Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI aliuliza:- Mkoa wa Ruvuma umepata mnunuzi wa tumbaku ambaye amekubali kuwawezesha SONAMCU kufufua kiwanda cha kuchambua tumbaku na kugeuza green leaf kuwa dry leaf. Aidha, kutokana na changamoto za kodi na soko mnunuzi huyo hajaweza kutekeleza azma yake. Je, Serikali inasaidiaje kutatua changamoto zinazomkabili mnunuzi huyo?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Kilimo na Serikali yetu kwa ujumla kwa jibu hilo zuri.

Hata hivyo ili tuwe na uelewa wa pamoja kati ya Serikali na wakulima wa tumbuku wa Namtumbo; je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuzifafanua changamoto hizo za mnunuzi wa tumbaku zinavyotakiwa kutatuliwa na Serikali kwa ujumla wake? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali dogo la pili, wakulima wa Namtumbo wanalishukuru sana Bunge lako tukufu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa kwa umahiri mkubwa na Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli, Rais wetu kwa kuwawezesha wakulima wa Namtumbo hadi sasa katika minada mitatu tu wamepata shilingi bilioni 5.5 la zao la ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani. (Makofi)

Je, Serikali iko tayari kuendelea kutatua changamoto za wakulima wa Namtumbo hususan katika mazao ya korosho, soya, mbaazi na mengineyo na hasa katika korosho wale wakulima wachache ambao mpaka sasa hawajalipwa, wameuza korosho zao mwezi wa kumi hususan wa Tarafa wa Sasawala, lini watalipwa? (Makofi)

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA): Mheshimiwa Spika, swali la kwanza Mheshimiwa Ngonyani angependa kupata commitment ya Serikali kama tunaweza tukakaa pamoja na Mheshimiwa Mbunge, pamoja na wakulima wake ili kuweza kutatua changamoto ambazo anakabiliana nazo huyu mwekezaji PATL. Kwa sababu ya muda na kwa vile Mheshimiwa Ngonyani ni mfuatiliaji mzuri, hili ni swali la pili katika kikao hiki basi nimuahidi kwamba nitakaa naye na tutafute muda kuweza kukaa pamoja na kuainisha hizi changamoto ambazo tayari Wizara tunazifahamu na kuzijadili na kuangalia namna bora ya kuzitatua haraka iwezekanavyo ili mwekezaji huyo aweze kuendelea na uwekezaji, wakulima wetu waweze kupata mahali pa kuchakata tumbaku yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Ngonyani anauliza kama Serikali iko tayari kufanya maboresho na kuongeza jitihada za kuhakikisha mazao ya korosho, soya, mbaazi na mazao mengineyo yanamsadia mkulima Mtanzania na jibu ni ndiyo. Azma ya Serikali ni kuhakikisha mazao yote haya na mengine tunaongeza uzalishaji na tunawasaidia wakulima wetu kuwa na kilimo cha tija na sambamba na hilo tunawasaidia wakulima wetu kuwaunganisha na masoko. Suala la malipo ya korosho nimhakikishie Mbunge kuwa Serikali inaendelea kufanya kila iwezekanavyo kuhakikisha waliobaki ambao hawajalipwa na ambao ni wachache waweze kulipwa malipo yao, ahsante.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa huyu mwekezaji amefanya jitihada kabisa kuhakikisha kwamba anawekeza katika kile kiwanda na amewekeza anadai zaidi ya dola za Marekani milioni tatu na hivi sasa alikuwa amesimama kutokana na changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikimkabili. Lakini Serikali tumepanga kabisa kwamba ndani ya wiki mbili hizi tutakaa naye ili tuweze kuzungumza pamoja ikiwa ni pamoja na kuangalia suala lile la madai ya VAT ambayo yalikuwa yamekaa muda mrefu ambayo anasema kwamba yamemuathiri katika kuendeleza hiki kiwanda. Kwa hiyo, tutakaa naye pamoja na makampuni mengine yale ambayo nayo yana changamoto hiyo hiyo ili tuweze kuhakikisha kwamba hili suala linafikia mwisho na kusudi waendelee kununua zao letu la tumbaku. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI aliuliza:- Mkoa wa Ruvuma umepata mnunuzi wa tumbaku ambaye amekubali kuwawezesha SONAMCU kufufua kiwanda cha kuchambua tumbaku na kugeuza green leaf kuwa dry leaf. Aidha, kutokana na changamoto za kodi na soko mnunuzi huyo hajaweza kutekeleza azma yake. Je, Serikali inasaidiaje kutatua changamoto zinazomkabili mnunuzi huyo?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Changamoto ya ununuzi wa tumbaku inafanana sana na changamoto wanayokabiliana nayo wakulima wa zao la mahindi. Hivi sasa ni msimu wa mavuno, ningependa kujua kwa Serikali imejipangaje kwa mwaka huu juu ya ununuzi wa zao hili la mahindi?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa katika msimu uliopita tulikuwa na changamoto ya masoko ya zao la kilimo, lakini kama sote tunavyojua, Serikali imekuwa ikihakikisha kwamba inatafuta masoko na muda huu tunapoongea tumepata masoko makubwa sana ya mahindi katika nchi za Kusini. Hivi sasa Rwanda wanahitaji zaidi ya tani 100,000; Burundi wanahitaji zaidi ya tani 100,000; lakini nchi ya Zimbabwe wanahitaji tani 800,000 za mahindi na nchi nyingine nyingi zinahitaji mahindi kwa wingi.

