Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN aliuliza:- Utalii wa Baharini kupitia “diving” unakua kwa kasi sana Duniani kote hali ambayo inaongeza soko la ajira katika sekta hiyo. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na changamoto za soko la ajira kwa vijana wa Kitanzania? (b) Je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha usalama wa watalii wanapokuwa chini ya maji hasa kutokana na uvuvi haramu wa kutumia mabomu?

Supplementary Question 1

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawli ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, ametaja vituo vya Mafia, Dar es Salaam na Tanga ambavyo vinatoa mafunzo ya elimu hii; nilikuwa nataka kujua vinatoa mafunzo kwa kiwango gani? Wanatoka Ma-diving instructor, diver masters au wanafunzi wa kiwango gani wanaotoka katika vituo hivyo vya kufundishia?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; siyo tu kwamba ile mitetemo wanapolipua wale wavuvi inawatisha na inawasumbua wale Ma-divers wanapokuwa chini ya maji lakini pia eneo ambalo limepigwa lile bomu huwa linaathirika sana na kupoteza ule uhalisia wake kiasi kwamba mpaka rangi ya eneo lile huwa inabadilika. Je, Serikali ina mpango wowote wa kufanya utafiti kuona ule uoto wa asili unarudi pale yale Matumbawe yaliyoharibiwa kwa muda wa miaka mingapi?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, kimsingi kwa mujibu wa swali lake la kwanza, mpaka sasa hatuna vyuo ambavyo vinatoa vyeti maalum lakini tuna vituo ambavyo vinatoa mafunzo kwa ajili ya kusindikiza watalii wanaokuja kwa ajili ya uzamiaji. Katika vyuo vyetu vyote vya Mbegani na wapi hatuna certificate maalum kwa ajili ya divers au snorkel au nini ambayo inatolewa katika maeneo hayo. Wanapata uzoefu kutokana na wale ambao wamekuwa waki-practice kwa muda mrefu kwahiyo vituo hivyo ndiyo nimevitaja katika jibu langu la msingi.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili amesema kuna utafiti gani unafanyika kujua athari zinzaotokana na ulipuzi; ni kweli kwamba milipuko inapolipuka ndani ya maji uharibu kabisa maumbile ya Dunia ndani maji na hasa Matumbawe ambayo ndiyo kivutio kikubwa cha wazamiaji na maeneo yote baharini na kimsingi maeneo haya ambayo yamekuwa ukifanyika uzamiaji yamekuwa ni maeneo yanayolindwa na kwa mfano, ukienda kule Mafia kuna kikosi maalum ambacho kinalinda maeneo hayo na kina patrol maalum. Kwa hiyo, uzoefu wa maeneo hayo kushambuliwa na wazamiaji haupo, kwa hiyo nimuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika maeneo ambapo tunapeleka watalii kwa ajili ya shughuli hii ni maeneo ambayo yanalindwa na kusimamiwa vizuri na hakuna uwezekano wa matumizi ya mabomu.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba tena ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kuongezea kujibu swali la Mheshimiwa la Mheshimiwa Yussuf kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza vilevile Mvuvi mwenzangu Mheshimiwa Kanyasu kwa majibu yake yale ya awali. Lakini pia nieleze tu kuwa katika chuo Kikuu cha Dar es Saalam katika kozi ya Aquatic Science moja ya jambo la msingi kabisa kwenye kozi ile watu wanafundishwa kitu kinachoitwa swimming and snorkeling.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, swimming and snorkeling mtu anayekwenda kupata shahada ya swimming mathalani mimi mwenyewe hapa ni lazima unafundishwa namna ya kuweza kuogelea na kuweza kuingia kwenye maji kwa muda mrefu na ndipo upate degree yako. Lakini kama haitoshi alivyosema Mheshimiwa Kanyasu kuwa Ndegani wanao utaratibu ambao wanashirikiana hasa na Mamlaka ya Bahari Kuu ambapo wanafundishwa pale kwa muda mfupi nakupewa udhoefu. Wataalam wetu ambao wanakwenda kuwa observer’s watazamaji katika meli hawa pia wanafundishwa namna hata ya ku-dive.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili la Matumbawe ni conservation, Matumbawe yanachukua si pungufu ya miaka 50 hadi 100 yale ambayo yamevunjwa na mabomu, kwa hivyo kitu pekee ambacho sisi wataalam wa Sayansi ya Majini tunachokifanya ni kuhakikisha kuwa maeneo yaliyoharibiwa namna hiyo yanakwenda kuhifadhiwa tumefanya jitihada kubwa kwa kupitia mradi wetu mkubwa unaitwa sea offish ukanda wa Pwani ambapo kuanzia Tanga kule MOA mpaka Mtwara maeneo ya Mtwara mwishoni kule tumekuwa na huo mradi ambao tunadhibiti na kuyalinda maeneo yetu ya miamba na tumeonesha mafanikio makubwa sana katika Wilaya ya Kilwa, hivi sasa hata mazao yanayopatikana katika miamba ile kwa maana ya Matumbawe yameongezeka kwa kiasi kikubwa sana.