Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Katika kujenga Tanzania ya viwanda, Serikali imekuwa na mikakati ya muda mrefu. Je, ule mkakati wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI wa kujenga viwanda 100 kwa kila Mkoa ni sehemu ya mkakati na umeainishwa kwenye waraka gani wa Serikali ili kuwapa wananchi rejea ya pamoja ya kitaifa?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, report ya UNESCO ya mwaka 2018 inaeleza kwamba huwezi kuwa na viwanda kama huna nishati ya kutosha na maji ya kutosha. Je, Serikali inajua suala hilo? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; suala la viwanda 100 kila Mkoa ni suala lililotamkwa kisiasa. Serikali inaweza ikatuambia ni viwanda vingapi vilivyotengenezwa tayari katika Taifa hili la Tanzania ikiwepo Mkoa wa Mbeya kuna viwanda vingapi vimeshajengwa? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza anataka kujua kama Serikali inatambua umuhimu wa nishati ya umeme wa kutosha ili kuendesha viwanda hivi. Jibu ni kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi, Awamu ya Tano inatambua sana na ndiyo maana imeanzisha mikakati mbalimbali ya kuboresha na kuongeza umeme, kuna umeme wa gesi unazalishwa, lakini pia mpango mkakakti mkubwa sana ambao namuomba Mheshimiwa Sophia auunge mkono, ule wa kupata umeme kutoka Bonde la Mto Rufiji ili tupate umeme wa kutosha kwenye viwanda lakini pia matumizi ya majumbani. Lakini hata na wananchi wa kawaida hawajasahaulika ndiyo maana kuna umeme wa REA unalipwa kwa gharama ndogo sana ya shilingi 27,000 kwa kila Mtanzania na kila Kijiji, na nyumbani kwao watapata umeme wa kutosha sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili anataka kujua idadi ya viwanda ambavyo vimepatikana katika kila Mkoa na anasema ni tamko la kisiasa. Kwanza naomba nimwambie Mhehsimiwa Mbunge kwamba hili ni tamko mahususi la mpango mkakati wa Chama cha Mapinduzi, siyo tamko la kisiasa linatekelezeka, tumeshazindua, tumetuma mwongozo nchi nzima, Wakuu wa Mikoa wameitwa hapa Dodoma, Wakuu wa Wilaya wameelekezwa, Mamlaka ya Serikali za Mitaa imetenga maeneo mbalimbali ya kuanzisha viwanda, imeshiriki Mbeya, tumeenda Lindi na maeneo mengine. Tumeshapata viwanda vipya zaidi ya 3000 katika nchi nzima na nitawasiliana na viongozi wa Mkoa kupata idadi haliis ya Mkoa wa Mbeya ambao anatoka yeye kupata hivyo. (Makofi)

Kwa hiyo, naomba nimuombe Mheshimiwa Sophia ashiriukiane na Serikali ya Chama cha Mapinduzi na ikiwezekana na mwenyewe awezeshe, awe na kiwanda ili akina mama kama yeye waweze kupata uchumi jumuishi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:- Katika kujenga Tanzania ya viwanda, Serikali imekuwa na mikakati ya muda mrefu. Je, ule mkakati wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI wa kujenga viwanda 100 kwa kila Mkoa ni sehemu ya mkakati na umeainishwa kwenye waraka gani wa Serikali ili kuwapa wananchi rejea ya pamoja ya kitaifa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya vijana, akinamama na walemavu umeonesha kwamba katika baadhi ya mikoa fedha hizi zinatumika vibaya, lakini baadhi ya Mikoa kama Simiyu na Dar es Salaam wamebuni utaratibu wa kuwakopesha vijana na kuanzisha viwanda vidogo vidogo ambavyo vinajumuisha vijana, akinamama na walemavu kwa pamoja na hivyo kuanza taratibu utekelezaji wa hii sera ya viwanda katika jamii.

Sasa je, Serikali haioni kwamba upo ulazima wa mawazo haya na utekelezaji huu wa Simiyu na Dar es Salaam kuenezwa katika mikoa mingine ili fedha hizi ziweze kusaidia kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwa ajili ya kutekeleza huo mkakati wa viwanda?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, Mheshimiwa Selasini ni Mjumbe wa Kamati ya Utawala ya Bunge hili tukufu pamoja na Mheshimiwa Rweikiza, Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tabora, lakini Wajumbe hawa wa Kamati hii tunawashukuru sana Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwenye bajeti iliyopita tumeshirikiana vizuri, haya ni mawazo ya Kamati ya Utawala ambapo Mheshimiwa Selasini alikuwepo pale. Simiyu tumeenda na mimi nimetembelea Kiwanda kile cha Chaki lakini pia Dar es Salaam tunafahamu na juzi Jumatatu iliyopita nimefanya ziara katika Mkoa wa Dodoma na wenyewe wamesaidia kununua mashine ya kutengeneza matofali na vijana wanaendelea kujiajiri.

Mheshimiwa Naibu Spiika, naomba nitoe maelekezo ambayo yatakuwa ni marudio; tumetoa maelekezo asilimia 10, asilimia nne ile ya akinamama, nne kwa vijana na mbili kwa watu wenye ulemavu au mahitaji maalum. Tumeelekeza badala ya kutoa fedha kwa vikundi au mtu mmoja mmoja ambazo kimsingi hazileti tija, lengo la kukopesha fedha hizi ni kuwasaidia akinamama na makundi haya muhimu ili yaweze kuboresha maisha yao. Wakurugenzi wameelekezwa, Makatibu Tawala wameelekezwa ili iete tija. Wanaweza wakaatenga maeneo ya viwanda, wakawakusanya vijana, akinamama na watu wenye ulemavu na tumeshatoa kanuni ipo mtaani ili waelekezwe na wanapata mafunzo wakianzisha viwanda vidogo vidogo watajiajiri, fedha itapatikana, wataboresha maisha yao, lakini pia warudishe fedha ili makundi mengine zaidi yaweze kupata huu msaada na mchango wa Serikali. Ahsante. (Makofi)