Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHID A. AJALI) aliuliza:- (a) Je, kipimo halisi cha barabara kwa barabara kuu ya lami ni kipi? (b) Je, upana kwenye miji ipitayo barabara unafanana na eneo ambalo halina makazi? (c) Kama upana haufanani kwenye miji na eneo ambalo halina makazi, je, nini kipimo halisi?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kama ambavyo ameeleza kwamba maeneo yenye makazi wamepanua barabara kwa ajili ya kuangalia usalama wa raia na sasa hivi tunaweka zebra na matuta, lakini kumejitokeza matumizi mabaya ya zebra kwa sababu wakati mwingine unakuta waenda kwa migu ndio wanapewa muda mrefu sana kuliko hata magari na hivyo kusababisha msongamano.

Je, kwa nini Serikali isiweke taa za kuruhusu waenda kwa miguu, ili wao wawe wanapita pale kwa zamu badala ya kuwa wanapita wakati wote?

Mheshimiwa Spika, pili, matuta nayo imethibitika kwamba, kwa kuweka matuta mengi barabarani na matumizi ya madereva wetu imesababisha matatizo ya mgongo, hasa kwa wanaotumia magari.

Je, hakuna utaratibu mwingine wa kuweka usalama kwa waenda kwa miguu zaidi ya kuweka matuta barabarani?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge na kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Hawa Ghasia kwa namna anavyofuatilia mambo mbalimbali ya maendeleo. Na niseme kuhusu matumizi ya zebra na matuta ni kwamba ni kweli kumekuwepo na changamoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini utakubaliana na mimi kwamba tunaweka zebra na matuta ni kwa ajili ya kuhakikiha wananchi wetu wanakuwa salama kutokana na baadhi ya watumiaji wa barabara kuwa wanatumia barabara zetu bila kuzingatia utaratibu na masharti yaliyowekwa ili kuwafanya wananchi wetu waweko salama. Kwa hiyo, nilikuwa napenda Bunge lako litambue kwamba uwekaji wa zebra na matuta haya ambayo saa nyingine yameonekana kuwa ni usumbufu, lakini ni nia njema ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanabaki kuwa salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata hivyo Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi kwa siku za hivi karibuni tumejipanga vizuri maeneo mengi nchini tunaendelea kuweka taa. Kwa hiyo, iko mipango ambayo imefanyika na Halmashauri zetu, kuna taa nyingine wanaweka kupitia halmashuri zetu za wilaya na miji tunaendela kuweka taa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge hilo nimelichukua kwa maana ya kuweka msukumo mkubwa zaidi ili maeneo mengi tuweke taa kutoa usumbufu ambao unajitokeza, ili matumizi ya barabara yaweze kwenda sawasawa na watumiaji wa magari pia waweze kwenda vema.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niseme kuhusu matuta, kipindi sio kirefu sana nilijibu hapa swali kuhusu matuta kwamba, sisi Serikali tumeendelea kuyapunguza matuta maeneo mengi. Tuliweka matuta kwa sababu ya usalama wa wananchi, lakini tumegundua baada ya kuweka matuta elimu imeendelea kuwa kubwa kwa wananchi wetu wanaotumia barabara pale tunapothibitisha kwamba sasa eneo fulani hali ya hatari ya wananchi imepungua matuta hayo tumeyaondoa. Tumeondoa matuta mengi sana kwa hiyo, Mheshimiwa Hawa Ghasia kubaliana na mimi hilo, lakini kama kuna maeneo ambayo ni mahususi tutaona kuna matuta yanaleta shida mtufahamishe na sisi Serikali tutakuwa tayari kwenda kufanya marekebisho, ili kutoa usumbufu wa watumiaji wa barabara hususan wanaotumia magari.

