Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za ujenzi wa jengo jipya la kisasa la Askari Polisi wa Makunduchi?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri na yenye tija ndani yake na pia nakiri kwamba katika kituo cha Dunga ni kweli tayari hili jengo liko katika kukamilisha mwisho wake kuwa zuri sana na lifanye kazi. Niseme maswali yangu mawili ya nyongeza, kwa kuwa jengo la Makunduchi la muda mrefu na mwaka 2015 waliamua polisi kuweka foundation pale ili wapate kituo chao cha uhakika, je sasa swali langu liko hapa; Serikali itamaliza ujenzi huu lini? Swali langu la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwamba eneo la Makunduchi ni eneo la utalii. Kila mwaka kule Makunduchi kunakuwa kunafanywa Mwaka Kogwa, na ukizingatia hata mwaka jana Mheshimiwa Waziri wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa yeye ndiyo mgeni rasmi alikwenda kule. Swali langu lipo hapa, Serikali ina mpango gani wa kuweka ulinzi katika eneo lile hasa sambamba na ujenzi wa vituo vya polisi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikianza na swali lake la kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika maeneo ambayo tunayaangalia kwa karibu pale ambapo bajeti itakapokaa vizuri tuweze kumaliza ni hilo jengo ambalo amelizungumza la kituo cha polisi Makunduchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kuimarisha ulinzi hasa ukizingatia eneo la Makunduchi ni sekta ya utalii, nimhakikishie kwamba sasa hivi tunavyozungumza tuna mkakati kabambe wa kuimarisha usalama katika maeneo hususan Ukanda wa Pwani wa Zanzibar maeneo ambayo yamekuwa yanatumika kiutalii ili tuweze kuongeza imani ya watalii na wawekezaji katika ukanda huo. Kwa hiyo, tutakapokamilisha mkakati huo, sehemu ya Makunduchi ni moja katika maeneo ambayo yatafaidika.