Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ni machache, madogo na machakavu hasa yale ya kulaza wagonjwa:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo hayo na ujenzi wa majengo mapya?

Supplementary Question 1

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza kwa niaba ya wananchi wa Ulanga, naomba niishukuru Serikali ya CCM kwa kutupa kipaumbele kwenye Sekta ya Afya. Maana yake tumepata shilingi milioni 400, Kituo cha Afya cha Lupilo kimeisha na shilingi milioni 400 imeingia juzi.

(a) Hospitali hii ya Wilaya wakati inajengwa, mwaka 1905 wilaya ilikuwa na watu 23,000, leo hii wilaya ina watu zaidi ya 200,000: Serikali haioni kiasi hiki cha fedha, shilingi milioni 400 kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa hospitali hii ni kidogo sana?

(b) Hospitali yetu ya Wilaya ya Ulanga imekuwa na changamoto kubwa sana ya watumishi wachache na wasio na sifa: Je, lini Serikali italeta watumishi wa kutosha na wenye sifa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza tunapokea pongezi za Serikali kutoka kwa Mheshimiwa Mbunge na kwa niaba ya wananchi wa Ulanga. Mheshimiwa Mbunge ana maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, tumepeleka shilingi milioni 400, anadhani kwamba ni pesa kidogo.

Naomba tu nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba hii ni awamu ya kwanza, tunapeleka fedha katika maeneo mbalimbali ya nchi hii kama alivyosema kwa kuzingatia kipaumbele cha afya. Baada ya awamu hii kwisha tutaangalia pia kutokana na uwezo wa Serikali tutaongeza fedha nyingine. Lengo ni kuimarisha hospitali hii iweze kutoa huduma inayostahiki na hata kadri ambavyo wananchi wapya wataendelea kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, swali la pili Mheshimiwa Mlinga anauliza habari ya watumishi. Muda uliopita Naibu Waziri mwenzangu, Mheshimiwa Kandege, alitoa taarifa kwenye Bunge hili Tukufu kwamba tumeshapeleka barua kuomba kupata kibali cha kuajiri watumishi kwa upande wa Sekta za Elimu na Afya. Kwa hiyo, wakati wowote tukipata kibali hicho, tutakapoajiri tutazingatia maombi ya Mheshimiwa Mbunge lakini pia na maeneo mengine ya nchi hii. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ni machache, madogo na machakavu hasa yale ya kulaza wagonjwa:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo hayo na ujenzi wa majengo mapya?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Hospitali yetu ya Ulanga ina tatizo na tatizo ni kuwa haina gari la wagonjwa: Je, Serikali ni lini itatupatia gari la wagonjwa kwenye Hospitali yetu ya Ulanga?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni kweli kwamba kuna maeneo mengi ambayo bado tuna upungufu wa vitendea kazi. Tunaomba tulipokee swali hili. Kadri tutakavyopata uwezo tutapeleka gari katika eneo hili pamoja na maeneo mengine ya nchi ambayo kwa kweli kuna changamoto ya mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa tumeelekeza kwamba katika maeneo ya jirani au kwenye Hospitali ya Wilaya ya jirani inapotokea shida au hata magari ya Halmashauri yatumike kutoa huduma hiyo. Tutajitahidi kadri itakavyowezekana magari yapatikane katika Hospitali ya Wilaya, ikitokea shida ya mgonjwa basi apate huduma haraka kupelekwa kwa hatua nyingine ya mbele.

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ni machache, madogo na machakavu hasa yale ya kulaza wagonjwa:- Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo hayo na ujenzi wa majengo mapya?

Supplementary Question 3

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Majimbo ya Kibamba na Ubungo kabla hayajaondolewa kwenye Manispaa ya Kinondoni yalikuwa yanahudumiwa na Hospitali ya Mwananyamala. Sasa baada ya kuanzishwa kwa Wilaya mpya ya Ubungo, huduma tunazipata kwenye Hospitali ya Sinza Palestina ambayo hailingani na wingi wa watu wa Majimbo haya mawili ya Kibamba na Ubungo na haina eneo kubwa kwa ajili ya kuipanua kuwa hospitali kubwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, sasa je, Serikali iko tayari sasa kwa kuwa Makao Makuu ya Wilaya ya Ubungo yako ndani ya Jimbo la Kibamba eneo la Kwembe na kuna ardhi kubwa imepimwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa satellite town Luguruni: Je, Serikali iko tayari sasa kwenda kujenga hospitali ya wilaya kule ili wananchi wa maeneo ya kule wapate huduma ya eneo la karibu zaidi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni kweli kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge anazungumza, lakini katika Mkoa wa Dar es Salaam tumepeleka fedha kuimarisha kituo pale Kinondoni, tumepeleka fedha shilingi milioni 200 pale Sinza, tumepeleka fedha Kigamboni shilingi milioni 1.5 kwa awamu ya kwanza na pale Ilala na tumeongeza shilingi milioni 500.

Mheshimiwa Spika, naomba tupokee ombi hili. Ukweli ni kwamba kila palipo na Makao Makuu ya Wilaya patakuwa na huduma ya wananchi. Awamu hii ikimalizika tutapeleka fedha katika eneo hilo ili wananchi wetu waweze kupata huduma. (Makofi)