Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Makutano-Nyamuswa- Sanzate. (a) Je, ni lini barabara ya Makutano Juu - Sanzate itakamilika? (b) Je, Serikali kupitia wataalam wake imeridhika na kiwango cha uwekaji lami katika barabara hii?

Supplementary Question 1

MHE. BONIFACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tunamshukuru Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutupa barabara ya Makutano - Sanzate na kuna kipande cha Sanzate cha kwenda Nata - Mugumu na barabara ya Nyamswa - Bunda, Bunda - Buramba, Buramba - Kisorya.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Makutano - Sanzate kama ni mkandarasi amepewa nafasi ya kumaliza barabara hi ni zaidi ya mara saba na tarehe 06.09.2018 Mheshimiwa Rais ameenda pale na akaagiza barabara hii imalizike haraka iwezekanavyo.

Sasa ni nini kifanyike sasa ili barabara hii ikamilike kwa sababu kama mkandarasi ambae tunamuita wazawa amepewa fedha, ana vifaa, ana wataalam lakini barabara haiishi. Nini kifanyike barabara hii ikamilike?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kuna barabara ya Mgeta - Sirorisimba ambayo TANROADS waliitengeneza ikabaki kilometa tisa. Nilikuwa namuomba Waziri sasa atamke kwamba hiki kipande cha kilometa tisa kitaisha lini? Ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze tu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa akifuatilia sana hii barabara lakini pia hiyo barabara aliyoitaja ya kutoka Mgeta - Sirorisimba. Ninampongeza sana na niwashukuru tu Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Mara kwa sababu siku ya Jumatano nilijibu swali kama hili hili, swali namba 377 la Mheshimiwa Agness Marwa kuonesha namna wanavyoshirikiana, lakini kuonyesha barabara hii ni kipaumbele kwenye Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nini kifanyike; kweli kumekuwepo na changamoto muda mrefu wa ukamilishaji wa barabara hii lakini labda nipende tu kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna sehemu ya kilometa 18 ilikuwa ina shida mpaka tulilazimika kubadilisha design kwa maana ile barabara ya kutoka Makutano kuja Butiama kilometa 18. Ni sehemu ambayo ilikuwa ni korofi, ni sehemu ya mlima ilikuwa na mawe mengi, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi sasa ninavyozungumza changamoto ile mkandarasi ameiondoa kwa maana yale mawe ameshayatoa na kilometa 13 sasa ameshaweka tabaka la sub-base kwa maana ya kwamba cement na mchanga wameweka kilometa 13 na kilometa sita wameshaweka base.

Nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi ni kwamba sasa kufikia Januari kama makubaliano ambayo watayakamilisha kesho, kesho kutakuwa na kikao kati ya mkandarasi na uongozi wa TANROADS Makao Makuu kwa maana ya kuijadili barabara hii muhimu. Vuta subira Mhehsimiwa Mbunge nitakupa feedback kwamba hayo makubaliano yatakuwa ya mwisho kuhakikisha kwamba tunakubaliana na barabara hii inakwenda kukamilika, kwa hiyo, usiwe na wasiwasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu barabara ya Mgeta - Sirorisimba; zipo kilometa 22 katika barabara hii. Kimsingi barabara hii inasimamiwa na TARURA, lakini kulikuwa kuna ombi maalum la Mheshimiwa Mbunge ndiyo maana nilianza kwa kumpongeza ili sasa upande wa TANROADS kuweza kusaidia barabara hii muhimu na barabara hii kilometa 22 ulifanyika ujenzi wa kuweka kokoto kilometa zote 22; lakini kuna maeneo ambayo barabara ilipanuliwa na kuweka makalavati makubwa kama sita hivi kilometa zile 13 na ikabakia kilometa tisa ambazo Mheshimiwa Mbunge unaulizia hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, na niseme tu kwamba tumekubaliana na nielekeze pia zaidi watu wa TANROADS Mkoa wa Mara hizi kilometa tisa maeneo ambayo yalikuwa yamebakia kama ni korofi waweze kumalizia na natumaini pia upande wa TARURA kuna fedha wametenga kwa ajili ya kufanya maboresho. Na niwahakikishie wananchi wa Mgeta na Sirorisimba kwamba barabara hii tunaijali na mimi mwenyewe binafsi nimefika maeneo haya na nimeongea pia na Wananchi wa Sirorisimba na Mgeta wameridhika kwa kiwango kikubwa kazi iliyofanyika kwa hiyo Mheshimiwa Getere nafahamu na unafahamu kwmaba tunafanyakazi nzuri katika maeneo yako.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Makutano-Nyamuswa- Sanzate. (a) Je, ni lini barabara ya Makutano Juu - Sanzate itakamilika? (b) Je, Serikali kupitia wataalam wake imeridhika na kiwango cha uwekaji lami katika barabara hii?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa barabara ya Puge - Ziba - Manonga hufanyiwa matengenezo mara kwa mara na kutoa gharama kubwa sana ya matengenezo hayo, je, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kujenga barabara hii kwa awamu kama ifuatavyo; kujenga kutoka Puge - Ziba - Manonga kwa kiwango cha lami angalau ianzie Ndala mpaka Ziba?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Mwanne Mchemba kwa sababu barabara hii ameifuatilia sana na imezaa matunda kwa kweli kwa sababu maeneo yote korofi tunafanya matengenezo makubwa ikiwepo ujenzi wa daraja kubwa kabisa katika Mto Manonga. Nia ya Serikali ni kuboresha maeneo haya. Kwa sasa Serikali ilikuwa inaendelea kuunganisha mikoa na Mkoa wa Tabora umeunganishwa na mikoa mingine kwa maana ya Tabora kwenda Shinyanga kuja Singida. Uvute subira tu kidogo tumeiweka kwneye mpango barabara hii na sasa eneo hili unalolisema la kutoka Ndala kwenda Ziba ni eneo muhimu ambao linapita kwenye Hospitali ya Nkinga, tutaliangalia ili tukipata fedha tuanze na eneo hili ambalo pia lina shughuli nyingi za kiuchumi. Ahsante sana.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Makutano-Nyamuswa- Sanzate. (a) Je, ni lini barabara ya Makutano Juu - Sanzate itakamilika? (b) Je, Serikali kupitia wataalam wake imeridhika na kiwango cha uwekaji lami katika barabara hii?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante wka kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Sera ya Wizara hii ni kuunganisha mikoa na mikoa kwa kiwango cha lami na kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya ujenzi wa barabara ya kutoka NJiapanda - Mang’ola - Karatu mpaka Lalago ambayo inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu na kumekuwa kuna ukarabati mdogo mdogo unafanyika mara kwa mara ambao unagharimu fedha nyingi.

