Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA (K.n.y. MHE. OMARI A. KIGODA) aliuliza:- Kuna mgogoro mkubwa wa ardhi unaondelea katika Wilaya ya Handeni ambao kama hatua za haraka hazikuchukuliwa unaweza kusababisha ugomvi mkubwa kati ya wananchi. Je, nini tamko la Serikali katika kuzuia tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri juu ya tatizo hili, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la migogoro ya ardhi imekuwa ni changamoto kila eneo katika nchi hii na kama swali la msingi linavyosema kwamba katika Jimbo la Wilaya ya Handeni kuna changamoto ya migogoro ya ardhi. Je, nini mpango mkakati wa Serikali hususan kwa kupima maeneo haya ya ardhi kwa kuainisha maeneo ya wakulima na wafugaji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, changamoto hii ya migogoro ya ardhi iliyopo Handeni inafanana sana na changamoto iliyopo kuna mgogoro baina ya Wilaya ya Kilindi na Wilaya ya Kiteto ambayo imedumu muda mrefu sana. Je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha kwamba inatatua mgogoro huu? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nijibu maswali ya nyongeza mawili ya Mheshimiwa Mbunge wa Kilindi kwa niaba ya Mbunge wa Handeni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna maeneo mengi ambayo hayajapimwa katika Halmashauri zetu na katika Tawala za Mikoa, lakini bahati nzuri Serikali imepunguza sana gharama za upimaji na najua wapo wadau mbalimbali ambao wanaendelea katika maeneo mbalimbali ya kupima maeneo yetu. Mimi naomba nitoe maelekezo kwa viongozi na ushauri kwa wananchi kwamba ukipima eneo lako thamani yako inapanda, unaweza ukakopesheka na ukapata fedha ili kujiendeleza katika eneo lako. Kwa hiyo, wale watu muhimu ambao wanafanya huo upimaji katika maeneo yetu ambao unatambuliwa na viongozi wetu wa vijiji, mitaa, kata, halmashauri na mikoa wawape ushirikiano na wapime maeneo yao ili kuweza kupata hati lakini pia kuweza kupata fedha katika benki mbalimbali katika kuendeleza maeneo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili anauliza suala la mgogoro ambao upo kati ya Kilindi na Kiteto. Yako maeneo mbalimbali ambayo tumepokea malalamiko yao, iko migogoro ambayo ipo katika Wizara ya TAMISEMI ya mipaka, tunaishughulikia na tunafanya hivyo kwa sababu mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili angalau maeneo haya yaweze kutambulika vizuri na uchaguzi usiwe na maneno maneno mengi ya kuhusu mipaka. Yapo mambo ambayo yanahusiana pia na matumizi ya ardhi ambayo yapo kwenye Wizara ya Ardhi, haya pia tunashirikiana na wenzetu wa WIzara ya Ardhi ili kuweza kuyatatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama kuna mgogoro ambao ameutaja hapa sasa tuwasiliane baadae ili tuweze kupata details/taarifa sahihi za eneo hili na ninamhakikishia tutafanya kazi nzuri kuweza kuhakikisha kwamba eneo hili mgogoro unamalizika na watu wetu waendelee kuishi kwa amani na kushirikiana kama ni wafugaji au wakulima, Mheshimiwa Rais tayari ameshatoa maelekezo ili maeneo yatengwe na kuheshimiwa ili watu wetu wafanye kazi bila kugombana kwa kuleta maendeleo katika nchi yetu. Ahsante.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA (K.n.y. MHE. OMARI A. KIGODA) aliuliza:- Kuna mgogoro mkubwa wa ardhi unaondelea katika Wilaya ya Handeni ambao kama hatua za haraka hazikuchukuliwa unaweza kusababisha ugomvi mkubwa kati ya wananchi. Je, nini tamko la Serikali katika kuzuia tatizo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Upo mgogoro wa ardhi wa kimpaka kati ya vijiji vya Msandamuungano, Sikaungu na Gereza la Molo, je, ni lini Serikali itatatua mgogoro huo? Bahati nzuri na Waziri wa Mambo ya Ndani nilishamuona juu ya mgogoro huu.