Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza:- Ajali za barabarani bado zimekuwa tishio kubwa kwa maisha ya Watanzania, kutokana na ajali hizo tunapoteza nguvu kazi ya Taifa na familia nyingi zinabaki zikitaabika. Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na ajali hizo?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri je, yupo tayari kuwaeleza Watanzania ni namna gani wanatakiwa kuzitumia alama za barabarani ikiwemo pamoja na zebra cross kwa sababu sasa hivi hata kama hakuna mtu lakini kuna askari wanasimama maeneo hayo na kuwavizia watu ili wakipita wawakamate sehemu inayofuata? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kumekuwa na tabia mbaya sana ya askari wetu wa usalama barabarani kwa vijana wetu wa bodaboda na hii nadhani ni Tanzania nzima, wanapotaka kuwakamata huwa wanakimbiza na kuwachapa viboko migongani na wengine kuwavuta na wale vijana wanadondoka chini wanaumia. Ni nini tamko la Serikali kuhusu suala hili kwa sababu nia ni kuzuia ajali? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na elimu juu ya matumizi ya alama barabarani nadhani alama za barabarani ziko nyingi, kwa hiyo, kuanza kuzungumzia elimu hapa itachukua muda mrefu, lakini yeye ametoa mfano wa hii zebra cross ni kwamba utaratibu wake unatakiwa unapofika kwenye zebra cross unaangalia kulia, unaangalia kushoto, unaangalia kulia tena halafu unakata kwa mwendo wa kawaida si kwa kukimbia wala mwendo wa taratibu na huo ndio utaratibu na gari ambapo inapopita inapokuja inatakiwa itakapoona mtu amegusa kwenye ile zebra cross isimame na kumsubiri na sio kuongeza speed ili yule mtu asivuke.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kuhusiana na swali lake la pili kwamba askari wanachapa viboko, askari wa Jeshi la Polisi hawachapi viboko, mimi hiyo sijawahi kuona pahala au kusikia kwamba kuna askari wa Jeshi la Polisi amechapa viboko badoboda. Kwa hiyo naomba nisizungumze hatua kwa sababu hakuna hilo tukio ambalo tumelipokea kuhusiana na tuhuma za askari polisi kuchapa viboko waendesha bodaboda. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y. MHE. HAWA S. MWAIFUNGA) aliuliza:- Ajali za barabarani bado zimekuwa tishio kubwa kwa maisha ya Watanzania, kutokana na ajali hizo tunapoteza nguvu kazi ya Taifa na familia nyingi zinabaki zikitaabika. Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na ajali hizo?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa ajali za barabarani zimekuwa zikisababisha vifo na kuacha baadhi ya familia katika mazingira magumu kwa kupoteza wategemezi na pia wengine kupata ulemavu wa kudumu. Je, wahanga hao hulipwa bima au fidia yoyote ili kuwapunguzia machungu? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba ajali za barabarani ziwe zimesababishwa na bodaboda, bajaji, baiskeli au magari zimekuwa zikisababisha vilema kwa wananchi au hata vifo na inapotokea yule aliyeathirika kama ni kifo ama majeruhi anatakiwa kupitia Shirika la Bima ambalo ile gari imekingwa katika ajali aweze kufuatilia na mpaka aweze kulipwa mafao yake ya bima. Kwa hiyo, hili ni suala la kisheria na ninaomba Watanzania wote wafuatilie bima zao pale ambapo ajali zinatokea na pia niwaelekeze Jeshi la Polisi wamekuwa wakiwasumbua baadhi ya wananchi katika kuwapatia document muhimu ikiwemo michoro ya ajali pamoja na document zingine ambazo Mashirika ya Bima yanazihitaji ili waweze kupata bima zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia bado Tanzania hapa Watanzania bado wanalalamika na hususani hawa bodaboda. Bodaboda hawa nilishatoa maelekezo kwa mujibu wa Ilani hii ya CCM, ibara ya nne kwamba Ilani hii ya CCM kwa makusudi kabisa CCM imeamua kupambana na umasikini, kwa makusudi kabisa CCM imeamua kutengeneza ajira na ikatamka hasa kwa vijana. Ni nia ya Serikali kuwalinda vijana hawa wanaopambana na umaskini na wanaotengeneza ajira. Nikaelekeza kuanzia siku ile ya bajeti hakuna bodaboda itakayokamatwa na askari wa usalama barabarani na kupelekwa kituoni kama bodaboda hiyo haipo kwenye makundi matatu yafuatayo narudia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kundi la kwanza ni bodaboda ambayo imehusika kwenye uhalifu itapelekwa kituoni; bodaboda kundi la pili ni ile ambayo haina mwenyewe imeokotwa, imetekelezwa itapatikana na kupelekwa kituoni; na kundi la tatu ni bodaboda ambayo yenyewe imehusika kwenye ajali ama ilikuwa imeibiwa imepatikana itakuwa kama kielelezo lakini makosa ya amebeba mshikaki, hana element, side mirror sijui imekuaje, wataendelea kupigwa adhabu zao na siku saba watatafuta faini bila bodaboda zao kupelekwa kituoni na nimesema tarehe 15 kama ambavyo imeandikwa kwenye Biblia kwamba siku ya kuja kwa mwana wa adamu mwana wa Mungu aliye hai hakuna ajuaye siku wala saa nitaanza kutembelea Vituo vya Polisi na ole wao nikute bodaboda hizi nilizokataza kwa nia njema ya CCM kwa watu wake zimewekwa kituoni, ahsante sana. (Makofi)