Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM aliuliza:- Mwaka 2019 kutafanyika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria. Je, Serikali ina mkakati gani unaoendelea katika maandalizi ya mchakato wa uchaguzi huo?

Supplementary Question 1

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, nina maswali mawili ya nyongeza kama yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza; kumekuwepo na hofu na malalamiko makubwa juu ya mbinu chafu ambazo zimeweza kujitokeza hivi karibuni wakati wa urejeshaji wa fomu kwa vyama vya upinzani kuambiwa kwamba viongozi hao/wagombea hao wa upinzani hawana sifa jambo ambalo limekuwa likileta hisia mbaya kwamba Chama cha Mapinduzi kinataka ibaki peke yake katika uchaguzi.

Je, huoni Mheshimiwa Waziri mbinu hii chafu ya kusema wagombea wa upinzani hawana sifa kwa hila na ujanja kutaweza kupelekea uchaguzi huu usiwe wa haki na huru na kweli atakayeshinda mtatangaza? La kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; kumekuwa na taratibu ambazo zimekuwa zikiendelea hivi sasa katika baadhi ya maeneo kuanza kufanya kampeni kwa njia ya ujanja ujanja. Mfano, pale Morogoro kumekuwa na uzinduzi wa Morogoro ya Kijani huku wakieleza kwamba tunaelekea chaguzi za Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji wakati uchaguzi uko Oktoba.

Je, ni kwa nini basi matangazo haya, mabango haya na utaratibu huu unaofanywa kwa upande mmoja tu wa Chama Tawala usidhibitiwe mapema ili kutuondoa na matatizo ambayo yanaweza kujitokeza? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwanza hakuna mbinu chafu. Utaratibu wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa utatangazwa tarehe na mwenye mamlaka, uwekwe utaratibu wa kujiandikisha kwa muda utakaotajwa, yatabandikwa majina kwenye mbao za matangazo kila watu watahakiki wakazi katika mtaa husika na kijiji au kitongoji, wataenda kwenye kampeni sawa kwenye vyama vyote na uchaguzi utafika watachaguliwa ila kwa sababu Mheshimiwa Masoud anajua kwamba watakaochaguliwa wengi wagombea wa Chama cha Mapinduzi hiyo ndiyo hofu uliyonayo kwa sababu kazi nzuri ya Chama cha Mapinduzi ambayo imefanywa chini ya Dkt. John Pombe Magufuli, miradi mikubwa ya kimkakati, Rais ambae ni wa mfano katika Afrika na dunia anayekutana na makundi mbalimbali, uchaguzi ukitangazwa uwezekano mkubwa wa kupata asilimia 98 wagombea wa Chama cha Mapinduzi ndiyo huo ambao unakutisha, lakini tutakwenda kwenye uchaguzi, watu wako wajiandae vizuri, kanuni zipo, kuna Kamati za Rufaa, kama hujaridhia unaweza ukaenda Mahakamani ukapata haki yako Mheshimiwa Mbunge usiwe na hofu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge anauliza kuanza kufanya kampeni na CCM ya Kijani. Hapa ni mipango ya Chama cha Mapinduzi. Chama hiki ni Chama Tawala, kinakagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi na kujipanga na uchaguzi ujao. Chama makini, chama kikongwe lazima kiwe na mbinu nyingi kila wakati na ndizo zonachanganya watu akiwepo Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika na CCM wanaita wanachama wao, wanakagua kadi za uanachama, wanapata taarifa ya uchaguzi, usiwe na hofu na hata hivyo ukiangalia CHADEMA wale CHADEMA ni msingi walikuwa Katavi, wameenda Rukwa, wapo kila mahali tuna taarifa hizo na wanafanyakazi.

