Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali kwanza tunashukuru kwamba, wameweza kutupatia gari la canter kwa ajili ya kubeba mahabusu katika Wilaya ya Uvinza, lakini tunaomba sasa ni lini Serikali itampatia OCD wa Wilaya ya Uvinza gari la kufanyia patrol kwa sababu kwa kipindi kirefu sana hakuna gari la kwa ajili ya kufanya patrol?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Katika Wilaya ya Lushoto ambayo ndio wilaya kongwe ya kipolisi nchini jengo la utawala ambalo anatumia OCD limesimama kwa muda mrefu sasa na jengo hili linajengwa kwa msaada wa fedha za DFID. Je, ni lini jengo hili la Polisi Wilaya ya Lushoto litakamilika?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na gari la OCD, kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi Uvinza, lipo gari aina ya Land Cruiser ambayo anatumia OCD kwa sasahivi. Ingawa tukipata gari jingine tutaongeza tunatambua umuhimu wa mahitaji ya gari hasa katika Wilaya ya Uvinza na Mkoa wa Kigoma kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na hoja ya kituo cha Polisi ambacho ujenzi wake umesita kule Lushoto; kimsingi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kituo hiki ambacho kilikuwa kinajengwa chini ya ule mradi pesa za ufadhili kutoka mradi wa STAKA pamoja na Serikali, ilisita kwa muda, hata hivyo tumeshafanya tathmini na kugundua kwamba, zinahitajika fedha kwa ajili ya kukamilisha kituo hiki na ninadhani takribani kama shilingi milioni 300 si pesa nyingi. Fedha hizi tunatarajia kuzipata kupitia kwenye mfuko wa Tuzo na Tozo, hivyo tutakapokamilisha kupata fedha hizo tutamaliza kituo hiki kiweze kutumika.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona, pamoja na majibu mazuri ya kwenye swali la msingi la Naibu Waziri, Wilaya ya Korogwe ina Halmashauri mbili ambapo Polisi wanakaa kwenye jengo la mkoloni ambalo Mkuu wa Wilaya yumo, Mahakama imo na hiyo Polisi ipo hapo.

Je, katika mipango ambayo wanakusudia sasa kuanza baadaye atakuwa tayari kuipa kipaumbele Korogwe ili wawe na jengo la ofisi kwa sababu kiwanja wanacho?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi kwamba, tuna upungufu wa vituo vya Polisi katika baadhi ya wilaya nchini na hivyo basi nimhakikishie kwamba, katika mipango ya Serikali ya kujenga vituo hivyo na Korogwe ni moja katika maeneo ambayo tunayatambua hayana kituo na hivyo ni moja katika maeneo ambayo tuna mpangonayo wa kujenga vituo pale ambapo mipango hiyo itakapokamilika, hususan katika eneo la upatikanaji wa fedha.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 3

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi. Swali hili nauliza kwa mara ya tatu leo, kwa kuwa Milima ya Kitonga, Ruaha Mbuyuni mpaka Mikumi Iyovi, Malolo, kituo wanachotegemea cha Polisi ni kimoja cha Ruaha Mbuyuni, lakini hawana gari la Polisi na hivi juzi nimetoa pikipiki mbili kwenye kile kituo. Sasa je, Serikali haini ni wakati muafaka wa kuniunga mkono kwa sababu, accident inapotokea wanapata shida kubwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze kwa kuchangia pikipiki kwa askari wetu, lakini na mimi namjibu tena kwa mara nyingine kwamba, pale ambapo magari yatafika tutaangalia uwezekano wa kuweza kupeleka pale kwa sababu, sasahivi tunavyozungumza hatuna magari ambayo yamepatikana kwa hiyo, avute subira Mheshimiwa Mbunge.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 4

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, kwa kuwa mwaka 2015 mimi mwenyewe niliifadhili Wizara ya Mambo ya Ndani gari la Polisi kutoka Japan, jipya, na nikalipeleka kwenye kituo cha Polisi kilichoko Maore kwa ajili ya Jimbo la Same Mashariki, lakini Serikali mpaka leo mnashindwa kutoa hata pesa kidogo kwa ajili ya kupeleka service gari lile. Waziri unaniambia nini sasa hivi? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunathamini sana jitihada za Mheshimiwa Anna Kilango Malecela za kuweza kutusaidia gari kwa matumizi ya Jimbo la Same. Namhakikishia Mheshimiwa kwamba hatushindwi kufanya service hiyo gari; na kama kuna tatizo la service, basi tumelipokea na tutahakikisha kwamba gari hiyo inafanyiwa service ili iweze kutumika. (Makofi)

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 5

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wilaya ya Ikungi ni Wilaya iliyoanzishwa mwaka 2013; na hivi tunavyoongea, ofisi au OCD anakaa kwenye majengo ambayo yalikuwa ni maghala ya mkoloni. Kwa sababu ulishaanzwa ujenzi wa kujenga jengo la OCD kwa maana ya wilaya, ni lini sasa Serikali itamaliza, kwa sababu limesimama muda mrefu, miaka mitatu iliyopita?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mimi na Mheshimiwa Mtaturu tulishazungumza pembeni kwamba niende Jimboni kwake, nimhakikishie kwamba moja katika mambo ambayo tutafanya ni kwenda kukitembelea kituo hiki kwa pamoja halafu tushauriane juu ya utaratibu muafaka wa kukimaliza kituo hiki kwa haraka.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 6

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa vile Serikali ikishawekeza pesa nyingi kujenga Kituo cha Polisi cha Mkalama; na kwa vile Naibu Waziri alishafika na akakiona kituo hicho sasa kinaanza kuharibika, ni lini kituo hicho kitakamilika?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kituo hiki nakifahamu na tuliambatana na Mheshimiwa Kiula kukitembelea. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kama ambavyo tulizungumza wakati wa ile ziara, nami nimeshawasilisha hiyo taarifa na hivi sasa Serikali ipo katika harakati za kutafuta fedha ili kituo hiki kiweze kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Kiula avute subira wakati Serikali inaendelea na jitihada hizo za kupata fedha za kumaliza Kituo hiki cha Polisi.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 7

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Halmashauri ya Geita DC ina population zaidi ya watu 1,300,000 na tunaye OCD mmoja peke yake ambaye anafanya kazi kwenye Halmashauri hiyo ya watu 1,300,000 plus Geita Mjini yenye watu zaidi ya 600,000.

Je, Waziri ananiambiaje kuhusiana na kutafuta Kanda Maalum Nzela ili kumsaidia OCD wa Geita, kumpunguzia ukubwa wa eneo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, maamuzi ya kutengeneza kanda maalum yanategemea sababu mbalimbali au vigezo mbalimbali ikiwemo ukubwa wa kijiografia, hali ya uhalifu katika eneo husika na kadhalika. Kwa hiyo, sitaki nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaweza kufanya hilo jambo kama ambavyo amependekeza kwa sasa hivi, kwa sababu sina hakika kwamba eneo hilo imekidhi vigezo ambavyo vinahitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunalipokea na tuone, kama imekidhi vigezo na kama hali itaruhusu, basi tutalitafakari na kulitolea maamuzi sahihi kwa wakati muafaka.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. HASNA S. K. MWILIMA) aliuliza:- Wilaya ya Uvinza imeanzishwa tangu mwaka 2002 lakini hadi sasa Jeshi la Polisi katika Wilaya hii halina nyumba za kuishi, Ofisi pamoja na vitendea kazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha vitendea kazi Jeshi la Polisi katika Wilaya hiyo kama vile magari, Ofisi pamoja na makazi?

Supplementary Question 8

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni Wilaya kongwe yenye umri zaidi ya miaka 44 sasa; pamoja na kwamba Halmashauri wametenga eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi, lakini hadi leo Wilaya ya Liwale haina Kituo cha Polisi. Nini kauli ya Serikali namna ya kuwapatia wananchi wa Liwale ujenzi wa Kituo cha Polisi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Kuchauka hiki kimekuwa ni kilio chake cha muda mrefu sasa, lakini nimhakikishie kwamba kilio chake siyo cha peke yake, hata sisi Serikali tuna kilio hicho hicho kuhakikisha kwamba Wilaya ya Liwale kulingana na umuhimu wake inapata Kituo cha Polisi. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba pale ambapo tutaweza kufanikiwa kupata fedha, basi tutajenga hicho Kituo.