Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuza:- Je, ni lini Serikali itaifanya Halmashauri ya Itigi kuwa Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa fursa hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza, majibu haya Serikali ni mazuri na yana dhamira njema ya kuijenga nchi hii ifikie katika malengo mazuri. Lakini kuna majibu ya swali kama hili ambao niliuliza mwaka 2016 kama 2016/2017 na bahati nzuri kwenye hansard ninalo lilipata majibu ambao yalionyesha matumaini kwamba kuna siku Halmashauri ya Itigi inaweza kuwa Wilaya. Lakini kwa kuwa Halmashauri ya Itigi ni engeo ambao lina ukubwa wa Squire kilometa 17,000 ni sawa sawa baadhi ya mikoa ambao ipo katika nchi hii na ni tarafa moja.

Je, sasa Serikali ipo tayari kuwa tuachane na suala la kuongeza Wilaya tuondoe walau tuongeze tarafa ambazo hazitakuwa na ghamara kubwa za uendeshaji ikiwemo ofisi ya Wakuu na nini au madiwani?

La pili, katika eneo langu kuna kijiji kinaitwa Mitungu ambacho nacho kina eneo kubwa ukubwa wa eneo ni mkubwa sana lakini wananchi ni wengi. Kutoka katikati ya kijiji mpaka pembeni ni kilometa 40 upande mmoja na upande wa pili hivyo hivyo.

Je, Serikali iko tayari kufanya kazi nzuri kama nazofanya Mheshimiwa Dkt. Medard Kalemani ambaye anatamka jambo na linafanyiwa kazi na haraka unapata matokeo. Je, kwenye kijiji hiki kimoja tu ambacho tunataka kugawanywa angalu kupata vijiji viwili kina watu zaidi elfu 30 Serikali ipo tayari angalu kusaidia na kunipa uwezekano wa mwaka 2020 kuona wepesi katika eneo hili?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Mbunge tunakusudia na kutengependa apate wepesi mwaka 2020 na kwa kazi nzuri anayoifanya kuwasemea wananchi wake wa Manyoni tunaamini kwamba wataendelea kumwani na kumunga mkono.

Mheshimiwa Naibu Spika, ameuliza maswali mawili ya nyongeza kwa uchungu na akionyesha ukubwa wa nchi ulivyo na ameonyesha namna ambavyo alishapata majibu ya matumaini hapa Serikali inafanya tathimini kutoka mwaka hadi mwaka. Baada ya kufanya tathimini ya kuangalia maeneo ambayo bado yanazidi kuimarishwa kwa maana ya Ofisi na vitendea kazi vingine miradi ya maendeleo iliyopo na uwezo wa Serikali ndio maana tukaja na jibu la namna hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo amezungumza hapa kwanza maeneo haya yanafanya uchanguzi kwa mfano vijiji vya mwaka huu tayari timu yetu imeshatembelea maeneo mbalimbali kuangalia maeneo ya migoro mahali ambapo ilikubadilisha GN wameshafanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tulipokee hili tuendelee kushauliana tuone kama haitaingiza gharama kubwa Serikalini. Kama ambavyo tunajua tukiongeza maeneo itakauwa gharama zaidi tutaona namna ambavyo kama kuna wepesi wa kuifanya ile kazi ili hawa wananchi waweze kupata huduma karibu. Lakini nawaomba waendelee kuwahimiza nia ya Serikali ni njema sana na Wabunge watakubaliana na sisi kwamba kwa kweli kama unaanzisha maeneo mapya na kati ya hapa kuna watu ambao wadai ofisi za mikoa kuna ofisi za wilaya, Ofisi za Wabunge, Ofisi za kata vijiji na mitaa kwa kweli ukiangalia huo ukubwa na wingi wa shughuli hiyo unahitaji tutulie kuimalisha maeneo ambayo kweli tunayo sasa ili tuweze kuongeza baadaye ahsante.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuza:- Je, ni lini Serikali itaifanya Halmashauri ya Itigi kuwa Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Pamoja na kutambua nia njema ya Serikali katika kusitisha kuongeza maeneno mengine mapya ya utawala hasa kwa maeneo ya mikoa na wilaya na halmshauri ambazo pengine gharama ya kuanzisha ni kubwa lakini kule chini kwenye kata na vijiji na mitaa hali ni mbaya sana na gharama yake sio kubwa kiasi hicho, badala kuyabeba yote pamoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Serikali kwa nini isifikirie hasa tunapokwenda kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa kwenye mitaa, kwenye kata na vijiji kwenda kuongeza maeneo ya kiutawala kwa sababu hali halisi inakataana na huo msimamo wa Serikali?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema ni kweli kuwa tunaangalia gharama ni kubwa lakini naomba nikubaliane na maoni ya Wabunge walio wengi humu kwamba tuangalie kama nilivyomjibu Mheshimiwa Massare tuangalie kama kuna maeneo ambayo hatutakuwa na gharama kubwa tuyazingatie.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu lengo la Serikali nikusogeza huduma karibu na wananchi na kuna maeneo kwa kweli wanatembea km 40, 30 kwenda kuomba barua ya mtendaji wa kata kitendo ambacho sio sawa sawa. Kwa hiyo, tulipokee hili kwa niaba ya Bunge hili Tukufu na kwa niaba ya Serikali tumelifanyia kazi kwa pamoja na tutashirikisha Wabunge wa maeneo husika namna kuweza kulifanya hili kutekelezeka. Ahsante.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuza:- Je, ni lini Serikali itaifanya Halmashauri ya Itigi kuwa Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo Naibu Waziri amesema kwamba swali hili liliulizwa kuhusu Tanga wiki iliyopita ningependa kujua Mkoa ambao una halmashauri 11 na tunaposema pamoja na kupeleka maendeleo karibu na wananchi lakini lengo haswa ni kuboresha huduma. Huoni kama ni mzigo kubwa sana kwa mkoa mmoja kuwa na halmashauri nyinigi wakati baadhi ya mikoa halmashuri zake hazizidi nne hadi tano?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri nimewahi kuwa katibu wa vijana wa Chama cha Mapinduzi wa Mkoa wa Tanga, nina zifahamu halmashauri 11 na ukiangalia jiografia kwenda mpaka kule kilindi mpaka Tanga kule Nkinga ni jiografia kubwa. Lakini tunajua kuna mikoa mingine pia ni mikubwa sana ukiangalia kwa mfano Lindi, Ruvuma kule kwa kweli kuna maeneo makubwa sana kiuongozi labda kwa jibu la jumla tu ni kwamba msimamo wa Serikali ni kwamba kwa gharama iliyopo kama ilivyotajwa kwenye REA ujenzi wa miundombinu ya mkoa na wilaya ni kubwa sana ni mabilioni ya fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tulipokee tushauriane ndani ya Serikali tuone kama tunaweza kulifanya kesi by kesi kulingana na ukubwa wa eneo hili tuone kama tunaweza kulifanyika kazi kwa sasa siwezi kuahidi kama tutafanya kesho. Tunaona ile ku-concern ya huduma karibu na wananchi jiografia yetu kubwa mikoa ni mikubwa lakini tulipokee kama maoni ya Wabunge tuendelee kuyafanyia kazi wakati ambapo ikiwa wakati muafaka hili litatekelezwa. Lakini hayo ndio majibu ya Serikali kwa sasa.