Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi kubwa na ngumu sana hasa Mtwara Mjini na maeneo mengine ya nchi yetu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwalipa mishahara kama ilivyo kwa Watendaji wa Vijiji na Mitaa?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza kwa kuwa hawa Wenyeviti wa Serikali za Vijiji na Mitaa wanafanya kazi inayofanana kabisa na hawa Watendaji wa Vijiji na Mitaa, lakini Serikali inawalipa Watendaji tu. Je, Serikali haioni kwamba inawabagua Wenyeviti hawa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa Halmashauri nyingi hivi sasa mapato yake yamechukuliwa na Serikali ikiwemo kodi ya majengo pale Mtwara Mjini na nchi nzima kiujumla ambayo ilikuwa inasaidia sana kupata makusanya ili kuweza kuwalipa posho kwa mujibu wa sheria hawa Wenyeviti wa Vijiji Serikali ama Vijiji vingi ama Halmashauri nyingi zinashindwa kutoa hata posho ya shilingi 20,000 kwasababu haina vyanzo vya mapato ikiwemo kodi ya majengo.

Je, Serikali ni lini itarudisha kodi hii ili halmashauri nyingi ziweze kukusanya na kuwapa posho Wenyeviti wa Mitaa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge swali lake la kwanza anasema Serikali inawabagua Wenyeviti kwa sababu Watendaji wanalipwa. Suala hili siyo kweli kwa sababu wanapokuwa wanaomba hizi kazi utaratibu unatofautiana, Wenyeviti wa Mitaa wanachaguliwa na wananchi wao na wale Watendaji wanaomba kazi na wanaajiriwa na Serikali na nimeeleza kwenye jibu la msingi ni kwamba malipo ya Wenyeviti wa Mitaa na Wenyeviti wa Vijiji na Wajumbe wao inategemea makusanyo ya mapato ya ndani na tumeshapitisha bajeti, hatujazuia Halmashauri kuwa na uwezo wa kuwalipa Wenyeviti tukazuia, ndiyo maana tukasema tunatambua kazi nzuri inayofanywa kwa sasa utaratibu uliopo Halmashauri yenye uwezo italipa posho kulingana na uwezo ule na Wenyeviti wa Mitaa waendelee kutuvumilia uwezo ukiruhusu hatujakataa kuwalipa ila uwezo ukiruhusu watalipwa.

Kwa hiyo, Halmashauri zetu kama watabuni vyanzo vingine vya mapato wakipata uwezo wa kuwalipa watalipa Serikali haijazuia kabisa. Lakini hakuna ubaguzi na Wenyeviti wanajua kwamba hawa ni waajiriwa, wanaombwa na vyeti, wana-qualify na hawa ni watumishi wa wananchi ambao wamechaguliwa na wananchi wale na wanafanyakazi nzuri sana kama tulivyosema.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anazungumza kurudisha kodi ya majengo, kwa hiyo, kuwezesha Serikali zetu kwenye Halmashauri kuwalipa Wenyeviti wa Mitaa.

Mheshimiwa Spika, baada ya kodi hii kuchukuliwa kodi ya majengo pamoja na mabango pamoja na kodi zingine hii fedha inachukuliwa yote kwa ujumla wake nchi nzima inapelekwa kwenye kapu kuu la Serikali, kwa hiyo, hata miradi ya kimkakati barabara zinazojengwa, miradi ya maji, mishahara ya watumishi hii ni fedha ambayo inatumika kule, kwa hiyo siyo kwamba haina kazi. Lakini tumeelekeza Halmashauri na tumewaambia wabuni miradi mbalimbali ya kimkakati na Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Fedha tunawezesha kuanzisha miradi mikubwa mikubwa na Mtwara nimekuja pale kuna miradi mikubwa inaanzishwa.

Kwa hiyo ukipata uwezo kama huu ukapata fedha katika eneo lile na vyanzo vingine ukibuni bila kunyanyasa wananchi wataongezewa posho zao. Kwa sasa Halmashauri itaendelea kulipa kwa kadri itakavyoweza na pamoja kazi nzuri inayofanyika hatujazuia Halmashauri kulipa kulingana na uwezo wake.

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi kubwa na ngumu sana hasa Mtwara Mjini na maeneo mengine ya nchi yetu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwalipa mishahara kama ilivyo kwa Watendaji wa Vijiji na Mitaa?

