Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dunstan Luka Kitandula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkinga
Primary Question
MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji kutoka chanzo cha Mto Zigi kwenda Mkinga na Horohoro utaanza?
Supplementary Question 1
MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, na kama ulivyosema, ni kweli kwamba swali hili ni la muda mrefu. Kwa kuwa wananchi wa Mkinga wanazo taarifa kwamba mtaalam huyu amekwishapatikana tangu mwezi Novemba, na ilikuwa waingie mikataba lakini yakawa yanafanyika majadiliano yaliyokuwa na lengo la kupunguza scope ya kazi kwa vijiji vile 37, jambo ambalo limeleta taharuki. Je, Waziri yuko tayari kutuhakikishia kwamba hayo majadiliano hayatapunguza wigo ambao utawahakikishia wananchi wa Mkinga vijiji vile 37 vyote vipate maji? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa mradi wa Horohoro umepigiwa kelele sana kwa muda mrefu na sasa unakwenda kutimia, kutekelezwa, na mwezi wa sita sio mbali. Je, Waziri yupo tayari mwezi wa sita utakapofika atoe ahadi kwamba ataandamana na mimi kwenda kuweka msingi wa kuanza ujenzi wa mradi ule kwa wakati?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kiukweli nitumia nafasi hii, dhati ya moyo wangu kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, amekuwa mfuatiliaji mkubwa sana si kuchangia tu Bungeni lakini hata ofisini amekuwa akija mara kwa mara kuhusu suala zima la mradi huo.
Mheshimiwa Spika, sisi kama viongozi wa Wizara tulikwishasema kwamba hatutakuwa kikwazo kwenye utekelezaji wa miradi ya maji. Wakati mwingine tunatumia muda mrefu sana kwa kuwatumia wakandarasi wetu, sisi kama viongozi tumejadiliana tumeona haja sasa kazi zile zifanywe na wataalam wetu wa ndani ili kuhakikisha kwamba hii kazi inafanyika kwa haraka na wananchi wake waweze kupata maji safi na salama katika kuhakikisha kwamba tunamtua mama ndoo kichwani.
Name
Hussein Nassor Amar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nyang'hwale
Primary Question
MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji kutoka chanzo cha Mto Zigi kwenda Mkinga na Horohoro utaanza?
Supplementary Question 2
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa wakandarasi wa Wilaya ya Nyang’wale wamekuwa wakiuchezea ule mradi na kuchukua muda mrefu na fedha ya Serikali kupotena na juzi Mheshimiwa Naibu Waziri umefanya ziara ukajionea mwenyewe. Je, Serikali inawachukulia hatua gani ya haraka hao wakandarasi?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, nipende kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya ambayo nimejionea mimi kwa macho nilipoenda hapo Nyang’wale, lakini kikubwa tulikuwa tunatabua kabisa na Waheshimiwa Wabunge wamelalamika sana, hususan utekelezaji wa miradi ya maji vijijini, imekuwa na changamoto kubwa sana na ndiyo maana sisi kama Wizara ya Maji tukaleta Muswada wa kuhakikisha kwamba tunakuwa na Wakala wa Maji Viijini.
Mheshimiwa Spika, tunalishukuru Bunge lako Tukufu kwamba limetupitishia haraka na Mheshimiwa Rais ameshatusainia ule Muswada na sasa ni Sheria. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Viongozi wa Wizara ya Maji, hakutokuwa na Mkandarasi ambaye atashindana na sisi, sisi tumejipanga vizuri, mkandarasi yeyote mbabaishaji ama awe mtalaam, kwa maana ya Mhandisi wa Maji, tutamchukulia hatua haraka iwezekanavyo katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma hii muhimu ya maji.
Name
Oliver Daniel Semuguruka
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa maji kutoka chanzo cha Mto Zigi kwenda Mkinga na Horohoro utaanza?
Supplementary Question 3
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Swali lililoulizwa namba 256 linafanana kabisa na changamoto iliyopo Wilaya ya Ngara katika mradi wa Muhweza, ni miongoni mwa vijiji 10, lakini mradi huu umechukua muda mrefu sana bila kukamilika. Je, ni lini mradi huu utakamilika ili kuwatua ndoo kina mama?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, napenda kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge, dada yangu Mheshimiwa Oliver amekuwa mpambanaji mahili katika kuhakikisha kuwapigania wananchi wa Kagera ili waweze kupata huduma hii muhimu ya maji. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini, kutokana na swali lake nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge, nimelipokea na nilifuatilie kwa haraka na tuweze kuongeza nguzu zetu ili mradi huo uweze kukamilika na wananchi waweze kupata huduma hii muhimu.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved