Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:- Je, ni lini miradi ya visima vya Waranga, Dumbeta, Endamudagya, Gidika, Murumba na Hirbadaw itakamilika na kuanza kusambaza maji kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri na Waziri kwa kazi iliyofanyika na inayotegemewa kufanywa nilikuwa nauliza kwamba katika visima hivyo vimewekwa nguvu ya solar ili kusukuma maji lakini bahati mbaya Hanan’g ni eneo ambalo muda wote halina jua. Je, wanafanya nini ili usambazaji huo uwe unawasaidia wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na swali la pili ni kwamba wakala wa visima ulijaribu kuchimba visima katika kijiji cha Gidamwai au Basodomi pamoja na kijiji cha Gauloli lakini kwa sababu walileta mashine yenye uwezo mdogo wa kuchimba kwenda chini na Hangan’g iko kwenye Bonde la Ufa. Je, ni lini na Wizara iliahidi kwamba ingeleta mashine hizo kuja kuchimba visima hivyo na wananchi walipewa moyo? Naomba nijue ni lini visima vya wakala mashine zawakala wa visima zitakuja Gauloli pamoja na Basodomi ili kuwachimbia hao watu ambao wamepewa moyo? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Mama yangu Dkt. Mary Nagu kwa kweli ni mwana mama supavu na amekuwa mpiganaji hasa katika Jimbo lake la Hanang’ na namuomba Mwenyezi Mungu mwanangu siku moja awe kama yeye kutokana na kazi kubwa anayoifanya katika Jimbo lake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kikubwa ninachotaka kukisema tumefanya kazi kubwa sana ya kuhakikisha wananchi wanapata maji lakini kama unavyojua utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na uwepo wa nishati lakini eneo lake kule kumekuwa na hali ya baridi kubwa sana. Sasa kama sisi Wizara ya Maji tutafanya mawasiliano ya karibu kabisa na wenzetu wa Wizara ya Nishati katika kuhakikisha maeneo yale hayana umeme yapelekwe umeme haraka ili wananchi wake waweze kunufaika na huduma hii muhimu sana ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu suala zima la uchimbaji wa visima hususani kwa wakala wetu wa uchimbaji wa visima DDCA maji ni uhai na sisi kama viongozi wa Wizara ya Maji hatupo tayari kupoteza uhai wa wana Hanan’g nimuombe Mheshimiwa Mbunge baada ya saa saba tukutane ili tufanye mawasiliano ya karibu na wenzetu wa DDCA waende kumchimbia visima vyake ahsante sana.