Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Nyumba za makazi pembezoni mwa reli Wilayani Muheza zimewekewa alama ya ‘X’ zikisubiri kubomolewa kwa kigezo cha kujenga kwenye eneo la reli wakati walipewa maeneo hayo kIhalali na Serikali. Je, ni nini hatma ya wananchi hao ambao wanaishi kwa mashaka?

Supplementary Question 1

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ni dhahiri Mheshimiwa Waziri anafahamu wakazi hawa wananchi hawa wa maeneo ya Kata ya Genge, Kata ya Tanganyika, Kata ya Tingeni na Kata ya Bwembwera wamekuwepo katika maeneo haya zaidi ya miaka 50.

Naomba nifahamu kwa kuwa Serikali ilikuwa inaendelea kupeleka huduma na Serikali imesajili mpaka baadhi ya vijiji ambavyo vina maeneo yaliyopitiwa na reli ambayo sasa hivi imeekewa ‘X’. Je, Serikali iko tayari kuwalipa fidia wananchi wale kwa kuwa wao ndio walibariki wananchi kuendelea kuishi pale zaidi ya miaka 50? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Wilaya ya Muheza kunaendelea urasimishaji wa makazi na katika maeneo na nyumba za watu ambao wana ‘X’ wamewekewa ‘X’ wanaambiwa na wao walipe kwa ajili ya urasimishaji. Nilitaka kufahamu Mheshimiwa Waziri yuko tayari kusitisha zoezi hili ili mpaka wananchi wale wenye nyumba za ‘X’ wapatiwe ufumbuzi? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme kwamba wananchi wanastahili kupewa ile huduma muhimu ambazo Serikali inapaswa kuwapa wananchi inastahili wazipate kwamba hakuna sababu ya kuwaadhibu wananchi kutokana na makosa labda ambayo yalitokana na watendaji. Kwa hiyo kupata huduma wananchi ni haki yao, lakini niseme tu kwamba kuhusu fidia, zoezi la kulipa fidia linafanyika kwa mujibu wa sheria, tutaangalia Sheria ya Ardhi, Sheria ya Ardhi ya Vijiji ndio inatumika kulipa fidia kwa wananchi, kwa maana hiyo Mheshimiwa Mbunge ukubaliane na mimi kwamba fidia inalipwa kutokana na sheria na taratibu ambazo zipo, kwa wale wanastahili kulipwa fidia Serikali inaendelea kufanya hivyo kwa sababu ni haki yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusu urasimishaji wa maeneo ambao zoezi linaendelea niseme tu kwamba sio vyema kurasimisha maeneo ambayo sio halali na mimi nafahamu wataalam waliopo kwenye maeneo haya watarasimisha maeneo tu ambayo ni halali kurasimisha na niseme tu kwamba Serikali itawachukulia hatua watumishi ambao watarasimisha maeneo ambayo hayastahili kurasmishwa kwa sababu ni kuvunja sheria, kwa maana hiyo wale watu waliowekewa ‘X’ kwa maana ya kupisha niwasihi tu wapishe maeneo haya kwa sababu ni maeneo ya reli na sio vyema kuendelea kuendeleza maeneo haya, kwa sababu tutaendelea kupata hasara bila sababu.