Sasa ndugu yangu Mheshimiwa kama wewe hujajipanga usiwaonee nongwa wenzako. CCM ipo kazini, CCM ya Kijani itaendelea kila mahali hata mimi Bunge likiaihirishwa nifanya Ukonga na nakushauri uende kwenye chama chako andaa mkakati. Watanzania wake mkao tayari, Serikali ya Chama cha Mapinduzi iko makini imejiandaa, sheria zitafuatwa, kanuni zitafuatwa na sheria zipo. Kama hujaridhika mahali popote uko aggrieved unakeenda Mahakamani lakini uchaguzi huu utakuwa uchaguzi mzuri sana, hofu yako nikutoe, wananchi ndiyo watakaochangua, wana macho wanaona, wana masikio wanasikia, CCM ndiyo habari ya mjini. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM aliuliza:- Mwaka 2019 kutafanyika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria. Je, Serikali ina mkakati gani unaoendelea katika maandalizi ya mchakato wa uchaguzi huo?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Watendaji wa Vijiji na Mitaa ni muhimu sana katika uchaguzi huu, lakini kuna vijiji vingi havina watendaji. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kujaza nafasi hizi kabla ya uchaguzi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni muhimu unasimamiwa na watendaji wa ngazi za chini wale Watendaji wa Vijiji na Mitaa, Watendaji wa Kata na mpaka ngazi ya Halmashauri na ni kweli kwamba kuna baadhi ya maeneo ambayo hayana watendaji hawa, lakini nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, uko utaratibu wa Kiserikali bahati nzuri hawa ni watumishi wa Serikali. Tunaendelea kuchukua hatua kuajiri na kuziba mapengo. Ikitokea uchaguzi unafika eneo fulani au kijiji hakuna Mtendaji, wale watumishi wa Serikali wakiwepo watumishi wa afya, walimu wanapewa jukumu watasimamia kwa sababu wote wanaitwa, wanapewa semina na mafunzo na wanaapishwa kiapo cha utii, halafu wanafanyakazi za Kiserikali na wakimaliza kazi hii wanarudi kwenye majukumu yao ya kawaida. Ahsante.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM aliuliza:- Mwaka 2019 kutafanyika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria. Je, Serikali ina mkakati gani unaoendelea katika maandalizi ya mchakato wa uchaguzi huo?

Supplementary Question 3

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, baadhi ya matukio yaliyojitokeza katika baadhi ya chaguzi za marudio ni lile tukio la Wakurugenzi kujificha pale inapotokea wagombea wa vyama vya upinzani wanarejesha fomu na hivyo kuwakosesha sifa ya kuwa wagombea.

Je, Mheshimiwa Waziri amesema Chama cha Mapinduzi kina mbinu nyingi, hii ni moja kati ya mbinu mnayoitumia ili kuhalalisha ushindi wa haramu? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, mbinu za CCM ni za ushindi safi siyo ushindi mchafu, kwa hiyo siyo mbinu chafu hizo anazozungumza, ni ushindi safi, mipango, mikakati.

Sasa naomba nirudie kumjibu Mheshimiwa Khatib kwamba Wakurugenzi wala hawajakimbia, hakuna Mkurugenzi aliyekimbia na ndiyo maana maeneo yote ambayo maana yake wagombea wa Chama cha Mapinduzi walikuwa na sifa kuliko wagombea wengine wote na walijua mapema kwamba wasingeweza kuchaguliwa, lakini mpaka leo hatuna taarifa ya nani anayesema Mkurugenzi wa Halmashauri fulani amekimbia na amefungua kesi Mahakamani kudai hiyo haki yake, hakuna hiyo kesi mpaka leo. Kama wamekimbia wangeweza kulalamika, hatuna malalamiko officially. Ofisi ya Rais, TAMISEMI ndiyo inasimamia Halmashauri zote nchini na mamlaka za mitaa, hatuna taarifa ya hiyo kesi.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirudie; Waheshimiwa wananchi wasitiwe hofu na watu ambao wanaogopa siasa za ushindani. Kinachofanyika hapa ni kushindanisha Chama cha Mapinduzi na kazi yake nzuri na vyama vingine ambavyo havijafanyakazi nyingine yoyote na huenda wakifanya ni mambo madogo madogo sana, mambo makubwa makubwa ya Tanzania haya yamesimamiwa na Serikali kwahiyo mnapopeleka wagombea kwanza lazima utegemee mambo mawili, aidha, unashinda au unashindwa. Ukishindwa kubali na ukishinda mshukuru Mungu. Ahsante. (Makofi)