Sasa kwa nini Wizara isifikirie angalau kuanza kilometa chache chache kwa kiwango cha lami mpaka itakapokamilika? Ahsante.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, naona Mheshimiwa Mbunge anatabasamu anafahamu kwamba Serikali inayo nia thabiti ya kufanya maboresho ya barabara katika maeneo haya na ndiyo maana kuna usanifu umefanyika wa barabara hii, hii bypass hii kutoka Karatu kupita eneo la Mang’ola kwenda Sibiti halafu kuunganisha katika Mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mwanza. Unafahamu kinachoendelea na nimfahamishe tu Mheshimiwa Mbunge hivi wiki iliyopita Mameneja wa TANROADS pamoja na wenzetu ambao pia walikuwa wanasanifu eneo hili wamekuwa na kikao madhubuti kwa maana ya kuliangalia eneo hili kwasababu usanifu ulishakamilika kwa barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini barabara hii tunaitazama sambamba na barabara ya kutoka Karatu- KIlimapunda kuja Mbulu Mjini, kuja Dongobeshi kwenda Haidom, kwenda Sibiti tunakwenda kuungana na hiyo barabara uliyoitaja Mheshimiwa Mbunge. Zote hizi barabara tunaziangalia kwasababu eneo la Mang’ola ni eneo muhimu na lina historia, Wahadzabe wako maeneo haya, lakini pia kuna kilimo cha vitunguu kikubwa katika maeneo haya kwahiyo Serikali imeliona eneo hili kwa maana ya kuwasaidia wananchi maeneo haya ili uchumi uweze kupanda kwa maana hiyo vuta tu subira tumejipanga vizuri, tunazitazama hizi barabara zote ili sasa eneo hili tuweze kulifungua na tuweze kutoa huduma muhimu hii ya barabara. Ahsante sana.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Makutano-Nyamuswa- Sanzate. (a) Je, ni lini barabara ya Makutano Juu - Sanzate itakamilika? (b) Je, Serikali kupitia wataalam wake imeridhika na kiwango cha uwekaji lami katika barabara hii?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, barabara ya kutoka Uvinza kuelekea kwenye Daraja la Kikwete - Malagarasi, barabara hii iliahidiwa kujengwa kwa pesa za kutoka Abu Dhabi. Nataka Serikali iniambie ni lini sasa kipande hiki cha kilometa 48 kitakamilika?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwanza nikupongeze Mheshimiwa Genzabuke kwa sababu unafahamu na unafuatilia sana juu ya barabara hii na ni faraja kwa wakazi wa Kigoma na Tabora na wananchi wengine kwa ujumla kwamba hii barabara muhimu kutoka Tabora kwenda Kigoma sasa maeneo yote pamoja na hili eneo yameshapata mkandarasi kwa maana ya ujenzi, kwa maana hiyo zile taratibu za kimanunuzi zilikuwa zimekamilishwa na kweli tumepata fedha kutoka Abu Dhabi na pia tumeonyesha kwenye bajeti Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba tumeonesha kwamba ujenzi unakwenda kuanza.

Kwa hiyo vuta tu subira zile taratibu za kimanunuzi zinaendelea vizuri na nikuhakikishie muda siyo mrefu utaona mkandarasi yuko site anaendelea na ujenzi katika eneo hili la Uvinza-Malagarasi kilometa 48 ambazo Mheshimiwa Mbunge unafahamu na umeizungumza hapa.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Makutano-Nyamuswa- Sanzate. (a) Je, ni lini barabara ya Makutano Juu - Sanzate itakamilika? (b) Je, Serikali kupitia wataalam wake imeridhika na kiwango cha uwekaji lami katika barabara hii?

Supplementary Question 5

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Kiwanda cha Dangote, lakini yale magari makubwa ya Dangote yanapita barabara ya kutoka Mtwara kuja Mnazi Mmoja kwenda Mtama - Masasi. Ile barabara hali yake haikutengenezwa kubeba magari makubwa ya kiasi kile kwa hiyo hali yake imekuwa mbovu sana. Kila mara unafanyika ukarabati na barabara inaendelea kuwa mbovu. Sasa Serikali inachukua hatua gani kumaliza tatizo hili la ubovu wa hii barabara kwa kila mara?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii imekuwa ikifanyiwa matengenezo lakini Mheshimiwa Nape atakubali kabisa kwamba hii barabara ni ya zamani, hii barabara ina zaidi ya miaka 30 na imekuwa ya muda mrefu na hata ukisoma kibao pale imeandikwa T2 (T Namba 2) na uone hata kwenye usajili wake ni kati ya barabara ambazo ni za zamani sana kwa maana hiyo iko haja sasa ya kufanyia rehabilitation kwa maana ya matengenezo makubwa na wiki iliyopita nilijibu hapa kwamba Serikali tumejipanga kwa ajili ya kuijenga upya barabara hii kutoka Mtwara kuja Mnazi Mmoja na kutoka Mnazi Mmoja kwenda Masasi kwa ufadhili wa World Bank.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Nape vuta subira ule utaratibu wa kawaida wa kifedha na kimanunuzi unaendelea. Tutakwenda kuifumua barabara hii na kuitengeneza kabisa ili iwe mpya kwa hiyo niwahakikishie wananchi wa Mtama, wananchi wa Mtwara, wananchi wa Lindi na Watanzania kwa ujumla kwamba tunakuja kufanya maboresho makubwa ya barabara hii.