Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Kampuni ya Azam Marine ambayo inafanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia boti kupitia baharini, huuza tiketi kwa abiria kwa ajili ya safari lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo huwa haitumiki na hivyo kusababisha hasara kwa abiria pamoja na usumbufu;- (a) Je, Serikali inalijua hilo? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana. Watanzania wengi wanapata hasara kubwa sana katika hili suala abiria akichelewa boti tu tiketi yake imekufa kabisa hawezi kutumia kwa wakati mwingine wowote inasababisha kadhia kubwa kwa Watanzania wetu.

Hakuna Shirika lolote la Ndege duniani ambalo ukichelewa tiketi yake inakuwa imekufa, unalipa kiwango cha fedha kama ni dola 50 tiketi yako inaweza kuendelea kufanya kazi, hata Shirika letu hili la Tanzania pia hata ukichelewa unaweza kupanda ndege kwa wakati mwingine lakini Kampuni hii ya Azam Marine ukichelewa tiketi imekufa kabisa wala huwezi kutumia tena ni jambo la ajabu sana. Sasa ni lini Serikali itaondosha kadhia hii ili hawa abiria wetu wapate maslahi makubwa kutumia vyombo hivi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, kwanza siyo kweli kwamba mashirika yote ya ndege huwa tiketi yake ukichelewa yanarudishwa kuna zile Easy Jets ambazo kwa mfano Fastjet ukichelewa tiketi huwa haurudishiwi wala haupangiwi safari siku nyingine kwahiyo siyo kwamba ni mashirika yote ya ndege.

Mheshimiwa Spika, pia najaribu kuwashauri hata Watanzania wenzetu unapokuwa umepanga safari basi ujue kwamba kuna muda wa kuondoka na muda wa kufika. Haiwezekani tuwe tuna panga safari halafu unafanya mambo mengine tofauti na safari yako.

Katika majibu yangu ya msingi nimeeleza tu kwamba Shirika la Azam Marine huwa lina utaratibu ukitoa taarifa mapema tena waliandika kwenye tiketi yao nyuma ukitoa taarifa mapema kabla ya safari kwamba hutasafiri wana utaratibu wa kuiuza hiyo tiketi kwa watu wengine ili wewe wakupangie wakati mwingine, lakini sasa muuliza swali Mheshimiwa Mbunge yeye nafikiri anafikiri kwamba akishachelewa bila kutoa taarifa anaweza akapewa, sasa yeye Azam Marine atakuwa ameingia hasara kitu ambacho siyo kweli.

Mheshimiwa Spika, nawashauri Watanzania tupange safari zetu tuwe na uhakika wa kusafiri siku husika, tujiandae, halafu tuweze kuwahi ili tusipate matatizo kama hayo. (Makofi)

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Kampuni ya Azam Marine ambayo inafanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia boti kupitia baharini, huuza tiketi kwa abiria kwa ajili ya safari lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo huwa haitumiki na hivyo kusababisha hasara kwa abiria pamoja na usumbufu;- (a) Je, Serikali inalijua hilo? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona. Serikali imekuwa ikitoa utaratibu elekezi wa kibei kwa maeneo mengi ya usafiri wa umma kwa wenzetu wenye mahitaji maalum na wanafunzi. Ni upi utaratibu uliowekwa kwenye usafiri wa maji kwa wenzetu hawa wenye mahitaji maalum? Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Khadija Nassir kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa vyombo vya Serikali utaratibu upo tunazo meli za MSCL ambao kwa kweli utaratibu wa nauli huwa upo na uko wazi, lakini kwa vile vyombo ambavyo ni vya binafsi ambavyo vinasaidiana na Serikali katika kuhudumia wananchi, huwa tunaacha soko lijipeleke lenyewe, lijiendeshe. Kwa hiyo wale watu wanaomiliki vyombo vya usafiri wa majini huwa wanapanga bei kutokana na faida wanahisi wataipata pamoja na huduma ambazo wanaweza wakawasaidia wananchi.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Kampuni ya Azam Marine ambayo inafanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia boti kupitia baharini, huuza tiketi kwa abiria kwa ajili ya safari lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo huwa haitumiki na hivyo kusababisha hasara kwa abiria pamoja na usumbufu;- (a) Je, Serikali inalijua hilo? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kutambua jitihada za Serikali katika kuboresha mawasiliano na uchukuzi katika nchi yetu na hasa maboresho yaliyofanyika katika Shirika la Ndege la Tanzania sasa hivi kumeanza kujitokeza tatizo la ucheleweshaji wa ndege. Kila mara unaposafiri ndege inasogezwa, inasogezwa, inasogezwa na hili jambo linakera sana. Chanzo cha tatizo hili ni nini na Serikali mnachukua hatua gani kurekebisha? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nape Moses Nnauye, Mbunge wa Mtama, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika siku za karibuni kumetokea changamoto ya uchelewaji (cancelation) kwa Shirika letu la Ndege la Tanzania. Tatizo hili limetokana na sababu mbalimbali za kiufundi ambazo zimerekebishwa.

