Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SIKOMBI aliuliza:- Kumekuwa na wimbi kubwa la wazee ambao wanaoishi mtaani katika mazingira magumu. Je, Serikali imejipanga vipi kuweza kusaidia wasiendelee kuteseka?

Supplementary Question 1

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Serikali kutengeneza makazi ya hawa wazee lakini nasikitika kusema makazi hayo yapo kwenye hali mbaya sana hali inayo sababisha hata maana ya kuwasaidia wazee hawa isiwepo kutokana na makazi hayo kuwa na hali mbaya sana yaani mazingira siyo rafiki ni mabovu na hili swala la wazee siyo la leo wala jana ni la siku nyingi kwa nini Serikali isione ni wakati muafaka kuwawekea makazi rafiki na yaliyo bora na salama kwa maisha binadamu?

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka Matibabu bure kwa wazee lakini nichelee kusema wazee bado wanapata shida sana ya matibabu bure na bado wapo mitaani wanazurura na kuombaomba mfano mzuri ni hapa Dodoma wazee bado wana randaranda hovyo ukizingatia Dodoma ni makao Makuu ya Serikali na ndio kioo cha Nchi yetu ya Tanzania.

Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kulifanyia kazi kinaga ubaga jambo hili ili kuondokana na adha hii ya kudhalilisha wazee tukikumbuka kwamba wote sisi ni wazee watarajiwa?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuboresha Makazi ya wazee nchini kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa Wizara imeboresha majengo ya makazi 3 ya Nunge-Dar es Salaam, Njoro-Kilimanjaro na Maguu- Manyara pamoja na kuunganisha makazi 4 ya Chaz - Morogoro, Mkaseka - Lindi, Nandanga - Lindi na Nge’he – Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la Msingi, Serikali imeendelea kuweka Mikakati ya kuwahudumia Wazee Wasiojiweza nchini, hususan kuwapatia matibabu bila malipo. Kuhusu wazee wanaozurura ni kwamba wajibu wa kuwatunza wazee ni wa familia, ndugu jamaa na marafiki. Nitoe rai kwa jamii husika kuendelea kutimiza wajibu wao wa kuwatunza wazee. Aidha, Serikali itaendelea kutoa huduma za msingi kwa wazee wasiojiweza ambao hawana ndugu kupitia makazi 13 ya wazee.