Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, ufaulu wa wanafunzi katika maomo ya Sayansi na hisabati yanaonekana kushuka kila mwaka, mathalani mwaka 2015 asilimia 85 ya wanafunzi walifeli somo la hisabati matokeo ya kidato cha nne. Aidha, katika masomo mengine ya Kemia, Fizikia na Biolojia ufaulu bado ni duni sana. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuinusuru Halmashauri ya Mji wa Tarime na janga hili la ufulu duni katika masomo ya sayasi? (b) Je, nini mkakati wa Serikali katika kuiwezesha maabara za shule za sekondari zilizojengwa kwa nguvu kubwa ya wananchi ndani ya Jimbo la Tarime mjini kuweza kupata wataalam na vifaa vya maabara ili kuinuka ufaulu kwenye masomo ya Sayansi?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nisikitike kwa majibu ya Serikali ambayo yametolewa na Naibu na Waziri sasa hivi Serikali ya Awamu ya Tano tunasema tunaelekea kwenye Tanzania ya Viwanda na kwa kasi kubwa sana ununuzi wa ndege ambao tuahitaji pilot na Ma-engeneer, mnajenga SGR, stiegler’s gorge zote zitahitaji wataalam.

Mheshimiwa Naibu Spika, haya majibu hayatoi uhalisia ni mwezi Mei mwaka huu tumepewa mwalimu mmoja wa sayansi sasa kama Mheshimiwa Naibu Waziri anazungumzia walimu toka Tanzania tupate uhuru kweli tunao walimu 59, na upungufu ni mkubwa. Maswali yangu sasa.

Ningependa kujua katika sekondari tisa ambazo zipo ndani mji wa Tarime ni sekondari mbili ambayo ni High School ya Tarime na sekondari ya Mogabili ndio maabara zimekamilika sekondari saba zote maabara hazikamilia majengo ni yale ambao wananchi wamejenga na kwa kufanya hivi inazorotesha ufaulu wa wanafunzi. Ningependa kujua Serikali ni lini mtaleta fedha ili tuweze kukamilisha maabara ya hizi sekondari saba ambazo hazijakamilika zikisubiri Serikali ikamilishe pamoja na vifaa?

