Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:- Je, kuna utaratibu wowote wa kuajiri watu wote waliohitimu Vyuo na kukidhi vigezo vya kuajiriwa?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, swali langu la msingi nilisema wahitimu wa vyuo vikuu waliokidhi Vigezo, sikusema waliohitimu tu ndiyo wote wanastahili kuajiriwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa taarifa ya Serikali, kila mwaka takribani Wahitimu laki nane, kwa mwaka, na wanaoajiriwa ni elfu arobaini peke yake, kwa hiyo laki saba na sitini wanabaki mtaani. Ningependa kujua Serikali ina Mkakati gani wa ziada, kwa sababu Mkakati uliopo umeshindwa kukidhi vigezo vya kuweza kuwaajiri vijana wengi ambao wamehitimu? Ni Mkakati gani wa ziada ambao Serikali inao kwa ajili ya kuwasaidia Vijana hawa ambao wengi wako mtaani?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Kumekuwa na vikwazo mbalimbali kwa hawa wahitimu wanapokuwa wanaomba kazi, na kikwazo namba moja, ni kikwazo ambacho wanawaambia kwamba wawe na uzoefu, na wakiamini wametoka chuoni. Ningependa kujua, Serikali haioni ni kuna Mkakati ambao unahitajika wa ziada sana, kuwa na programu maalum ya kuwa andaa Vijana hawa kabla ya hawajakwenda kazini? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, naomba niseme kabisa kwamba kila Mtanzania ana haki ya kuomba ajira kwenye Utumishi wa Umma. Lakini vilevile, tuangalie kwamba ajira za Serikalini huzingatia sana scheme of service, huzingatia sana ikama, na bajeti iliyopangwa kwa wakati huo, na vilevile kutegemea na vipaumbele vya Taifa wakati huo. Niwahase wahitimu wote nchini waendelee kuomba ajira kupitia sekretarieti yetu ya ajira ambayo tumeboresha sasa hivi inapitia ajira portal kupitia njia ya mtandao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naomba niliambie Bunge lako Tukufu pia kwamba mwaka ule wa fedha 2018/ 2019 Serikali iliweza kuajiri ajira mbadala na ajira mpya zaidi ya elfu arobaini na moja na laki na sita na Kada ya Walimu ilikuwa elfu nne na mia tano. Lakini kwa mwaka huu wa fedha naomba niliambie Bunge lako Tukufu kabisa kwamba Serikali inatarajia kuajiri zaidi ya ajira elfu arobaini na nne na laki na nane, lakini kana kwamba hiyo haitoshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niliambie Bunge lako Tukufu kwamba Serikali ya Awamu ya Tano pia imejipanga tumeanzisha Sera ya local content ili private sector zote nchini ziweze kuajiri Watanzania na nichukue fursa hii kuwapongeza sana Mkoa wa Pwani kwa sababu wao wamezingatia sana Sera ya Viwanda na Uchumi na wameweza kuajiri zaidi ya Watanzania elfu hamsini, iwe ni in direct iwe ni direct na naomba nitoe Rai, Mikoa mingine pia iweze kuiga mfano wa Mkoa wa Pwani ambao wanaufanya mpaka sasa hivi, ili Watanzania wengi pia waweze kupata ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili, la Mheshimiwa Mbunge Khenani anazungumzia Mikakati ya Serikali ambayo mingine nimeitaja, amezungumzia kuhusu uzoefu na naomba niseme katika Sera yetu mpya ya Utumishi 2004 Serikali imesema kabisa kwamba ajira mpya hazitazingatia uzoefu, uzoefu unakuja kwa wale ambao tayari wako kazini. Ahsante.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nirudi kwenye swali la nyongeza la pili la Mheshimiwa Aida Khenani na hasa eneo lile ambalo vijana wengi wa Kitanzania wamekuwa wakipata shida sana ya kigezo cha uzoefu, katika kutafuta ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na vijana, kweli limekuwa ni tatizo, Ofisi ya Waziri Mkuu inasimamia masuala ya Ustawi wa Vijana, na baada ya kugundua kwamba vijana wengi wamekosa sifa za kuajiriwa kwa sababu ya kigezo cha uzoefu, Ofisi ya Waziri ya Mkuu, iliamua kutengeneza mwongozo mpya, wa internship ili kuhakikisha vijana wanapomaliza masomo yao, waweze kupata maeneo ya kupata uzoefu kwenye private sector na maeneo mbalimbali, na zinapotoka nafasi za ajira kigezo cha uzoefu kiwe tena siyo kikwazo kwa ajili ya ajira zao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kulihakikishia Bunge lako Tukufu kuwa program hiyo sasa imekwisha kuanza, na Ofisi ya Waziri Mkuu imeshasimamia makundi ya kutosha ya vijana na kuwapeleka kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya internship programme tayari kwa kuwafanya wawe na uzoefu wa kuajiriwa. (Makofi)