Mheshimiwa Spika, kwenye hotuba ya kuhitimisha bajeti yetu tulitoa maelekezo Menejimenti na Bodi ya ATCL kwamba kama kutakuwa na cancelation yoyote au delay ya zaidi ya nusu saa tupate taarifa ya maandishi ya sababu zilizobabisha hiyo ndege ichelewe kuondoka kwa zaidi ya nusu saa. Hilo limeshaanza kufanyika na huwa tanapata taarifa.

Mheshimiwa Spika, tunaendelea kuwasisitiza ATCL kwamba wateja ndiyo watu wa thamani sana. Kwa hiyo, delay ambazo hazina sababu ya msingi ziepukwe sana.

Mheshimiwa Spika, nikutaarifu wewe na Bunge lako kwamba sasa hivi marekebisho yameshaanza kufanyika. Sasa hivi ATCL wameshaanza kwenda vizuri, delay na cancelation ambazo sio technical hazitokei tena.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Kampuni ya Azam Marine ambayo inafanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia boti kupitia baharini, huuza tiketi kwa abiria kwa ajili ya safari lakini abiria anapochelewa safari tiketi hiyo huwa haitumiki na hivyo kusababisha hasara kwa abiria pamoja na usumbufu;- (a) Je, Serikali inalijua hilo? (b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Adhabu ya kaburi aijuaye maiti. Sisi tunaosafiri na Azam ndiyo tunafahamu adha yake.

Mheshimiwa Spika, hata ukisafiri na ile charter ya abiria 11 mzigo wa kilo 15 - 20 hulipishwi lakini ndani ya boti ya Azam unalipishwa. Namwomba Mheshimiwa Waziri achukue mfuko mmoja wa mchele tuliogawiwa asafiri nao aone kama hatalipishwa. Kwa hiyo, tunaomba Serikali ifuatilie suala hili na itupatie ufumbuzi.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yussuf, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, suala la huduma ya safari za majini mara nyingi ni kati ya abiria na mwenye mali. Ukifugua nyuma ya tiketi ile kuna masharti ambayo yanaandikwa kwa uwazi na kwa lugha nyepesi kabisa. Ninawashauri sana Watanzania tuwe tunasoma masharti yale ili kama ukiona hayakidhi mahitaji yako basi usiende. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nyuma tiketi ya Azam kuna maelezo yanayoeleza mpaka kiwango cha mzigo unachotakiwa kwenda nacho ndani ya meli. Sasa anayepima ni yule mwenye meli kama imezidi anaruhusiwa kukukatalia kwa sababu ndiyo mkataba ulioingia wewe abiria na yule mwenye meli. Kwa hiyo, nawashauri Watanzania tuwe tunasoma vigezo na masharti vya kuingia kwenye huduma hizo.