Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Jimbo la Tunduru Kusini limepakana na Msumbiji kupitia Mto Ruvuma kuanzia mpaka wa Wilaya ya Nanyumbu na Wilaya ya Namtumbo:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua barabara ya ulinzi inayounganisha mikoa yote ya Kusini yaani Mtwara na Ruvuma?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Barabara ya Mitema Upinde kwenda Msinji iliyopo upande wa Tunduru ni sehemu ya barabara hiyo ya ulinzi katika upande wa mto Ruvuma. Barabara hiyo ilitolewa madaraja yake wakati wa vita vya Nduli Iddi Amin, na tangu yametolewa madaraja yale mpaka leo bado hayajaweza kurudishwa. Ni lini Serikali itarudisha madaraja yale ili barabara hiyo iweze kupitika kwa urahisi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Barabara ya Tunduru na Masakata Liwanga mpaka Misechela ni barabara ya ulinzi ambayo inaunganisha Msumbiji na Tanzania kupitia katika Kijiji cha Misechela. Je, Serikali haioni haja ya kukichukua kipande hicho kiwe Barabara ya Mkoa kwa sababu mchakato wote wa kufanya barabara hiyo ichukuliwe na TANROADS ulishafanyika kwa ngazi ya Mkoa? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, anafuatilia sana hususani mtandao wa barabara katika maeneo yake. Niseme tu kwamba hii barabara ya Itema Msinji ilitolea madaraja. Utaratibu wa kwetu kawaida ni kwamba madaraja yaliyowekwa kwa wakati wa dharura huwa tunayatoa na kuyahifadhi kama asset; pale ambapo itahitajika sasa kuyaweka madaraja haya sehemu zingine tutaenda kuyaweka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa hiyo nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge nielekeze tu wataalamu waangalie maeneo haya kama yanastahili kurudishia madaraja haya yaliyotolewa tutafanya utaratibu huo, lakini kama tutakuwa na mahitaji ya kujenga upya maeneo hayo ili kutoa huduma nzuri kwa wananchi pia tutafanya hivyo. Kwa hiyo nielekeze tu TANROADS Mkoa wa Ruvuma waangalie sehemu hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme tu kwamba tunafanya upembuzi yakinifu wa barabara hii kutoka Mtwara – Pachani – Lusewa – Ligusenguse kwenda Nalasi (km 211), na tumetenga fedha za kutosha. Kwa hiyo wakati wa zoezi hili la kutambua changamoto zilizoko katika maeneo haya pia tutatazama kwa macho mawili maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu barabara hii ya Misechela kuwa Barabara ya Mkoa tumeanzisha chombo hiki cha TARURA. Sisi juhudi zetu ni kuhakikisha TARURA inapata fedha za kutosha, lakini kama kutakuwa na mahitaji mahsusi ya kupandisha Barabara hii tutaiangalia kwa nia hiyo ambayo Mheshimiwa Mbunge umeomba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.