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHID A. AJALI) aliuliza:- (a) Je, kipimo halisi cha barabara kwa barabara kuu ya lami ni kipi? (b) Je, upana kwenye miji ipitayo barabara unafanana na eneo ambalo halina makazi? (c) Kama upana haufanani kwenye miji na eneo ambalo halina makazi, je, nini kipimo halisi?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna baadhi ya maeneo tunaona kwamba kuna upanuzi wa barabara nikitolea mfano barabara ya Dodoma mpaka Morogoro, maeneo ya Gairo na maeneo ya Dumila. Je, ni hatua zipi zinazochukuliwa sasa kwa wale wakandarasi ambao kazi zao hazikukidhi viwango?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunaendelea kupanua barabara maeneo mbalimbali. Kama nilivyozungumza jana hapa ni kwamba asilimia 90 ya fedha zinazokwenda kwenye ujenzi wa barabara ni kwa ajili ya matengenezo, kwa hiyo, zoezi linaloendelea nchi nzima kufanya maboresho ya barabara ni la kawaida kwa sababu barabara zinavyotumika zinachakaa na saa nyingine kutokana na umri, kutokana na hali ya hewa na mambo mbalimbali, kwa hiyo, matengenezo hayo ni muhimu yanaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niseme tu kwamba upanuzi huu wa barabara au kazi zinazoendelea barabarani ni kwa mujibu wa mikataba ambayo ipo na mikataba imezingatia specifications za kitaalam na mikataba pia imeweka masharti ya pande zote mbili, upande wa sisi Serikali, lakini upande wa mkandarasi na ziko hatua ambazo zinachukuliwa, tunacho chombo ambacho kinawasimamia wakandarasi, tuna Contractors Registration Board na lakini pia kuna ERB yaani Engineers Registration Board ambayo hawa wanafuatilia miradi mbalimbali kukagua kuona kama shughuli hizi zinaenda vizuri, lakini kwa kuzingatia pia mikataba.

Mheshimiwa Naibu Spika, wapo idadi ya makandarasi ambao wamechukuliwa hatua, wapo ambao amesimamishwa kwa muda, wapo ambao wamefutiwa usajili wao na tutaendelea kuchukua hatua kwa mtu ambaye anakiuka taratibu za ujenzi.

Kwa hiyo, nikuhakikishie tu na Bunge lako kwamba, sisi Serikali tuko makini kuhakikisha kwamba kazi zinafanyika kufuatana na mikataba iliyokuwepo, kufuatana na taratibu zilizokuwepo, ili kuhakikisha kwamba kazi ambazo tumeziweka kwa ajili ya ukarabati au ujenzi zinakamilika, lengo ni wananchi waweze kupata huduma nzuri na kwa haraka inavyowezekana.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHID A. AJALI) aliuliza:- (a) Je, kipimo halisi cha barabara kwa barabara kuu ya lami ni kipi? (b) Je, upana kwenye miji ipitayo barabara unafanana na eneo ambalo halina makazi? (c) Kama upana haufanani kwenye miji na eneo ambalo halina makazi, je, nini kipimo halisi?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, umepita Barabara ya Mbulu kwa upande wa Mashariki na Mheshimiwa Naibu Waziri amepita barabara hiyo ya Mbulu kwa upande wa Magharibi. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utuambie sasa na uwaambie wananchi wa Mbulu, barabara ile ya Mbulu – Haydom – Mbulu inajengwa lini kwa kiwango cha lami?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ziko changamoto katika huu ushoroba kwa maana ya hii barabara kuu ambayo anaizungumza Mheshimiwa Mbunge kwa maana itatuunganisha kutoka Karatu, tutakuja Mbulu, tunakwenda Dongobesh, tunakwenda Haydom, tunapita kule Sibiti ambako daraja kubwa limekamilika halafu tutakwenda kwenye Mikoa ile ya Shinyanga, Mkoa wa Simiyu, Mwanza, hii barabara muhimu na niseme tu na kuwahakikshia wananchi wa Mbulu na majirani zao ni kwamba, tunaanza sasa ujenzi kwa sababu ule usanifu ulishakamilika na katika bajeti hi mliyotupitishia tumetenga kuanza ujenzi wa kiwango cha lami wa kilometa 50 kutoka Mbulu kuja Dongobesh na tutaendelea hivyo hivyo kadri tutapopata fedha mpaka barabara hii muhimu iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante sana.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y. MHE. RASHID A. AJALI) aliuliza:- (a) Je, kipimo halisi cha barabara kwa barabara kuu ya lami ni kipi? (b) Je, upana kwenye miji ipitayo barabara unafanana na eneo ambalo halina makazi? (c) Kama upana haufanani kwenye miji na eneo ambalo halina makazi, je, nini kipimo halisi?

Supplementary Question 4

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika Tunduma ni mpakani na kuna msongamano mkubwa sana wa malori yanayovuka mpaka wa Tunduma kuelekea Zambia, lakini pia wananchi wamekuwa wakipata shida sana ya kuweza kutumia barabara moja ambayo iko kwenye mji wetu wa Tunduma, lakini kuna bypass ya barabara inayotokea Mpemba kuelekea Tunduma Mjini kilometa 12 na Mheshimiwa Naibu Waziri alipita kuja kuingalia barabara ile na akatuahidi kwamba barabara ile ingeweza kujengwa katika mwaka huu wa fedha.

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ile ili kupunguza msongamano na kuwapa unafuu Wananchi wa kuendelea kutumia barabara yetu ya Mji wa Tunduma? Ahsante sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mji wa Tunduma unakua kwa kasi na ni ukweli inahitajika maboresho mbalimbali ya miundombinu katika eneo hili na Serikali inachukua hatua nyingi kupaboresha sehemu hii ya Tunduma kwa sababu hata ukifika pale utaona magari ni mengi sana na sisi tumejipanga pia kuboresha kwenye kituo chetu hiko cha Mpemba pale, tukatakuwa na ujenzi wa kituo kile ambacho kitashughulikia mambo mengi, Mheshimiwa Mwakajoka anafahamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Mwakajoka hapo amechomekea kidogo kusema nilitoa ahadi ya kujenga kiwango cha lami katika mwaka huu wa fedha, siyo kweli. Nilichokisema ni kwamba Serikali inayo mpango wa kufanya maboresho maeneo haya ikiwepo kuangalia zoezi zima la ujenzi wa bypass ili kukwepesha adha ambayo watumiaji wa barabara wanaipata wakipita katika Mji wa Tunduma hususan wanaokwenda maeneo ya Rukwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa kweli tulifanya mazungumzo na mimi pia niliwatahadharisha uongozi uliopo pale ili tuanze kuangalia mipango kwa mapana, kwa sababu mji ule unakua sana. Utaona ile hifadhi ya magari (parking) muda siyo mrefu zitafika mpaka kwenye Mji wa Mbozi, kwa hiyo, ukuaji ni mkubwa sana. Kwa hiyo, kwa upande wa Serikali sisi tunaona kwamba mipango yetu lazima tuiweke vizuri ili siku za usoni kulingana na ule ukuaji wa mji huu kwamba huduma zile muhimu zinapatikana.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mwakajoka nakuomba uvute subira tu, wewe unafahamu umejaribu kuchomeka hapa lakini unafahamu kwamba umuhimu wa hii bypass lakini na sisi tumeichukua hiyo tunaendelea kuiweka kwenye mipango yetu ili kwa haraka tuje tuweke huduma hii ya barabara kwa maana ya bypass. Wewe vuta subira tu na ikikupendeza ukipata muda uje tuzungumze tuone kwenye strategic plan yetu tumeiweka namna gani ili hata ukipeleka information kwa wananchi wetu usiwaambie kwamba tutaanza kujenga mara moja, lakini uwaambie kutokana na hali ambayo ipo, kwenye utaratibu wetu ambao tumejiwekea ambao ni mzuri tu, kwa kweli tumewajali sana wananchi wa Tunduma.