Supplementary Question 2

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuwa Halmashauri nyingi nchini zinalipa hiyo posho ya Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji kati ya shilingi 5,000 mpaka shilingi 10,000. Je, Serikali haioni sasa kwamba imefika wakati ambapo wanapaswa kutoa maelekezo viwango vya posho hizo kupanda na vikawa vinafanana kwa Halmashauri zote nchini?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Moshi Mjini ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Halmashauri Mstaafu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hoja ya nyongeza ya posho ya Wenyeviti wa Mitaa inategemea na uwezo wa Halmashauri, mimi nafahamu natoka katika Halmashauri ya Ilala. Ilala wanalipa posho kwa mwezi shilingi 100,000 Wenyeviti wa Mitaa na wanalipa kila baada ya miezi mitatu, mitatu, lakini hiyo inategemea na mapato makubwa ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Kinondoni na Temeke.

Kwa hiyo, kama Moshi na maeneo mengine yana uwezo kama nilivyosema hatujazuia kabisa, fedha inayokusanywa kwenye Halmashauri kuna maelekezo yametoka, kwa mfano asilimia 10 itaenda kwenye vijana, akinamama na watu wenye ulemavu. Fedha zingine kuna maelekezo mengine yametoka, lakini inayobaki fedha ya maendeleo itatengwa, lakini inapohusika na uendeshaji kama ni Halmashauri ngazi ya Kata, Vijiji na Vitongoji inahusika. Kwa hiyo Halmashauri yenye uwezo itaendelea kulipa posho kubwa kulingana na uwezo wake. H lo linaruhusiwa hatujazuia. Ahsante.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi kubwa na ngumu sana hasa Mtwara Mjini na maeneo mengine ya nchi yetu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwalipa mishahara kama ilivyo kwa Watendaji wa Vijiji na Mitaa?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri mimi nimekuwa niliwahi kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya wakati ule Halmashauri zote vyanzo vyote vilikuwa pale, lakini kwa kuwa Serikali imechukua vyanzo vyote na tulikubaliana mpeleke ruzuku ya kutosha kwenye Halmashauri ili viongozi hawa Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Madiwani walipwe. Kwa nini hamuongezi ruzuku kwenye Halmashauri za Wilaya?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Senator Mzee Lubeleje kama ifuatavyo:-

Ni kweli ni Mwenyekiti wa Halmashauri Mstaafu na alivyozungumza ni kweli wakati huo, lakini sasa hivi ni kweli kwamba baadhi ya vyanzo vimechukuliwa ili viweze kuratibu kwa sababu kuna Halmashauri ambazo zilikuwa na majengo mengi na mabango mengi na walikuwa wanaweza kupata fedha nyingi kwa wakati mmoja tofauti na maeneo mengine, Serikali imetumia busara kwamba fedha hizi zikusanywe centrally, lakini zipelekwe kwenye miradi ya wananchi ambayo ni nchi nzima hata Halmashauri ambayo ilikuwa na mapato machache ya mabango au na majengo inapata miradi mikubwa ya kimkakati ili maendeleo yaende katika msambao unaofanana katika nchi yetu.

Lakini hoja yake ya kuongeza posho na kupeleke ruzuku, miradi mingi ya ruzuku ilikuwa inategemea pia na wafadhili kutoka nje, sasa hivi ndiyo tukasema fedha zipo za kuanzisha miradi ya kimkakati na maelekezo yameenda kwenye Mikoa yote na Halmashauri zote. Ni wataalamu wa Halmashauri yako Mheshimiwa Lubeleje wanakaa, wanaandaa andiko, wanakaa na watu wa Wizara za Fedha na TAMISEMI, miradi inapelekwa ndiyo maana nikasema ukipata miradi ya kimkakati, masoko, stand kubwa kubwa zile mapato yataongezeka na kwa hiyo Halmashauri itaweza kulipa posho za Wenyeviti wa Mitaa.

Mheshimiwa Spika, niseme maneno ya nyongeza wenyeviti wa mitaa tunatambua kazi kubwa sana ambayo wanafanya na ndiyo maana miradi yote mikubwa ya kimkakati ipo kule wanaisimamia kwa kushirikiana na viongozi wa Kata na Madiwani na wengine, uwezo wetu wa Serikali ukiwa mkubwa tungeweza kulipa mishahara na posho kubwa kubwa, kwa sasa hatujafikia huko.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Wenyeviti wa Mitaa waendelee kufanya kazi kwa sababu wameaminiwa na watu wao, uwezo wa Serikali …, lakini Halmashauri zetu wajipange kila kinachopatikana wasiwasahau Wenyeviti wa Mitaa, wawawezeshe ili waweze kufanya kazi zao vizuri. Ahsante.