Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. MARTIN A. MSUHA) aliuliza:- Uhaba wa walimu wa Hisabati na Sayansi umeathiri sana matokeo ya darasa la saba mwaka 2017 Wilayani Mbinga. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka walimu wa masomo hayo Wilayani Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kupata nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa vile uhaba huu wa walimu kwa sehemu nyingine unachangiwa na kutokuwa na msawazisho sawa wa shule zetu mbalimbali hasa baina ya shule za mijini na vijiji na hivi kusababisha shule za vijiji ziwe na walimu wachache zaidi ukilinganisha na sehemu za miji. Ni lini sasa Serikali itakamilisha mchakato wake wa kuhakikisha kwamba kuna kuwa na msawazisho wa walimu ili uhaba au toshelevu wa walimu ulingane mijini na vijijini?

Mheshimiwa Spika, pili, kwa vile tumeona vijana wengi waliohitimu taaluma ya ualimu bado wapo mtaani kwa muda mrefu sasa na wengine zaidi ya miaka minne/mitano na bado Serikali inawekeza fedha nyingi kwenye kusomesha vijana hawa katika vyuo vyetu vikuu kwa nini sasa Serikali isiangalie utaratibu mpya wa kusomesha vijana wetu kwa kulingana kwa mahitaji ya soko la ajira na mahitaji ya Taifa katika ujumla wake na kuwawezesha vijana wetu waweze kuwekeza zaidi katika ujasiliamali? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA W. WAITARA): Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa maoni na mtazamo wake, lakini wiki iliyopita nilitoa taarifa kwenye Bunge lako tukufu kwamba tumepeleka fedha katika Halmashauri zote ambazo kazi, moja, nikumalizia maboma ya shule za Msingi lakini pia lingine ni kusawazisha au ku- balance ikama katika shule zetu. Tumeelekeza Wakurugenzi, Walimu na Makatibu Tawala wa Mikoa kwamba wahahakishe kwamba fedha hii inatumika kuwahamisha walimu ili moja, kuangalia kusambaza walimu katika upungufu uliopo katika maeneo ya mjini ili waende maeneo ya pembezoni; lakini la pili kuangalia zile hoja kwamba kuna shule ina mwalimu kike haina mwalimu wa kiume au wakiume haina wakike pia izingatiwe hilo. Kwa hiyo kazi inafanyika tunatarajia kwamba Wakurugenzi na viongozi wa mikoa watasimamia hili na Waheshimiwa Wabunge ni kwa sababu ni sehemu ya mikoa yenu hili ni taarifa rasmi naomba mtusaidie kusimamia.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anasema tufundishe wanafunzi wetu kulingana na mahitaji, juzi Mheshimiwa Waziri wa Nchi alitangaza matokeo ya form four na mojawapo ya kazi iliyofanyika ni kugawanya wanafunzi katika maeneo mbalimbali, sasa hili la kusema tuweke kulingana na idadi, ni kweli kwamba walimu wapo mitaani lakini ukweli kwamba tunahitaji walimu wengi katika sekta zote shule ya msingi na sekondari.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa sababu kila mwanafunzi amelekwa mahali ambapo anahitaji, na tunatarajia kuna shule za Serikali na watu binafsi lakini pia na shughuli binafsi na tunaendelea kuangalia mchakato wa kuhakikisha wanafunzi hawa badala ya kutegemea kuajiriwa na Serikali ambalo ni jambo la kitaifa kwa kweli ni lazima tuanzishe utaratibu wa watu kufanya kazi hata kwa shughuli binafsi yaani isiwe ile knowledge based, iwe ni competent. Kwa hiyo tunalichukua tunafanyia kwa siku za usoni tutaweza kulizingatia, ahsante.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. MARTIN A. MSUHA) aliuliza:- Uhaba wa walimu wa Hisabati na Sayansi umeathiri sana matokeo ya darasa la saba mwaka 2017 Wilayani Mbinga. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka walimu wa masomo hayo Wilayani Mbinga?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, matatizo ya walimu wa sayansi yameikumba sana Wilaya Kilombelo hususani jimbo la Mlimba karibuni ina shule 26 za sekondari. Lakini hivi karibu tumepata walimu wa sayansi wanne tu na kupelekea shule nyingi za sekondari kukosa walimu wa sayansi.

Je, Serikali ina mpango gani kutupelekea walimu wa sayansi Wilaya ya Kilombero husani jimbo la Mlimba ukizingatia tunakula samaki, kwa hiyo, watoto wana akili sana ya mahesabu na sayansi kwa mfano bora angalia tumemtoa Mheshimiwa Likwelile alikuwa kule Wizarani tumemtoa Benno Ndulu kwa hiyo sasa hivi tunakosa wasomi kwa sababu hatuna walimu wa sayansi. Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA W. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge ameuliza mara kadhaa swali hili tunamshukuru, lakini tumepeleka walimu wachache kulingana na mahitaji yaliyopo, lakini tumeomba kibali cha kuajiri walimu wa kutosha mwezi huu wa sita au mwaka wa fedha mpya ukianza. Kwa hiyo, pindi tutakapopata hicho kibali Mheshimiwa Mbunge ndio maana nakuhakikisha kwamba suala Mlimba na maeneo mengine yenye upungufu mkubwa kama kwako kule tunazingatia maombi yako muhimu. Ahsante.