Kwa hiyo, ninachotaka kusema ni kwamba sasa hivi soko la mahindi ni kubwa sana, wakulima wote wenye mahindi tunaomba wajitokeze watuambie wana kiasi gani, washirikiane na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuanzia wiki taasisi zetu ikiwemo NFRA pamoja na CPB wanaanza kununua mahindi na kukusanya mahindi kutoka kwa wakulima mbalimbali pamoja na wafanyabiashara, lakini pia taasisi nyingine ambayo tumeipa jukumu la kupeleka mahindi Zimbabwe nayo inaanza kununua mahindi wiki hii.

Kwa hiyo wakulima wakae mkao kila mahali wenye mahindi sasa hivi ni wakati wa kula mkate mzuri, nakushukuru. (Makofi)

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI aliuliza:- Mkoa wa Ruvuma umepata mnunuzi wa tumbaku ambaye amekubali kuwawezesha SONAMCU kufufua kiwanda cha kuchambua tumbaku na kugeuza green leaf kuwa dry leaf. Aidha, kutokana na changamoto za kodi na soko mnunuzi huyo hajaweza kutekeleza azma yake. Je, Serikali inasaidiaje kutatua changamoto zinazomkabili mnunuzi huyo?

Supplementary Question 3

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi ya kuuliza swali.

Mheshimiwa Spika, sasa tunaelekea kwenye msimu ujao wa zao letu la korosho na nilitaka nipate maelezo kutoka Serikalini, mpaka hivi sasa wakulima hawajapata taarifa zozote juu ya uwepo na lini na bei elekezi ya pembejeo. Kwa hiyo, ningeomba Serikali itoe maelezo ili kuhakikisha wakulima wanapata ufahamu juu ya uwepo wa pembejeo lakini bei elekezi itatolewa lini, lakini pia ni lini itasambazwa?(Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ni kweli sasa hivi ni msimu wa kilimo cha zao la korosho hasa katika kupulizia madawa ikiwemo sulfur na maeneo mengine. Sasa hivi Serikali tumejipanga tumehakikisha kwamba sulfur ipo ya kutosha katika maeneo yote tumeshapaleka na bado tunajaribu kufanya tathmini kuangalia kama kuna sehemu tuna upungufu ili tuhakikishe kwamba hayo madawa yanakuwepo. Sambamba na hilo tumeanza kujiandaa kabisa katika msimu unaokuja ikiwa ni pamoja na uteuzi wa Bodi ya Korosho ambayo tayari tumeshaiteua kwa ajili ya kuanza kazi na kuweza kupanga mikakati mbalimbali ya kuendeleza hili zao la korosho.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge avute tu muda ni kwamba kila tumejipanga na kitakwenda vizuri na nina uhakika wakulima wa korosho watafurahi sana, ahsante.