Katika Halmashauri ya Mji wa Tarime tuna sekondari moja tu A-Level na kama unavyojua kwamba tuna sekondari tisa. Wanapomaliza form four wanafunzi wetu wengi na hasa wasichana wanashindwa kupata nafasi kuendelea na high school. Ni lini sasa Serikali itapandisha hadhi walau Mogabili Sekondari au Nyandoto kuwa A-level nayo ili kuchukua wanafunzi mchanganyiko kwa maana wavulana na wasichana ili watoto wetu wa kike waweze kwenda High School?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upole kabisa haya ndio majibu ya Serikali, yeye Mheshimiwa Esther kama ana majibu yake nadhani abaki nayo. Majibu ya Serikali majibu haya yanaandaliwa kutoka Halmashauri ya Tarime. Hakuna taarifa za uwongo ambazo zinatolewa hapa mbele ya Bunge letu Tukufu na ndio taarifa ya hali halisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili suala la kupeleka walimu na kupeleka vifaa vya maabara haliwezi kabisa kulinganishwa na miradi mingine ya maendeleo kwa sababu kila kitu kinajitegemea na vyote ni muhimu sana na vinafanyika sambamba. Tumeajiri walimu awamu hii ya juzi 4500 ndio imepata walimu wachache, awamu iliyopita walimu walipelekwa Tarime lakini bahati nzuri na mimi nimefika wanazungumza ukifika Tarime pale tunazungumza.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala shule kupandishwa hadhi Waheshimiwa Wabunge mnafahamu ni suala la mchakato ni lazima ninyi wenyewe kama Mbunge wa eneo husika kupitia halmashauri yako kupitia vikao vya halmashauri kamati ya fedha, bajeti ya ndani na wadau mbalimbali ikiwepo na mfuko wako wa jimbo mleta maoni TAMISEMI Wabunge walioleta maoni yakupandishwa shule zao kuwa high school yanafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ninaomba nitoe taarifa kuanzia mwezi mwaka huu tuna shule nyingi zinaanzishwa ambao tumepata maoni kutoka kwa Wabunge wenyewe kwa vyanzo vya ndani tumpelekee Serikali na walimu tunawapeleka katika maeneo hayo. Ahsante.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, ufaulu wa wanafunzi katika maomo ya Sayansi na hisabati yanaonekana kushuka kila mwaka, mathalani mwaka 2015 asilimia 85 ya wanafunzi walifeli somo la hisabati matokeo ya kidato cha nne. Aidha, katika masomo mengine ya Kemia, Fizikia na Biolojia ufaulu bado ni duni sana. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuinusuru Halmashauri ya Mji wa Tarime na janga hili la ufulu duni katika masomo ya sayasi? (b) Je, nini mkakati wa Serikali katika kuiwezesha maabara za shule za sekondari zilizojengwa kwa nguvu kubwa ya wananchi ndani ya Jimbo la Tarime mjini kuweza kupata wataalam na vifaa vya maabara ili kuinuka ufaulu kwenye masomo ya Sayansi?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya Tarime ni matatizo ya nchi nzima. Na utakubaliana nami kutokana na matatizo maabara ndio maana wanafunzi wengi wanapofika kidato cha pili majority wana-opt kwenda masomo ya Arts kutokana na upungufu mkubwa wa maabara lakini vile vile upungufu mkubwa wa walimu wa sayansi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri anapojibu hapo anasema kwamba wametenga takribani bilioni 59 mara nyingi fedha hizo tunatambua zinaenda walau nusu. Sasa nilitaka kujua Serikali ina mkakati gani mahususi katika miaka hii inayobakia mpaka tunapoenda kwenye Bunge la mwisho kuhakikisha kwamba wanatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maabara ili wanafunzi wetu wa opit kwenda masomo ya sayansi ili waendane na Tanzania ya viwanda.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, labda nitoe taarfa kwamba hapa tulipo sasa hivi tumepata shilingi bilioni 16.6 na tumeshaomba taarifa labda hili nisema inawezekana kuna tatizo la mawasiliano tukiomba maabara ambazo zimekamilika tunaomba kwa maafisa wetu wa elimu kuhamia mikoa na wilaya. Tumeshapata taarifa mbalimbali za halmashauri zote nchini. Mchakato unaendelea kupeleka vifaa tulitaja juzi hapa kwenye bajeti zaidi ya maabara 2500 nchi hii watapata vifaa vya maabara mpya.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini fedha inayozungumzwa hapa kwenye bajeti hii inazungumzia 2019/ 2020 ndio inayozungumzwa hapa. Lakini tunazingatia maeneo lakini tumeeomba taarifa kama kuna maabara zimekamilika tupate taarifa zao. Lakini kuna halmashauri zinatofautiana kutoka moja kwenda nyingine na tunaanza kama tunapeleka vifaa au wataalamu wa maabara au walimu wa sayansi tunapeleka mahali ambapo kuna changamoto kubwa zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tukipata taarifa zile labda niwaelekeze Waheshimiwa Wakurugenzi tunapoomba Taarifa kupitia Maafisa Elimu wa Mikoa, Msingi na Sekondari na Walimu, ni lazima wale watoe taarifa lakini pia na Waheshimiwa Wabunge mshirikishwe, maana yake tumepata kweli taarifa hapa hata ya maboma, ikaonekana tunapata taarifa ambazo ni old fashion Mbunge ana taarifa zake, na Mkurugenzi ameleta taarifa hapa zinatofautiana, ndiyo picha. Lakini, tukiomba taarifa ya Elimu au ya Afya au huduma nyingine kwenye halmashauri zetu, basi Wakurugenzi na Makatibu Tawala kabla ya kuleta taarifa kwenye Ofisi Kuu za Serikali wawasiliane na Waheshimiwa Wabunge ili wote tuwe kwenye line moja na tuweze kuzungumza lugha moja. Ahsante. (Makofi)

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Mheshimiwa Naibu Spika, ufaulu wa wanafunzi katika maomo ya Sayansi na hisabati yanaonekana kushuka kila mwaka, mathalani mwaka 2015 asilimia 85 ya wanafunzi walifeli somo la hisabati matokeo ya kidato cha nne. Aidha, katika masomo mengine ya Kemia, Fizikia na Biolojia ufaulu bado ni duni sana. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuinusuru Halmashauri ya Mji wa Tarime na janga hili la ufulu duni katika masomo ya sayasi? (b) Je, nini mkakati wa Serikali katika kuiwezesha maabara za shule za sekondari zilizojengwa kwa nguvu kubwa ya wananchi ndani ya Jimbo la Tarime mjini kuweza kupata wataalam na vifaa vya maabara ili kuinuka ufaulu kwenye masomo ya Sayansi?

Supplementary Question 3

MHE. SHAABAN O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona, kutofaulu kwa wanafunzi hasa wa masomo ya sayansi kuna changiwa sana na kutomalizika kwa maabara, Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za kutosha katika maabara hizi ili ziweze kumalizika hasa katika Jimbo la Lushoto? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, na anajua nimetembelea kwenye Jimbo lake, na anafanya kazi kubwa sana kuwasemea wananchi wake, na wananchi wa Lushoto wamejenga Shule nyingi ikiwepo shule ya high school, na nilienda akaniambia kuna upungufu wa Walimu, na namuahidi kwamba tulipomaliza kugawa mgao wa Walimu hawa wa Sekondari naye amepata mgao, na hili tumelipokea, vifaa ambavyo tumeelekeza, kama ile Shule ambayo nilitembelea ilikuwa na changamoto kubwa ya watoto wa kike wengi hawajapata vifaa ambavyo vya kuwasaidia ili waweze kusoma masomo ya sayansi. Ahsante.