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kutoa hoja hii, lakini iko migogoro mingi kama nilivyosema kwenye swali langu la msingi kwamba yako maeneo ambayo yana matatizo ya mipaka. Tumeshayapokea, tunayafanyia kazi na naomba nimuombe Mheshimiwa Mbunge, baada ya kumaliza kipindi cha maswali na majibu, tukutane ofisini kwa sababu akizungumza mpaka wa kijiji na kijiji hii inakuwa ni kazi ya TAMISEMI inahusiana na mambo ya GN. Ukizungumza habari ya magereza maana yake ni gereza kati ya wananchi lakini pia na Wizara yetu ya Mambo ya Ndani. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tuonane, tuone kama maeneo haya ni miongoni mwa maeneo ambayo tumeyaainisha yenye malalamiko ili tuyafanyie kazi, mgogoro huu utaisha. Kama ni mipaka na mipaka na wenzetu wa Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kwamba maeneo yote ambayo yana migogoro yaishe mapema iwezekanavyo, kama kuna magereza iko pale inafanya kazi nzuri ya watu wetu, kama kuna vijiji ni kazi nzuri ya watu wetu ili malalamiko yasiwepo tuyamalize sisi kama viongozi kwa niaba ya Mheshimiwa Rais. Ahsante.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA (K.n.y. MHE. OMARI A. KIGODA) aliuliza:- Kuna mgogoro mkubwa wa ardhi unaondelea katika Wilaya ya Handeni ambao kama hatua za haraka hazikuchukuliwa unaweza kusababisha ugomvi mkubwa kati ya wananchi. Je, nini tamko la Serikali katika kuzuia tatizo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, upo mgogoro kati ya Manispaa ya Singida pamoja na Halmashauri ya Singida DC katika eneo la Kata ya Muhamo kijiji cha Muhamo, eneo la njiapanda ambapo tuna uongozi wa kitongoji na wakati huo huo eneo hilo hilo lina Mwenyekiti wa Mtaa na Mheshimiwa Naibu Waziri alipofika kwenye ziara Singida aliambiwa na anazo taarifa za mgogoro huu. Je, ni lini mgogoro huu utatatuliwa ili wananchi hao waweze kukaa kwa amani? Ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ni kweli kwamba mimi nilifanya ziara Singida Mjini na Vijijini na katika kikao changu na watumishi Waheshimiwa Madiwani wa eneo lile walitoa taarifa za mgogoro huu na kuna GN pale mbili. Wakati Singida inaanzishwa kuwa mji mdogo, waligawana mali na mipaka ikatengenezwa na GN ikawekwa. Baada ya kuwa Manispaa kulikuwa na GN nyingine. Sasa yapo mambo ambayo nimeshaelekeza wataalam wetu wanafanyia kazi na Mheshimiwa Mbunge anafahamu, tulizungumza mara kadhaa, ninaomba nitoe maelekezo kwamba mgogoro ili tuutatue sisi TAMISEMI ni lazima watu wa Halmashauri ile na Manispaa wafanye kazi yao na watu wa Mkoa wafanye kazi yao halafu watuletee taarifa hapa. Lakini inavyoonekana ni kwamba bado kama kuna mambo ambayo hayajaenda sawa kwa maana ya ngazi ya Wilaya ya Manispaa lakini pia na Mkoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge jambo hili tumeshalichukua kama TAMISEMI, nimeshatoa maelekezo kwa wataalam wetu wapitie zile GN mbili zinaleta mgogoro ili kabla ya uchaguzi wa mwaka 2019 mwaka huu ambao utafanyika Novemba, hili jambo tuwe tumelimaliza ili watu wetu kwa kweli waendelee kufanya kazi kwa kushirikiana vizuri sana kwa sababu Singida ni moja haiwezi kuwa na malalamiko ya hapa na pale ambayo hatuwezi kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili tunalifanyia kazi kabla ya uchaguzi ujao tutakuwa tumelipatia majibu na Mheshimiwa Mbunge Monko waendelee kuwa na amani na watu wako wajue kwamba tutalifanyia kazi kama Serikali na litaisha mapema sana. Ahsante.