Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA) aliuliza:- Serikali imerejesha vyuo vilivyokuwa vya maendeleo kuwa chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukibadili Chuo cha Maendeleo Ikwiriri FDC kuwa VETA ili kubadili fikra za wananchi wa Rufiji, Kibiti na Ikwiriri na hatimaye kuleta mwamko wa elimu?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza maswali ya nyongeza.

Kwa kuwa wananchi wa Rufiji wamekuwa na shida kubwa kupata Chuo cha VETA rufiji, pamoja na juhudu za Mbunge wao kupambana kutafuta jinsi gani ya kupata Chuo cha VETA ndio sababu akaona hata kuna haja kubadilisha vyuo vya FDC labda wanafunzi wa Rufiji waweze kupata elimu hiyo ya VETA, na Kwa kuwa Serikali sasa imeshatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa VETA - Rufiji ni jambo la shukrani na pongezi sana kwa Serikali, je, Serikali sasa ni lini ujenzi huo utaanza rasmi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kwa kuwa katika Mkoa wa Dar es Salaam kuna Chuo kikubwa sana cha VETA Kipawa, chuo hiki ni kikubwa mno, lakini hatujawahi kuona matangazo mbalimbali juu ya elimu inayotelewa hapo au ni mwaka gani wa mafunzo ambao unaanza lini na lini wanafunzi waweze kuhamasika kujiunga na Chuo cha VETA Kipawa?

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kukitangaza hiki Chuo cha VETA Kipawa ambacho Serikali imewekeza fedha nyingi sana na chuo ni kizuri mno, ili wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali waweze kujiunga na chuo hiko?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, kuhusiana na lini ujenzi wa Chuo cha VETA cha Rufiji kitaanza, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba fedha zimetengwa katika mwaka wa fedha unaokuja na fedha hizo zipo, kwa hiyo, siyo za kutafuta. Kwa hiyo, ujenzi utaanza mara moja, Rai yetu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji ni kwamba watupatie eneo lenye hati ili ujenzi uanze bila kuchelewa.

Mheshimiwa Spika, lakini pia swali lake la pili kuhusiana na Chuo cha VETA Kipawa, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba VETA nchi nzima kawaida inakuwa na utaratibu wa kutangaza nafasi za masomo katika vyuo vyake vyote lakini kama Mheshimiwa Mbunge anaona haitoshi katika Chuo cha Kipawa naomba nitumie fursa hii kumuagiza Mkurugenzi Mkuu wa VETA ahakikishe kwamba matangazo yale yanatolewa na aongeze kasi na wigo wa kutangaza nafasi mbalimbali za VETA zote nchini.

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI (K.n.y. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA) aliuliza:- Serikali imerejesha vyuo vilivyokuwa vya maendeleo kuwa chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukibadili Chuo cha Maendeleo Ikwiriri FDC kuwa VETA ili kubadili fikra za wananchi wa Rufiji, Kibiti na Ikwiriri na hatimaye kuleta mwamko wa elimu?

Supplementary Question 2

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha VETA Ludewa kilipaswa kiwe kimeshakamilika toka mwaka jana mwezi wa nane, lakini mpaka leo hivi ninavyozungumza Chuo cha VETA kile Ludewa hakina dalili na mkandarasi hayupo. Je, ni lini Chuo cha VETA Ludewa kitakamilika? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kwanza nitumie nafasi hii kukiri na kuweka wazi kwamba Mheshimiwa Deogratias Ngalawa amekuwa akifuatilia sana ujenzi wa Chuo cha Ludewa au Chuo cha VETA Mkoa wa Njombe.

Mheshimiwa Spika, uchelewaji wa ujenzi wa chuo husika umetokea kwa sababu mkandarasi ambaye alipewa kazi ya kujenga chuo kile alifanya madudu na Serikali ilibidi kusitisha mkataba. Kwa sasa tayari mfadhili wa mradi ambaye ni Benki ya Maendeleo ya Afrika tayari ameshatupa ruhusa ya kutangaza kandarasi upya. Kwa hiyo, kwa sasa tupo katika hatua za kumpata mkandarasi mpya ili ujenzi uweze kuendelea.

Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ujenzi utaanza mara tu Mkandarasi mpya atakapopatikana na hatutegemei ichukue tena muda mrefu.