Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:- Tangu Wilaya ya Kilolo ipate hadhi ya kuwa wilaya mwaka 2002 Serikali haijaweza kujenga ofisi za polisi na nyumba za kuishi yalipo Makao Makuu ya Wilaya:- Je, ni lini Serikali itajenga ofisi na nyumba hizo za polisi Wilaya ya Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali ya nyongeza na nishukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa umbali yalipo mahabusu, Ofisi ya OCD, karibu kilometa 70 mpaka yalipo Makao Makuu ya Kilolo, hivi Serikali inatumia gharama kubwa sana kusafirisha mahabusu, kumsafirisha OCD na askari kwenda yalipo Makao Makuu. Je, Serikali huwa inaangalia tathmini ya gharama inazozitumia kwa kuchelewesha kujenga hizi Ofisi za Wilaya.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa nyumba za polisi zilizopo wilaya ya Mufindi, zilizopo FFU Kihesa na Central line polisi Iringa Mjini ni nyumba ambazo kwakweli ni chakavu mno, vyo haviingiliki, askari wetu wamekuwa wakiishi familia 5 chumba kimoja na kuna adha nyingi sana ambazo wanazipata hata watoto na kinamama ambao wanaishi katika zile nyumba.

Mheshimiwa Spika, nimuombe Mheshimiwa Waziri anipe siku, tarehe na mwezi ambao tutakwenda kukagua nyumba zote za Mkoa wa Iringa na kubwa ambazo wamekuwa wakizipata askari wetu walioko katika Mkoa Iringa, ili mwenyewe ajionee na aone jinsi gani ambavyo pamoja na ufinyu wa bajeti yeye mwenyewe ataona kwamba iko haja sasa haya majengo ya Askari au nyumba za askari ziweze kukarabatiwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza kwa dhati ya moyo wangu Mheshimiwa Ritta Kabati, kwa jinsi ambavyo amekuwa akitetea sana Jeshi letu la Polisi katika Mkoa wa Iringi, lakini siyo kwamba amekuwa akitetea kwa maneno, ni miongoni mwa Wabunge ambao wameshiriki kikamilifu katika kuhakikisha kwamba wanapunguza changamoto za Askari wetu kwa yeye mwenyewe kujitolea kujenga kituo cha polisi kilichopo eneo la Semsema.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, baada ya pongezi hizi, Mheshimiwa Rita Kabati na jitihada kubwa ambazo tunaziona anazozifanya katika kupigania polisi, nimhakikishie kwamba tutaambatana mimi na yeye kwa ruhusu ya Mheshimwa Spika, ili twende tukashirikiane kwa pamoja kubabiliana na changamoto ambazo amezizungumza. Hata hivyo, nataka nimhakikishie kwamba tayari Serikali imeshaanza jitihada. Kwa mfano hivi tunavyozungumza kuna ujenzi wa nyumba sita unaendelea kwenye Makao Makuu ya FFU pale Iringa ni kuonesha kuguswa na upungufu na uchakavu wa nyumba za Askari katika Mkoa wa Iringa.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tayari kuna eneo ambalo tumelibaini kwa ajili ya ujenzi wa kituo kwa baadaye kwenye wilaya yake, tukitambua kwamba kuna umuhimu wa Makao Makuu ya Polisi ya Wilaya kuwa katika Makao Makuu ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nadhani nimeshamjibu maswali yake mawili ya nyongeza kwa pamoja.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:- Tangu Wilaya ya Kilolo ipate hadhi ya kuwa wilaya mwaka 2002 Serikali haijaweza kujenga ofisi za polisi na nyumba za kuishi yalipo Makao Makuu ya Wilaya:- Je, ni lini Serikali itajenga ofisi na nyumba hizo za polisi Wilaya ya Kilolo?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa hii nafasi. Kwa kuwa swali limekuwa likijirudia kila mara na majibu ambayo yanatofautiana, sasa niombe, tu kwa kuwa umbali huo ni mrefu na gari hakuna, Serikali itakuwa tayari sasa kutoa gari na kuongeza mafuta kwa ajili ya kwenda Kilolo na kurudi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, tutakuwa tayari kupeleka gari Kilolo pale ambapo fedha zitakapopatikana.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:- Tangu Wilaya ya Kilolo ipate hadhi ya kuwa wilaya mwaka 2002 Serikali haijaweza kujenga ofisi za polisi na nyumba za kuishi yalipo Makao Makuu ya Wilaya:- Je, ni lini Serikali itajenga ofisi na nyumba hizo za polisi Wilaya ya Kilolo?

Supplementary Question 3

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kama inavyofahamika, kituo cha Polisi katika Wilaya ya Lushoto ni cha tangia Mkoloni, lakini
nashukuru Serikali imetutengea fedha tumejenga kituo cha Polisi lakini kituo kile mpaka sasa hivi takribani miaka mitano sasa kiko kwenye mtambao wa panya. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia kituo kile?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Lushoto kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa lugha ambayo ameitumia kidogo imenipa utata kuielewa…

SPIKA: Iko kwenye leta.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Ameseama mtambaa wa panya…

SPIKA: Iko kwenye lenta, pale, wanaita mtambaa wa panya.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, sawa sawa. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo amependekeza, tutakweda mimi na yeye kuangalia nini cha kufanya ili sasa tuvuke hapo mtandaa panya kuelekea kwenye kukimaliza kitu hicho.

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:- Tangu Wilaya ya Kilolo ipate hadhi ya kuwa wilaya mwaka 2002 Serikali haijaweza kujenga ofisi za polisi na nyumba za kuishi yalipo Makao Makuu ya Wilaya:- Je, ni lini Serikali itajenga ofisi na nyumba hizo za polisi Wilaya ya Kilolo?

Supplementary Question 4

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, katika majibu yake ya msingi Mheshimiwa Naibu Waziri aliesema kwamba kwa upande wa wilaya mpya, Serikali inatafuta fedha ili iongeze bajeti kwa ajiliya ujenzi. Sasa Wilaya yetu ya Ubungo ni Wilaya mpya na Serikali kupitia Serikali, nguvu za wananchi na Mfuko wa Jimbo, tumejega kituo cha polisi cha wilaya pale Gogoni.

Mheshimiwa Spika, sasa kituo kile cha polisi ni kituo kikubwa, lakini huduma zinakuwa finyu kwa sababu Askari wanatoka maeneo ya mbalimbali sana. Sasa je, Serikali iko tayari, katika kutafuta fedha za ujenzi, itafute vilevile fedha za kujenga nyumba za Askari katika Jimbo la Kibamba karibu na Kituo cha Polisi cha Gogoni?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza naye nimpongeze kwa jitihada zake kama alivyozungumza, kwamba kupitia Mfuko wake wa Jimbo na nguvu za wananchi wameweza kujenga hicho kituo. Nikijibu swali lake ni kwamba, tutakuwa tayari, pale ambapo fedha zikipatikana basi tutashirikiana naye katika kumaliza ujenzi wa nyumba iki kituo hicho kiweze kutumika masaa yote.