Kwa maana hiyo, Mheshimiwa Mbunge tusaidiane tu kwamba wananchi wa maeneo haya ya Muheza uwashauri kwa maeneo ambayo unaona kabisa kiuhalali yako maeneo ya reli wapishe maeneo haya na kama kuna tatizo lilijitokeza kutokana na utendaji basi Serikali itachukua hatua kutokana na namna ya hali ilivyokuwa. Ahsante.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa. Nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, nilipenda kutoa nyongeza tu kwenye swali la pili la Mheshimiwa Yosepher.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba lengo na dhamira ya Serikali ni kuwawezesha Wananchi. Sasa unapokuta kwamba yuko kwenye eneo ambalo halitakiwi lifanyiwe urasimishaji maana yake ameingia kwenye eneo ambalo haliko kwenye mpango. Sasa na unaposema kwamba kuzuia watu wengine mpaka ufumbuzi upatikane, wale watu tayari wako ndani ya maeneo ambayo hayaruhusiwi kujengwa kwa sababu ni kwa kazi nyingine ambayo imewekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi niombe tu Halmashauri zetu wawe makini katika kuangalia namna ambavyo vipimo vya barabara na reli ambavyo vimekaa kiasi kwamba watu wasiingie kwenye yale maeneo. Na sasa hivi Wizara imeanza kuweka mpango wa upimaji katika maeneo yanayopitiwa na reli. Kwa hiyo, ni vizuri wakazingatia yale masharti ambayo tunayatoa ili baadae wasije wakajikuta wameingia kwenye eneo ambalo haliruhusiwi. Ahsante.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Nyumba za makazi pembezoni mwa reli Wilayani Muheza zimewekewa alama ya ‘X’ zikisubiri kubomolewa kwa kigezo cha kujenga kwenye eneo la reli wakati walipewa maeneo hayo kIhalali na Serikali. Je, ni nini hatma ya wananchi hao ambao wanaishi kwa mashaka?

Supplementary Question 2

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya kutoka Masasi hadi Newala Serikali imekwishadhamiria kuijenga kwa kiwango cha lami na kwamba inatarajia kutangazwa zabuni mwezi wa saba.

Je, wananchi wa Kijiji cha Mpeta, Chiungutwa, Nagaga, Mkangaula pamoja na Msanga ambao walipaswa kulipwa fidia ni lini Serikali itawalipa fidia ili kupisha ujnzi huo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni utaratibu wa Serikali kulipa fidia kabla ya kuanza ujenzi na kwa kuwa utaratibu wa kuanza ujenzi wa barabara hii muhimu, barabara ya uchumi hii kutoka Mtwara – Masasi – Newala utaanza hivi karibuni, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge na wananchi hawa wa maeneo ya Mpeta, Chiungutwa, Kangaula na Lulindi kwa ujumla kwamba watalipwa fedha zao mapema, ili kupisha ujenzi kuanza kwa maana hiyo kwa sababu, tutaanza hivi karibuni ina maana kwamba ni hivi karibuni watalipwa kabla ujenzi haujaanza.

Name

Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Nyumba za makazi pembezoni mwa reli Wilayani Muheza zimewekewa alama ya ‘X’ zikisubiri kubomolewa kwa kigezo cha kujenga kwenye eneo la reli wakati walipewa maeneo hayo kIhalali na Serikali. Je, ni nini hatma ya wananchi hao ambao wanaishi kwa mashaka?

Supplementary Question 3

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Shirika la Reli la Taifa linamiliki hayo maeneo kihalali, lakini kwa kuwa Wizara ya Ardhi na Halmashauri za Wilaya mbalimbali zimetoa hati za umiliki wa ardhi katika maeneo hayo hayo ambayo ni maeneo ya reli; kwa mfano kule Moshi Kiwanda cha Serengeti kiko chini ya eneo ambalo linamilikiwa na reli.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuondoa msuguano uliopo kati ya hati halali zilizotolewa na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi na zile hati ambazo ziko chini ya Shirika la Reli la Taifa ili wananchi hawa na maeneo haya yaweze kuendelezwa kwa haraka iwezekanavyo? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Kubenea kwa kutambua kwamba maeneo haya yanamilikiwa kihalali na Shirika la Reli na ndio maana niendelee kumsihi Mheshimiwa Mbunge Kubenea na Waheshimiwa Wabunge tuendelee kuwasaidia wananchi wetu kwa sababu maeneo ambayo unatambua ni halali na kama inatokea makosa ambayo ni ya kiuadilifu, wananchi wanapewa maeneo ambayo ni halali kwa ajili ya miundombinu ya reli kwamba sio vema. Kwa hiyo, tuwasaidie wananchi wetu na tuchukue hatua mnapema, ili Wananchi wasidumbukie kwenye shida ambayo inajitokeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, na niseme tu hakuna msuguano, hakuna msuguano kwa sababu kama maeneo haya ni halali kwa ajili ya shirika la reli msuguano haupo, isipokuwa ni ile hali tu ya utovu wa nidhamu uliotokea kusababisha baadhi ya wananchi wachache labda wakamilikishwa maeneo sio kihalali. Kwa maana hiyo niendelee kutoa wito tu kwa watumishi wote wa umma kwamba tunapotekeleza majukumu yetu tutekeleze kwa kuzingatia sheria, ili tusiendelee kuwasumbua wananchi wetu kama tutakuwa tumevunja sheria.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Nyumba za makazi pembezoni mwa reli Wilayani Muheza zimewekewa alama ya ‘X’ zikisubiri kubomolewa kwa kigezo cha kujenga kwenye eneo la reli wakati walipewa maeneo hayo kIhalali na Serikali. Je, ni nini hatma ya wananchi hao ambao wanaishi kwa mashaka?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo Muheza linafanana kabisa na tatizo lililoko pale Kurasini ambapo nyumba zilizokuwa za TRC zilikabidhiwa kwa TBA na TBA iliwauzia wapangaji waliokuwa katika nyumba hizo, lakini sasa hivi baada ya TRC kuwa vizuri imeenda tena kuzidai nyumba zile na kuwavunjia vibanda wale watu ambao wamenunua nyumba hizo.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inakwenda kutatua tatizo hili kwa kuwataka TBA kuwapa hati wale wote walionunua nyumba hizo?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, uko utaratibu wa kuwalipa fidia wananchi pale ambapo wanapopisha maeneo kwa ajili ya maendeleo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mtolea nikuhakikishie tu kama wananchi hawa walipewa hizi nyumba kihalali na wanastahili kulipwa, ni kwamba utaratibu uleule wa kupisha maeneo kwa ajili ya maendeleo utatumika kwa ajili ya kuwatazama hapo, lakini kwa sababu suala hili umelileta hapa naomba nilichukue kama mahususi ili tuangalie nini kilitokea na ili haki iweze kutendeka kwa wananchi hawa. Ahsante sana.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. YOSEPHER F. KOMBA aliuliza:- Nyumba za makazi pembezoni mwa reli Wilayani Muheza zimewekewa alama ya ‘X’ zikisubiri kubomolewa kwa kigezo cha kujenga kwenye eneo la reli wakati walipewa maeneo hayo kIhalali na Serikali. Je, ni nini hatma ya wananchi hao ambao wanaishi kwa mashaka?

Supplementary Question 5

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Serikali kwa kufanya ukarabati wa reli Tanga - Korogwe - Mombo na Mazinde na kuendelea. Nilikuwa nataka kujua kwenye maeneo yale ya reli kuna nyumba za Serikali ambazo zilikuwa zimejengwa kwa ajili ya watumishi ambao walikuwa wanaishi katika maeneo yale. Sasa katika ukarabati huu wa reli, je, mko tayari sasa kuzikarabati nyumba zile ili kusudi wale wafanyakazi waendelee kukaa kwenye zile nyumba kwa kusaidia kulinda mataruma yale yasiendelee kuibiwa?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza pongezi za Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Serikali nazipokea, lakini na nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali imedhamiria kufanya maboresho makubwa katika mtandao wa reli ikiwepo maeneo haya ambayo umeyataja na kwa sababu hiyo, hivi karibuni tu Bunge lako limetupitishia fedha kwa ajili ya kufanya pia maendeleo ya mtandao mzima wa reli.

Nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, hizi nyumba ambazo zilikuwa za watumishi unazizitaja tutazifanyia ukarabati na kwa sababu, tumedhamiria kufanya maboresho tutaboresha mtandao wa reli pamoja na huduma nyingine ambazo zinahusiana na huduma hii ya reli. Ahsante sana.