Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA (K.n.y. MHE. GRACE V. TENDEGA) aliuliza:- Walimu wenye weledi wa kuwafundisha Watu Wenye Ulemavu ni wachache sana nchini. Je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha Walimu hao ni wa kutosha?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimimiwa Spika, ahsante, kwanza nipongeze nchi za Scandinavia zilikuwa zikisaidia sana Serikali yetu kupeleka Walimu wa mahitaji maalum kwa muda wa miaka mingi, swali langu la kwanza.

Je, ni lini Serikali itaongeza nguvu ya kipesa kuweza kuwadahili wanafunzi wengi zaidi watakaosomea mafunzo ya alama?

Mheshimimiwa Spika, swali la pili katika Wilaya ya Rungwe kuna shule ya watu wenye ulemavu ya Katumba ambayo ina miundombinu iliyochakaa kwa muda mrefu na ina Walimu wachache wa lugha za alama pamoja na lugha za watu wenye ulemavu, Serikali itatia jitihada gani kuweza kusaidia shule hii ya Katumba kupata mahitaji hayo? Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimimiwa Spika, ni kwamba suala la watu Wenye Ulemavu ni muhimu sana na Serikali inatambua na kulipa
kipaumbele. Katika kuhakikisha kwamba kunakuwa na wanafunzi wengi wanaoweza kujifunza lugha ya alama kwa sababu haitoshi tu kila mtu kuongea anavyoelewa ni vizuri kukawa na lugha ambayo kwa yoyote utakayemkuta anaongea lugha ya alama itakuwa ni hiyo hiyo. Wizara tayari ilishashughulikia na kuna vitabu ambavyo vimeshatayarishwa ambavyo vinaweza kuwafundisha watu wengi tukiacha wanafunzi hawa wazazi waweze kuifahamu lugha ya alama.

Mheshimimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuwezeshwa suala hilo. Na kwa upande wa shule ambayo imezungumzwa ya Katumba niseme tu kwamba kwa suala la Watu Wenye Ulemavu hilo ni suala muhimu kwa sababu Tanzania inahitaji kuona kwamba wananchi wote wanafaidika na elimu, iwe mlemavu, iwe asiye mlemavu. Kwa misingi hiyo nikuombe tu Mheshimiwa nitaona kwamba kuna umuhimu wa kutembelea shule hiyo ili iweze kusaidiwa inavyotakiwa.