yalikuwa ni maelekezo ya Bunge. Hata hivyo, tumeenda katika suala zima la uboreshaji katika eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa Wabunge, nia yetu ni kwamba Mfuko huu uende kufanya vizuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Dada Malapo, hilo ni jambo ambalo Serikali hivi sasa inalifanyia kazi, lengo likiwa, walemavu waweze kushiriki vizuri katika shughuli za kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)